Nini lengo la HR anapokuuliza hili swali?

Nini lengo la HR anapokuuliza hili swali?

Mbishi 4 real

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2014
Posts
640
Reaction score
655
Habari wapendwa,

Nini lengo la HR anapokuuliza "What is your salary expectations ? " ilihari anajua fika kwamba kampuni yake ina salary scale ya kila position
 
hapana kampuni siyo zote zina scale hivyo yeye akikupata mfanyakazi wa bei rahisi mno bosi humpongeza kwa kupata poyoyo let say ilibidi wakulipe 1.3M lakini wewe ukasema 0.85M itakutosha kuna kuwa na saving ya pesa hapo kama 0.45M na mpaka uje ufikie hiyo 1.3M ni mda sana wanakua wamekutumia mno!
 
Si ulitaje

Mwambie according to scale salary ya kampuni anayolipa kwa wafanyakazi wa level yako Ila Kama unajua scale anayolipa kwa wafanyakazi wa level yako unamwambia iyo iyo or unaongeza kidogo hope umeelewa
 
Jibu hv hata mshahara wa mwalim wa primary(ngaz ya cheti) anayeanza kaz utakutosha kw kuwa huna namna nyngne zaid ya kukubal matokeo tu
 
Mwambie according to scale salary ya kampuni anayolipa kwa wafanyakazi wa level yako Ila Kama unajua scale anayolipa kwa wafanyakazi wa level yako unamwambia iyo iyo or unaongeza kidogo hope umeelewa

Yes kuongezea kabla hujaenda kufanya interview make sure unapata profile ya mahali hapo ikiwa pamoja na mishahara wanalipa vipi ndio maana nikamwambia ni jibu ni simple tu.
 
Habari wapendwa,

Nini lengo la HR anapokuuliza "What is your salary expectations ? " ilihari anajua fika kwamba kampuni yake ina salary scale ya kila position

If your expectation is too higher compared to company scale they better leave you even if you are qualified
 
Ukweli ni kuwa, lengo la swali hilo ni kutaka kubaini iwapo unafahamu "thamani ya post uliyoiomba".

Ukiulizwa swali kama hilo, lazima uwe mjanja sana. Ni bora utaje kiwango kikubwa kuliko kuwa too low. Kwa Tanzania, kwa fresh graduate tuna expect ukiulizwa swali hilo uta-range Tsh 900,000 hadi 1.5m

Chonde Chonde, usiwe too cheap. Kuwa cheap inajenga dhana kuwa aidha hujiamini au uliingia kazini utakuwa mwepesi kupokea rushwa au kuiba mali za ofisi.

Na ukisema, nilipwe kama salary scale ya kampuni husika, inajenga picha kuwa pindi ukipata kazi, utakuwa mlalalimishi.

Binafsi nimekuwa katika panel za usaili kwa miaka mitatu sasa.
 
I think ni vema u study kwanza wanalipaje na ujiandae kwa hilo swali......dont be specific say around figure flan.........
 
Si ulitaje


Kikubwa ktk swali hili, HR anataka kujua km mhusika ana uelewa wowote wa viwango VYA mishahara kwa kazi km hii.

Pili, hr anataka apate mwanga km kampuni inaweza kukidhi matarajio ya kimshahara ya mfanyakazi huyu.

Si kweli kwamba utalipwa kulingana na ulichotamka hata km ulijishusha! Utalipwa kulingana na budget yao.

CHA msingi ni kwamba, majibu ya swali hili, hayatamnyima mtu kazi km alikidhi vigezo!
 
Kuna swali mshahara wako wa mwisho ni kiasi gani?

Hii nayo wakati mwingine inakatisha tamaa kama utakuwa mkubwa kuliko kazi unayoomba
 
Habari wapendwa,

Nini lengo la HR anapokuuliza "What is your salary expectations ? " ilihari anajua fika kwamba kampuni yake ina salary scale ya kila position

Ukiona linakuzingua, waambie unalipwa ngapi huko unakofanya kazi sasa (au most recent employment). Kutoka hapo unaweza kutaja amount unayotaka na panelist wengine wanaweza kukutight ujustify kwa nini unaexpext nyingi zaidi. Kuwa mkweli maana niliwahi kuombwa salary slip ya kazi yangu ya nyuma.
 
Habari wapendwa,

Nini lengo la HR anapokuuliza "What is your salary expectations ? " ilihari anajua fika kwamba kampuni yake ina salary scale ya kila position



Lengo la HR anapokuuliza ni kiwango gani cha mshahara ungependelea kulipwa kwanza ni kupimwa jinsi gani unajiamini na uwezo ulionao (competency, talent and skills) ambao unaenda kuwekeza katika company.

Pili wengi hutaka kujua "if high salary is the only source of motivation and satisfaction to u

Na endapo ntakutana na swali hilo kwenye interview najibu " ningependa kulipwa kiwango kulingana na utendaji wangu, ujuzi, thamani na mchango nitakaoleta katika taasisi "
 
Back
Top Bottom