kaburunye
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 672
- 74
Nini maana ya WOZA, naomba kuulizia
Neno linanitatiza, kila nikifiria
Wale nilowauliza, jibu hawakunipatia
Nipeni maana yake, wale mnaofahamu.
Nilimwuliza ayubu, jibu hakunipatia
Akajifanya ni bubu, nilipomfuatilia
Nasemwa sina adabu, swali nikiulizia
Nipeni maana yake, wale mnaofahamu
Kwangu hili neno geni, nawaambia ukweli,
Maana yake ni nini, lijibuni langu swali
Msiingie mitini, nipeni jibu la kweli
Nipeni maana yake, kwa wale mnaofahamu
Hapa tamati nafika, mbele ninaona giza
Mwenzenu mi nimechoka, mambo yamenitatiza
kuendelea nataka, moyo unanikataza
Nipeni maana yake, kwa wale mnaofahamu
Neno linanitatiza, kila nikifiria
Wale nilowauliza, jibu hawakunipatia
Nipeni maana yake, wale mnaofahamu.
Nilimwuliza ayubu, jibu hakunipatia
Akajifanya ni bubu, nilipomfuatilia
Nasemwa sina adabu, swali nikiulizia
Nipeni maana yake, wale mnaofahamu
Kwangu hili neno geni, nawaambia ukweli,
Maana yake ni nini, lijibuni langu swali
Msiingie mitini, nipeni jibu la kweli
Nipeni maana yake, kwa wale mnaofahamu
Hapa tamati nafika, mbele ninaona giza
Mwenzenu mi nimechoka, mambo yamenitatiza
kuendelea nataka, moyo unanikataza
Nipeni maana yake, kwa wale mnaofahamu