Nini maana ya kushikilia shilingi kwenye mshahara wa Waziri?

WINGER_TEREZA

JF-Expert Member
Jul 31, 2015
242
450
Habari wanajukwaa. Naomba nijielekeze moja kwa moja kwenye mada, Kuna baadhi ya Wabunge wakiwa wanachangia mijadala kadhaa pale bungeni (hasa katika bunge hili la bajeti) Mbunge anaweza kuwa ameuliza swali fulani na kutaka majibu toka serikalini na Waziri anaweza kujibu hilo swali ila Mbunge anaweza kuwa hajaridhika na majibu hayo na utamsikia akisema "nashikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri" au baada ya kuuliza swali anaweza kuongezea kabisa kwa kusema "kama sitoridhika na majibu ya swali hili toka kwa Waziri nakusudia kushikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri".

Pia katika siku za hizi karibuni nilimsikia Spika wa Bunge, Mh Job Ndugai, alisema kuwa endapo Waziri wa fedha, Dr Mwigulu, asipotoa maelezo sahihi kwanini pesa zinazo tolewa na nchi wahisani katika kupambana na changamoto za mazingira why hazitumiki na kupelekea wakati mwingine kukaa mda mrefu hazina na hatimaye kurudishwa zilikotoka ili hali kuna uhitaji wa hizo pesa kwa sababu ya vikaa zisivyo isha huko Wizarani.

Katika hilo Spika alisema atashikilia shilingi yeye mwenyewe toka kwenye mshahara wa Waziri endapo Waziri asipokuja kutoa maelezo yakina kwanini pesa hizo za "bure" zinarudigi zilikotoka. Hapa nilipo nasubiri siku ya kuwasilishwa kwa bajeti ya Wizara ya fedha na Mipango au bajeti kuu ya serikali kama Dr Mwigulu atadadavua kwa kina suala hilo kama alivyo ahidi au atakubali shilingi yake ishikiliwe na Spika (japo ambalo sidhani kama atakubali litokee kwani mbunge tu wa kawaida akitishia kushikilia shilingi Waziri, Waziri uhaa na kutoka majibu ya kumlidhisha huyo mbunge ASAP)

Swali langu: Ni nini maana ya kushikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri? Na yapi ni madhara ya yake?

Asante.
 
Simply toka kwenye maelezo yako huo msemo unamaanisha Waziri ataulizwa swali la nyongeza.
 
Simply toka kwenye maelezo yako huo msemo unamaanisha Waziri ataulizwa swali la nyongeza.
Nadhani hujaelewa, swali lanhu ni nini maana ya hili neno la kibunge la kushikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri?. Na siyo kuulizwa swali la nyongeza.
 
Kushikilia shilingi ni kutoridhishwa na majibu ya waziri kuhusu suala fulani. Mara nyingi linakuwa limefuatiliwa kwa miaka mingi na hakuna la maana linalofanywa na serikali hivyo mbunge anaamua kusimamia haki yake ya kutaka kupatiwa suluhisho la kueleweka.

Mara nyingi wanaoshikilia shilingi huwa wanalegeza misimamo yao na bajeti zinapita. Ni kuonyesha kutoridhishwa na hatua za kiserikali za utatuzi wa suala fulani.
 
Habari wanajukwaa. Naomba nijielekeze moja kwa moja kwenye mada, Kuna baadhi ya Wabunge wakiwa wanachangia mijadala kadhaa pale bungeni (hasa katika bunge hili la bajeti) Mbunge anaweza kuwa ameuliza swali fulani na kutaka majibu toka serikalini na Waziri anaweza kujibu hilo swali ila Mbunge anaweza kuwa hajaridhika na majibu hayo na utamsikia akisema "nashikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri" au baada ya kuuliza swali anaweza kuongezea kabisa kwa kusema "kama sitoridhika na majibu ya swali hili toka kwa Waziri nakusudia kushikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri".

