Nini maana ya hadhi ya ubalozi?

Nini maana ya hadhi ya ubalozi?

NostradamusEstrademe

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2017
Posts
3,840
Reaction score
5,097
JF Ni darasa la kuelimishana

Hivi karibuni Humphrey Polepole kanyang'anywa hadhi ya kibalozi na mama yetu wa taifa SSH
Wibroad Slaa naye kuna wakati alisema na ubalozi wenu chukueni.

Je mtu akinyang'anywa hiyo hadhi ni kipi anakosa hata kama sio balozi tena maana anakuwa hawajamkata kichwa.

Na je na ambaye ameshastaafu lakini hakunyang'anywa hiyo hadhi ni kitu gani bado anafaidika nacho?

Naomba weledi waje
 
Write your reply...nokia 230 via opera mini =jamii forum without vpn.#october tunatick
 
Mimi ninafahamu chache tu ambazo nimekuwa naziona kwa hao wanadiplomasia aidha awe balozi au waambata wao.

Mojawapo ni kinga[immunity] ulinzi kuhusu mashtaka uwapo nje /ndani ya eneo la kazi ndio maana Dr Slaa alipotaka kushtakiwa kwa kesi ya uhaini wa kubumba baada ya kupinga mkataba wa DP World alivuliwa kwanza ubalozi.

Wanafanya manunuzi ya bidhaa katika maduka maalum ya kidiplomasia ambayo bidhaa zake hazina ushuru [duty free] hii ni kudumisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi na nchi kupitia mikataba ya kimataifa ya kidiplomasia mfano duka la wananchi kawaida bidhaa yaweza kuwa $3 kule kwenye maduka ya kidiplomasia unakuta ni $1.99

Pasi maalum ambayo inawapa nafasi kuhudumiwa haraka wawapo katika majukumu yao ya kikazi na safari [fast track]

Nyingine ni posho kadhaa kama makazi, umeme, chakula, mavazi , internet na kadhalika.
 
Kama hajapokonywa hadhi basi anabaki nayo mpaka kifo na atajulikana kama balozi mstaafu
Hapo sawa nimepata jibu kumbe ndio maana yule mzee huwa anaheshimika sana na ni mwenyekiti au member wa board mbali mbali.
Na anavyoishi japo kastaafu utadhani bado yuko kwenye ajira.
Kumbe basi uwaziri hauna issue bora mtu uwe balozi ukistaafu heshima bado ipo
Kuna waziri mmoja wa zamani mtaani tulikuwa tunakunywa naye ugimbi na dengelua sasa ni marehemu tena anatokea huko kwenu.
 
Hapo sawa nimepata jibu kumbe ndio maana yule mzee huwa anaheshimika sana na ni mwenyekiti au member wa board mbali mbali.
Na anavyoishi japo kastaafu utadhani bado yuko kwenye ajira.
Kumbe basi uwaziri hauna issue bora mtu uwe balozi ukistaafu heshima bado ipo
Kuna waziri mmoja wa zamani mtaani tulikuwa tunakunywa naye ugimbi na dengelua sasa ni marehemu tena anatokea huko kwenu.
Balozi Amy Mpungwe?
 
Back
Top Bottom