Nini maana ya hizi tofauti?

Nini maana ya hizi tofauti?

RNA

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2013
Posts
1,692
Reaction score
2,860
Habari ,Hivi wanaJF kuna nini Nyuma ya Tofauti hizi Mbili ambazo ziko wazi zinajionyesha :-

1. Mitaani watu wanamkubali Sana Hayati JPM kuliko Mitandaoni .

2. Mitaani wanaona kuna Ugumu wa maisha na tunapotea Mitandaoni idadi kubwa wanaona tunarudi kwenye mstari na tunaenda vizuri.

Binafsi nimefuatilia sana nimekosa Jibu Hasa kwenye huu mlinganisho wa hizi Awamu .
 
Mbona mi naona kama hayo ndo majibu, au kuna la ziada?
 
Mtaani ni wamachinga,mama ntilie,mnaonaje nimtumbue????? Ambao hata report ya CAG hawajui ni kitu gani, mtandaoni ni watu wa fact they know each and everything, kiufupi cake 🍰 ya taifa ni kubwa acha kila mtu afaidike nayo
 
Jibu ni namba moja,kumpata mtu kama magu itachukua miaka hata mia,kwenye mtandao mfano jf wengi wanaogopa kumsifia kwa kuogopa kutukanwa ila ukweli ndio huo.
Mitaani watu wamelewa propaganda za magu na uelewa wa Mambo ya nchi ni duni..hawajui FDI,gdp Wala nini,wao Mambo kuwa magumu Leo hawadhani ni athari za magu..magu ilikua ajali kubwa ya kisiasa kupata kutokea nchi hii
 
Nchini, kama wasipoongeza juhudi za kusifia na kupiga kelele kama walivyo amriwa, jina litazimika mazima, zaidi ya 80% watasahau kama kuna mtawala!

Ni mwendo wa kiki na kushtua kijoti, "safirisha wanyama, sikilizia, imevuma ila haina kwere, izime hewani, endeleeni off-air", limeisha hilo.

"Bwawa kubwa mno, lingechukua miaka mitano", wenyewe kiiiiimya, hakuna ngendembwe, simamisha, fufua miradi yetu, tuuze umeme tanesco, limeisha.

"Tengeneza timu ya kutoa maoni ya msaafu, idhinisha bulungutu tugawane, nani anakumbuka bulungutu la bunge la msaafu? kimyaaa, hakuna wa kuuliza kwanini pesa mingi zitumike kwa jambo lile lile", imekwenda hiyo.

"Safari zangu ni za manufaa kwa ardhi hii", gharama yake vs manufaa? Hakuna anayejua, kila mtu kapata mgao wake, si mlitaka safari, na kwa taarifa yenu tumeongeza PADIEMU. Sawa, tuendelee kuhondomola.

"Tunaajiri maelfu kwa mamia elfu", tija ikibaki pale pale, pato haliongezeki, nani wa kuhudumia wage bill kwa watumishi hawa wanaenda kujawa na urasimu, upigaji, kukosa maadili na kutokuwajibika? Jibu ni Tozo, Ajira na madaraja oyeee, tusonge mbele!

"Baada ya kuachiwa na kuingia jengo jeupe mara kadhaa", nina imani nae! Ni makosa kusema ya kikao hadharani, ni shujaa!

"Nimelipwa madeni yangu yote", marehemu hafai kabisa.

"Mentor wangu karudi, mi mwenyewe nimekalia kiti, kupiga goti kitu gani", Mungu kaamua ugomvi

"Mama amepewa tuzo kwa kujenga miundo mbinu, Mama - anayestahili hayupo", alipo mama, vijana tupo!

"Bilioni 600s tulizolipwa na akashia, kwanini tusilipwe kwa kadiri ya makubaliano?", ooonho, nani kamtuma aropeke, pesa yenyewe kwanza ipo basi. Kidumu.
 
Mtandaoni watu wako obsessed na chuki tu zinawasumbua. Kiukweli hali iko tight hakuna mfano.

Wengi wasiokuwa na elimu kubwa pia hawana kazi maalumu ndio wanaumizwa.
Labda ambao wanaona hali iko shwari nadhani ni wale ambao wako serikali na walamba asali.

Na kikubwa kinachoumiza ni hii kula kulingana na urefu wa kamba. Watu ni wanavimbiwa. Mfano hizi taasisi za serikali wanawakamua sana mafundi kwenye miradi mbalimbali ujira ni mdogo ukilinganisha na fedha ambayo iko allocated.

Ila all in all huenda hali itatulia hapo baadaye. Tuwe wavumilivu.
 