Pia katika siku za hizi karibuni nilimsikia Spika wa Bunge, Mh Job Ndugai, alisema kuwa endapo Waziri wa fedha, Dr Mwigulu, asipotoa maelezo sahihi kwanini pesa zinazo tolewa na nchi wahisani katika kupambana na changamoto za mazingira why hazitumiki na kupelekea wakati mwingine kukaa mda mrefu hazina na hatimaye kurudishwa zilikotoka ili hali kuna uhitaji wa hizo pesa kwa sababu ya vikaa zisivyo isha huko Wizarani. Katika hilo Spika alisema atashikilia shilingi yeye mwenyewe toka kwenye mshahara wa Waziri endapo Waziri asipokuja kutoa maelezo yakina kwanini pesa hizo za "bure" zinarudigi zilikotoka. Hapa nilipo nasubiri siku ya kuwasilishwa kwa bajeti ya Wizara ya fedha na Mipango au bajeti kuu ya serikali kama Dr Mwigulu atadadavua kwa kina suala hilo kama alivyo ahidi au atakubali shilingi yake ishikiliwe na Spika (japo ambalo sidhani kama atakubali litokee kwani mbunge tu wa kawaida akitishia kushikilia shilingi Waziri, Waziri uhaa na kutoka majibu ya kumlidhisha huyo mbunge ASAP)

Swali langu ni nini maana ya kushikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri?.. na yapi ni madhara ya yake?. Asante.
Msemo huo umekuwepo tangu enzi za Mwalimu. Lakini hawasemi wanashikilia shilingi kwenye mshahara wa waziri. Wanachosema ni kutoa shilingi kwenye bajeti iliyowasilishwa na waziri. Kwa mfano waziri amepanga bajeti ya shilingi bilioni moja kwa shughuli za wizara yake kwa mwaka wa fedha unaokuja. Ukiondoa shilingi ina maana kunakuwepo na pengo na alichopanga waziri hakitafanikiwa. Kwa hiyo waziri anabidi ainusuru hiyo shilingi ili aliyopanga yaendelee. Neno shilingi ni msemo tu wa kumaanisha anaweka pengo kwenye bajeti ya wizara. Si kwamba mbunge anamaanisha shilingi moja kweli.
 
Msemo huo umekuwepo tangu enzi za Mwalimu. Lakini hawasemi wanashikilia shilingi kwenye mshahara wa waziri. Wanachosema ni kutoa shilingi kwenye bajeti iliyowasilishwa na waziri. Kwa mfano waziri amepanga bajeti ya shilingi bilioni moja kwa shughuli za wizara yake kwa mwaka wa fedha unaokuja. Ukiondoa shilingi ina maana kunakuwepo na pengo na alichopanga waziri hakitafanikiwa. Kwa hiyo waziri anabidi ainusuru hiyo shilingi ili aliyopanga yaendelee. Neno shilingi ni msemo tu wa kumaanisha anaweka pengo kwenye bajeti ya wizara. Si kwamba mbunge anamaanisha shilingi moja kweli.
Asante Mkuu
 
Kushikilia shilingi ni kutoridhishwa na majibu ya waziri kuhusu suala fulani. Mara nyingi linakuwa limefuatiliwa kwa miaka mingi na hakuna la maana linalofanywa na serikali hivyo mbunge anaamua kusimamia haki yake ya kutaka kupatiwa suluhisho la kueleweka.

Mara nyingi wanaoshikilia shilingi huwa wanalegeza misimamo yao na bajeti zinapita. Ni kuonyesha kutoridhishwa na hatua za kiserikali za utatuzi wa suala fulani.
Asante, vipi ishawahi kutokea Mbunge akashikilia shilingi na akagoma kuiachia?.. vipi ikitokea hali hiyo bajeti ya hiyo Wizara itapita au inakwama?.. au kwa kuwa tuna maspika kama Job ataipitisha kwa lazima kama wale Covid 19😄😄😄
 
Nadhani hujaelewa, swali lanhu ni nini maana ya hili neno la kibunge la kushikilia shilingi toka kwenye mshahara wa Waziri?. Na siyo kuulizwa swali la nyongeza.
Swali la nyongeza huja pale ambapo mbunge hajaridhika na majibu ya Waziri, kama ameridhika hawezi ongeza swali jingine.
 
Asante, vipi ishawahi kutokea Mbunge akashikilia shilingi na akagoma kuiachia?.. vipi ikitokea hali hiyo bajeti ya hiyo Wizara itapita au inakwama?.. au kwa kuwa tuna maspika kama Job ataipitisha kwa lazima kama wale Covid 19😄😄😄
Ilitokea miaka ya nyuma enzi za spika akiwa Pius Msekwa lakini waziri wa wizara husika aliweza kumridhisha mbunge na shilingi ikaachiwa.
 
Back
Top Bottom