Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

Izack Mwanahapa

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2011
Posts
497
Reaction score
236
Swala la muungano wa Tanganyika na Zanzibar limekuwa likizua mijadala kila kukicha, hasa inapofikia kwenye mahali ambapo zanzibar na Tanganyika wanatakiwa kushiriki pamoja katika maamuzi makubwa ya nchi kama hili linaloendelea sasa kuhusu Muswada wa katiba.

Je kama Mtanzania unayejiamini na kujitegemea kimawazo, nini maoni yako kuhusu muungano huu?
 
Swala la muungano wa Tanganyika na Zanzibar limekuwa likizua mijadala kila kukicha, hasa inapofikia kwenye mahali ambapo zanzibar na Tanganyika wanatakiwa kushiriki pamoja katika maamuzi makubwa ya nchi kama hili linaloendelea sasa kuhusu Muswada wa katiba. Je kama Mtanzania unayejiamini na kujitegemea kimawazo, nini maoni yako kuhusu muungano huu?

Let Tanzanians themselves decide the fate of muungano, basi.
 
Siutaki!! nautaka utanganyika wangu uliozikwa kwa biriani bila nyama!
 
Muungano huu umefika pahala ambapo hauwezi kuokolewa. Lazima ufe tu, hauna dawa tena. Dawa yake alikufa nayo Mwalimu!!
 
Nadhani kabla ya maoni uengeuliza facts kuhusu muungano. Nini hatma yake Baada ya marekebisho ya Katiba ya Zanzibar mwaka jana!!!!!!!
 
Nadhani kabla ya maoni uengeuliza facts kuhusu muungano. Nini hatma yake Baada ya marekebisho ya Katiba ya Zanzibar mwaka jana!!!!!!!
Unfortunately when I think of the Union I get the following questions: 1. Why did Tanganyika unite with Zanzibar in 1964? 2. Who engineered the union and for whose benefits? 3. What is it's importance to the people of the united republic of Tanzania. 4. What is the feeling of the citizens of this great land on whether to be on union or not?
Maoni yangu yamejikita kwenye kupata majibu ya maswali yangu....
 
kabla hatujafikia muafaka wa uvunjwe au usivunjwe tuelezane 1. SABABU ZA MUUNGANO 2. Faida zake kwa pande zote mbili 3. HASARA ZAKE KWA PANDE ZOTE MBILI 3. KERO ZAKE .
 
PIA TUJUE KWANINI ZANZIBAR WALIREKEBISHA KATIBA YAO BILA KUTUSHIRIKISHA lkn kwenye yakwetu wanashirikishwa??
 
Sioni haja ya Muungano. Sanasana tunaongeza watu wa kusema ndiyooooooooo!!!!!!!!!!!!! bungeni tu. Muungano ufe, tena utokomee kabisa!
 
Ufe na ufe na ufe Zaidi..Wabunge wengine wa znz kero kubwa na sijui kama Dam zao si za kupima maana zaweza kuwa na Virus vya alqaida na na ndiyo maana wakiongea bungeni Waume zao huangalia na kutikisa vichwa kwani hawajawahi ona hivvyo kwa Wabongo
 
Mimi naona Wazanzibar waachwe waamue hatma ya nchi yao. Lakini sote tunatokana( kama wanadamu) na BABA wa BWANA yetu YESU CHRISTO. Wale tunaomwamini YESU kuwa alikufa akazikwa na siku ya tatu akafufuka kwa ajili yetu, tutakutana katika UFALME ujao wa MUNGU na wale wasioamini makao yao ni katika ziwa lile liwakalo moto na kiberiti.
 
Ni suala la kujadiliwa kwa undani na umakini. Kwa hali zote Muungano hauna faida kwa wote zaidi ya kuwapumbaza Wazanzibari na kuwadumaza kwa faida ya kundi dogo ndani ya nchi zote 2. Nawaomba Wazanzibari wasifumbwe macho na wabunge wajinga wanaoutetea bila kujali haki za wananchi.Napongeza maandamano ya Wazanzibari wanaoupinga.Huu ufe na kama tunahitaji tuunde mpya wenye mashiko.
 
Swala la muungano wa Tanganyika na Zanzibar limekuwa likizua mijadala kila kukicha, hasa inapofikia kwenye mahali ambapo zanzibar na Tanganyika wanatakiwa kushiriki pamoja katika maamuzi makubwa ya nchi kama hili linaloendelea sasa kuhusu Muswada wa katiba. Je kama Mtanzania unayejiamini na kujitegemea kimawazo, nini maoni yako kuhusu muungano huu?
Maoni yangu ni kwamba, kwa nia ya kufanya maamuzi sahihi juu ya muungano huu, ni vema tujadili uhalali wa hii serikali ya ushirikiano wa CCM na CUF zanzibar kwani ndoa hii imevunja na kuingilia misingi ya muungano.
 
Hakuna haja ya kuendelea kuishi na kiinimacho hiki kiitwwacho muungano..... kama tunautaka kwa dhati na kwa pande zote 2 then lazima kila nchi ipoteze identity (kama ilivyokuwa kwa Tanganyika) na autonomy yake (kama ilivyokubali Tanganyika) kuwe na serekali moja tu. Vinginevyo niko tayari kuingia bara barani kuupinga muungano wa kifedhuli usiokuwa na maslahi na unaoipoteza Tanganyika......
 
Ufe!ufe!ufe!ufe!ufe na utokomee kuzimu.huo ndio umetuletea wabunge wa kuzomea na kupiga meza.umepumbaza WATANGANYIKA na kuisahau tanganyika yetu kwa kukosa katiba yetu na wawakirishi ktk balaza la mapinduzi zanzibar.ushindwe na ulegeeee.
 
Kama hakuna uwezekano wa kuwa na serikali moja basi Muungano ni bora ufe tu. Maana hata USA wameungana zaidi ya mataifa 40 lakini wameweza kuwa na serikali moja. Kwa nini kwa TANZANIA iwe nongwa?? No Single Government, No Muungano
 
Maoni yangu,
1.Huu muungano wa nchi Mbili ni lazima uzalishe serikari moja(Serikari ya jamuhuri ya Muungano ya Tanzania)-ni kiini macho cha hali ya juu kuwa nchi mbili zilizoungana zinazalisha serikali mbili eti ya Muungano na ya Zanzibar,hata mtoto mdogo wa darasa la chekechea anaelewa kuwa ilitakiwa serikali moja tu au ilitakiwa serikali tatu.
2.Haki ya mtanganyika imemezwa na Muungano huu,ni lazima tuutafute utanganyika wetu(asili yetu) kwa namna yoyote ile,kila binadamu ana asili yake nasi kama watanganyika tunataka asili yetu ya kuwa mtanganyika mtanzania.
3.Mambo ya muungano yaelezwe kinagaubaga pasipo maficho yoyote yale,Tunaficha nini?
4.Ikishindikana kabisa ningependa Muungano uvunjwe na kila nchi ibaki na haki zake kama nchi.

nawasilisha
 
Swala la muungano wa Tanganyika na Zanzibar limekuwa likizua mijadala kila kukicha, hasa inapofikia kwenye mahali ambapo zanzibar na Tanganyika wanatakiwa kushiriki pamoja katika maamuzi makubwa ya nchi kama hili linaloendelea sasa kuhusu Muswada wa katiba. Je kama Mtanzania unayejiamini na kujitegemea kimawazo, nini maoni yako kuhusu muungano huu?

Kuwe na serkali Moja ima Muungano uvunjwe!
 
Back
Top Bottom