Nchini, kama wasipoongeza juhudi za kusifia na kupiga kelele kama walivyo amriwa, jina litazimika mazima, zaidi ya 80% watasahau kama kuna mtawala!
Ni mwendo wa kiki na kushtua kijoti, "safirisha wanyama, sikilizia, imevuma ila haina kwere, izime hewani, endeleeni off-air", limeisha hilo.
"Bwawa kubwa mno, lingechukua miaka mitano", wenyewe kiiiiimya, hakuna ngendembwe, simamisha, fufua miradi yetu, tuuze umeme tanesco, limeisha.
"Tengeneza timu ya kutoa maoni ya msaafu, idhinisha bulungutu tugawane, nani anakumbuka bulungutu la bunge la msaafu? kimyaaa, hakuna wa kuuliza kwanini pesa mingi zitumike kwa jambo lile lile", imekwenda hiyo.
"Safari zangu ni za manufaa kwa ardhi hii", gharama yake vs manufaa? Hakuna anayejua, kila mtu kapata mgao wake, si mlitaka safari, na kwa taarifa yenu tumeongeza PADIEMU. Sawa, tuendelee kuhondomola.
"Tunaajiri maelfu kwa mamia elfu", tija ikibaki pale pale, pato haliongezeki, nani wa kuhudumia wage bill kwa watumishi hawa wanaenda kujawa na urasimu, upigaji, kukosa maadili na kutokuwajibika? Jibu ni Tozo, Ajira na madaraja oyeee, tusonge mbele!
"Baada ya kuachiwa na kuingia jengo jeupe mara kadhaa", nina imani nae! Ni makosa kusema ya kikao hadharani, ni shujaa!
"Nimelipwa madeni yangu yote", marehemu hafai kabisa.
"Mentor wangu karudi, mi mwenyewe nimekalia kiti, kupiga goti kitu gani", Mungu kaamua ugomvi
"Mama amepewa tuzo kwa kujenga miundo mbinu, Mama - anayestahili hayupo", alipo mama, vijana tupo!
"Bilioni 600s tulizolipwa na akashia, kwanini tusilipwe kwa kadiri ya makubaliano?", ooonho, nani kamtuma aropeke, pesa yenyewe kwanza ipo basi. Kidumu.