Mtandaoni huku ipo ile timu ya praise and worship wamemwagwa ukimsifia tu magufuli unatukanwa na kukejeliwa kisha wao wana sign out na kwenda kuchukua buku 7 zao

Ila ukweli mchunguTanzania itachukua miaka bilioni 6 kumpata kiongozi kama magufuli

Kwa miaka hiyo wewe ndugu unayesoma hii comment pamoja na mimi mifupa yetu itakua imesagika ardhini na kua mbolea laini mara laki saba ya unga wa ngano
 
Mtaani wapi unazungumzia, mbona Mtaani kwetu hatujakuona kupita kukusanya maoni, taja mitaa uliyofanyia utafiti wako usijumuishe mitaa yote
 
Mitaani watu wamelewa propaganda za magu na uelewa wa Mambo ya nchi ni duni..hawajui FDI,gdp Wala nini,wao Mambo kuwa magumu Leo hawadhani ni athari za magu..magu ilikua ajali kubwa ya kisiasa kupata kutokea nchi hii
huna point ya maana kifupi mi namkubali magu.
 
Habari ,Hivi wanaJF kuna nini Nyuma ya Tofauti hizi Mbili ambazo ziko wazi zinajionyesha :-

1. Mitaani watu wanamkubali Sana Hayati JPM kuliko Mitandaoni .

2. Mitaani wanaona kuna Ugumu wa maisha na tunapotea Mitandaoni idadi kubwa wanaona tunarudi kwenye mstari na tunaenda vizuri.

Binafsi nimefuatilia sana nimekosa Jibu Hasa kwenye huu mlinganisho wa hizi Awamu .
Mtandaoni mafisadi wana machawa kibao kwa ajili ya kudhihaki kila lililo jema alilolifanya The late Jpm kuwatetea raia.

Na uyasikiayo mitaani ndiyo sura halisi ya Tz ilivyo kwa sasa, ni kama moto wa kinyesi cha ng'ombe unawaka mumo kwa mumo, ukiugundua utakuwa umechelewa, maana ulishateketeza kika kitu.
 
Mtaani ni wamachinga,mama ntilie,mnaonaje nimtumbue????? Ambao hata report ya CAG hawajui ni kitu gani, mtandaoni ni watu wa fact they know each and everything, kiufupi cake ya taifa ni kubwa acha kila mtu afaidike nayo
Acha matusi, mkulima anafaidi keki ya taifa?
Embu fafanua.
 
Nchini, kama wasipoongeza juhudi za kusifia na kupiga kelele kama walivyo amriwa, jina litazimika mazima, zaidi ya 80% watasahau kama kuna mtawala!

Ni mwendo wa kiki na kushtua kijoti, "safirisha wanyama, sikilizia, imevuma ila haina kwere, izime hewani, endeleeni off-air", limeisha hilo.

"Bwawa kubwa mno, lingechukua miaka mitano", wenyewe kiiiiimya, hakuna ngendembwe, simamisha, fufua miradi yetu, tuuze umeme tanesco, limeisha.

"Tengeneza timu ya kutoa maoni ya msaafu, idhinisha bulungutu tugawane, nani anakumbuka bulungutu la bunge la msaafu? kimyaaa, hakuna wa kuuliza kwanini pesa mingi zitumike kwa jambo lile lile", imekwenda hiyo.

"Safari zangu ni za manufaa kwa ardhi hii", gharama yake vs manufaa? Hakuna anayejua, kila mtu kapata mgao wake, si mlitaka safari, na kwa taarifa yenu tumeongeza PADIEMU. Sawa, tuendelee kuhondomola.

"Tunaajiri maelfu kwa mamia elfu", tija ikibaki pale pale, pato haliongezeki, nani wa kuhudumia wage bill kwa watumishi hawa wanaenda kujawa na urasimu, upigaji, kukosa maadili na kutokuwajibika? Jibu ni Tozo, Ajira na madaraja oyeee, tusonge mbele!

"Baada ya kuachiwa na kuingia jengo jeupe mara kadhaa", nina imani nae! Ni makosa kusema ya kikao hadharani, ni shujaa!

"Nimelipwa madeni yangu yote", marehemu hafai kabisa.

"Mentor wangu karudi, mi mwenyewe nimekalia kiti, kupiga goti kitu gani", Mungu kaamua ugomvi

"Mama amepewa tuzo kwa kujenga miundo mbinu, Mama - anayestahili hayupo", alipo mama, vijana tupo!

"Bilioni 600s tulizolipwa na akashia, kwanini tusilipwe kwa kadiri ya makubaliano?", ooonho, nani kamtuma aropeke, pesa yenyewe kwanza ipo basi. Kidumu.
Mauzauza hoyee!!!
 
Mitandaoni kuna wale walioishi km mashetani,mtaani kuna watu wa hali ya chini wengi hawajui kinachoendelea huku ambao Aliwatetea sana kipindi chake.
 
JPM ameshakufa, yes inawezekana alikuwa na mazuri yake....hayupo sasa tunafanyeje? tuendelee kuishi tu oooooh JPM JPM, tunafanya nini sasa sisi tulio hai?, amefanya yake amekwenda...
 
Mtandaoni mafisadi wana machawa kibao kwa ajili ya kudhihaki kila lililo jema alilolifanya The late Jpm kuwatetea raia.

Na uyasikiayo mitaani ndiyo sura halisi ya Tz ilivyo kwa sasa, ni kama moto wa kinyesi cha ng'ombe unawaka mumo kwa mumo, ukiugundua utakuwa umechelewa, maana ulishateketeza kika kitu.
Wazee wa buku 7
 
Back
Top Bottom