Nini maana ya ELIMU .?

Nini maana ya ELIMU .?

NestoryJ

Senior Member
Joined
Jun 3, 2017
Posts
117
Reaction score
132
Habari ya kwako ewe mTanzania unaesoma na kuutizama Uzi huu, ningependa kupata ushirikiano toka kwako juu ya swala hili ambalo nimekuwa nikijiuliza siku nyingi pasipo kupata ufumbuzi.

Wanasema palipo na ushirikiano ndipo mahala palipo na kuijenga hoja kuwa yenye tija na kimkakati kutokana na muunganyiko Wa mawaidha na maoni mbalimbali kutoka Kwa wadau wenye kuidadavua mada.

Nimekuwa nikipita sehemu nyingi na kuona maana mbalimbali ya ELIMU wengine kuinadi kama
-> elimu ni Mali
-> elimu ni bahari
-> elimu ni rasilimali
-> elimu ni ufunguo wa maisha
-> elimu ni ukombozi
-> elimu ni uhai
-> elimu ni fumbo la ujinga n.k

Ajabu ni kwamba maana hizi zote za elimu huwapo katika taasisi zinazojihusisha na maswala ya kuipata elimu.

Je!, yawezekana kuwapo na maana moja ambayo hubeba tafsiri nzima ya neno ELIMU .?
Naamini wazi hapa kuwa wapo watu wenye mawazo chanya na yenye kuleta kitu kimoja ambacho kitawakilisha maana harisi ya neno ELIMU na kunifumbua macho juu ya jambo hili ambalo nimekuwa nikijiuliza pasipo kuwa na jibu sawia

Karibu Kwa hoja ........
 
Habari ya kwako ewe mTanzania unaesoma na kuutizama Uzi huu, ningependa kupata ushirikiano toka kwako juu ya swala hili ambalo nimekuwa nikijiuliza siku nyingi pasipo kupata ufumbuzi.

Wanasema palipo na ushirikiano ndipo mahala palipo na kuijenga hoja kuwa yenye tija na kimkakati kutokana na muunganyiko Wa mawaidha na maoni mbalimbali kutoka Kwa wadau wenye kuidadavua mada.

Nimekuwa nikipita sehemu nyingi na kuona maana mbalimbali ya ELIMU wengine kuinadi kama
-> elimu ni Mali
-> elimu ni bahari
-> elimu ni rasilimali
-> elimu ni ufunguo wa maisha
-> elimu ni ukombozi
-> elimu ni uhai
-> elimu ni fumbo la ujinga n.k

Ajabu ni kwamba maana hizi zote za elimu huwapo katika taasisi zinazojihusisha na maswala ya kuipata elimu.

Je!, yawezekana kuwapo na maana moja ambayo hubeba tafsiri nzima ya neno ELIMU .?
Naamini wazi hapa kuwa wapo watu wenye mawazo chanya na yenye kuleta kitu kimoja ambacho kitawakilisha maana harisi ya neno ELIMU na kunifumbua macho juu ya jambo hili ambalo nimekuwa nikijiuliza pasipo kuwa na jibu sawia

Karibu Kwa hoja ........


Mkuu kwa maoni yangu maana zote hizo ni sawa na aghalabu kila moja hutumiwa katika mahali husika. Unaweza kufupisha kwa maneno haya:-

Elimu ni ujuzi/kipawa ambacho mtu amejifunza au amezaliwa nacho na anaweza kutumia kwa ajili ya manufaa yake na jamii kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom