Nini kipimo cha elimu ya mtu?

donniebrasco

JF-Expert Member
Joined
Aug 8, 2013
Posts
887
Reaction score
774
Habari ndugu zangu.

Kuna jambo moja kubwa sana hususani hapa Tanzania naomba tusaidiane kuelewishana. Nini kipimo cha elimu ya mtu? Elimu ya mtu huwezi kupima tu kwa kiwango cha mfumo tuliowekewa na uliozoeleka. Ni kwa namna ipi tunaweza kupima elimu ya mtu?

Maana kuna baadhi ya watu ambao mimi binafsi nawajua, wanakuwa kweli wana elimu ambayo inawatosheleza; ila ni elimu inayo wasaidia wao kuweza kufanya kazi zao tu (yani 'professions).

Tukifuata mfumo huu huu mfumo wa elimu yani sekondari na vyuoni; kwa upande mwingine kuna watu ambao wamesoma kidogo tu yani basic kama ni "O" level au "A" level tu na hawakwenda elimu za juu (Vyuoni) - lakini wana upeo mkubwa sana wa kuelewa vitu na kuchanganua mambo binafsi. Hao pia nimekutana nao. Nafikiri ndugu zangu mmenielewa ninachomaanisha.

Sasa je tutumie kigezo gani kujua uwezo wa kielimu wa mtu alionao? Tuangalie level aliyofikia au tuangalie kila siku ya maisha yake anaweza vipi kuishi katika jamii na kufanya kazi zake? Au kuna kigezo ambacho nyie wenzangu mnaona kinaweza kutumika kuelewa zaidi kiwango cha elimu?

Narudia mimi binafsi nimekutana na vijana ambao wameishia tu "O" level lakini wako very smart kiasi unaweza kufikiri ana masters na pia makazini wanakuwa wako very sharp hata katika mambo mengine mbali mbali na pia nimeona wengine ambao wamepata masters lakini kuna mambo mengi wanashindwa kukabiliana nayo au hata kuchanganua vitu.

Naomba mawazo na michango yenu.

CC: gfsonwin, Maganga Mkweli, Kiranga, Nicas Mtei, Mentor, Mtambuzi, Smile, lara 1, MziziMkavu (Karibuni wakuu)
 
Last edited by a moderator:
Am currently watching Sir Ken Robinson and his speeches on 'Changin education from bottom to top' 'How schools kill creativity' and 'Changing education paradigms'.

When I am done i sure will share with you something on 'Kipimo cha elimu'


PM Moderator,
Mentor.
 
kuweza kupambanua mambo .. kuyakabili vyema mazingira yanayomzungukuka..
 
1. Persobal morality and codes of ethics...
2.self determination and awareness
3.competence in social arena
4.wise judgements
Nk nk nk...
 
mwenye elimu ni yule mwenye kufanya jambo mahali pake na kwa wakati wake.
 
Binafsi huwa nawakubali sana watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri ambao haufungamani na upande wowote. Ufikiri wake ni ule unaomuwezesha kufikiria jambo na kulipambanua hadi likafikia mwisho wake na hatimaye kupata suluhisho la tatizo lililokuwa likimkabili katika mazingira yake. Ufikiri huo ni ule unaolenga pande zote yaani mlengo hasi na mlengo chanya ambao hautomfanya muhusika kujutia maamuzi yake. Mfano, wengi huwa tunakuja kutambua baadaye kuwa la hasha, ningefanya hivi yasingetokea haya!
 
Kipimo cha elimun ya mtu ni matendo yake kama ilivyosemwa awali.

Kwa mfano, Andrew Chenge ni mwanasheria (wanaojiita "wasomi"). Kasoma mpaka Harvard.

Lakini habari ya "vijisenti tu" imeonesha hajaelimika.
 

Niliona speech yake moje kwenye TED talk. Anasema mambo ya ukweli. Kwa kuongezea tuu. Adam Smith alisema kuwa ufanye ongezeko la uzalishaji ni muhimu kugawanya process ya uzalishaji katika sections ndogondogo ambazo zitakuwa specialized.

Miaka ya zamani, hili mtu ajifunze ilibidi aenze kwa maestro na kuwa apprentice na kujifunza. Muda wa kujifunza ulitegemea juhudi za mwanafunzi, kipaji na juhudi za maestro. Kwa mfano wanafalsa wa kigiriki walijifunza kwa maestro. Wasanii wa kitaliano wajifunza kwa maestro.

Mtindo huu ulitoa watu mahiri lakini wachache sana na sehemu kubwa ya umma ilibakia kizani. Wakati wa mapinduzi ya viwanda na kuendelea. Processes za ufundishaji ziligawanya kama vile processes za uzalishaji hili kuongeza idadi ya watu wenye elimu. Na mitaala ikaanza kutumika kuelezea ni kitu gani mtu ajifunze katika umri gani.


Hivyo kwa sehemu kubwa ya jamii, kipimo cha elimu ni masterly ya kilichomo kwenye mitaala. Na hii imeendelea mpaka kwenye elimu ya juu.
 
Mtazamo wangu ni kwamba kufuatia aina mbili za elimu:

Rasmi - kipimo chake ni vyeti vitolewavyo na taasisi iliyo rasmi na iliyosajiliwa

Isiyo rasmi - kipimo chake ni accomplishment alizopata mhusika na zikaonwa na wengine

Kwamba watu wasichanganye na walioelimika ila hawatumii elimu zao.
 
donniebrasco tatizo lako unachanganya IQ (intelligence quotiet) na EQ (emotional intelligence quotience)!
...
Kuna msemo unasema kumaliza mabanda si kuelimika! Bado unaukumbuka huu?
...
IQ ni uwezo wa kiakili unaomuezesha mtu kuweza kuelezea mambo kwa kina na nguvu ya kukremu!
Mtu mwenye IQ kubwa anakuwa hatari sana kwenye mambo ya academic! Kama unasoma nae unaweza ukajiuliza mara mbili mbili: "ivi uyu mtu uelewa alichotea mwenyewe nini?!!!"
...
EQ ni uwezo wa mtu kujitathmini na kutathmini wengine na kuwa na uwezo wa kuishi ktk mazingira yoyote! Mtu mwenye EQ kubwa anakuwa anajiamini, anacreativity power (mbunifu)
...
So, ni bora kuwa na EQ kuliko IQ! Mwenye IQ kubwa ndio hao unaowaongelea wewe, anaweza hata kuwa Profesa but akaact kama katoto kadogo vile! While mwenye EQ anakuwa makini sana, tena ni rahisi kufanikiwa kimaisha!
...
Sjui nimeeleweka hapa!
 
Last edited by a moderator:
ASanteeeee! mmetutia moyo hata sisi wa darasa la saba
japo hatukutajwa na mtoa maada safiiii
tutakutana hukuhuku uswazi wewe na mi masters yako
una ki rav4 cha mkopo wenzio tuna 7 au 4 tuna enda show room
na kulipa cash!
 
ASanteeeee! mmetutia moyo hata sisi wa darasa la saba
japo hatukutajwa na mtoa maada safiiii
tutakutana hukuhuku uswazi wewe na mi masters yako
una ki rav4 cha mkopo wenzio tuna 7 au 4 tuna enda show room
na kulipa cash!
kuna jamaa mmoja hivi alikuwa anafanya kazi katika machimbo ya madini.. basi katika kufanya kazi hiyo ya madini, kama mnavyojua, pesa huja fasta sana, jamaa kuona vile, akaenda S.A kutumbua maisha kwa pesa alizopata...

kufika kule bondeni, kama kawaida akaanza kula nguvu zake akiwa na sketi mbali mbali,
basi siku moja katika mizunguko yake, akakutana na jamaa akiwa analinadi gari lake kimya kimya, gari aina ya jaguar!

kama kawaida mchimba madini kwa vile alikuwa na pesa, akamwaga mchuzi akanunua gari!... aliponunua gari na kuanza kuitumia kama wiki mbili hivi, la haula! kumbe gari ile ilikuwa inakula sana fuel, mafuta yalikuwa yananyweka kuliko gari nyingine za kawaida!

Siku si siku, pesa zikaanza kumuishia jamaa, hakuwa na namna nyingine ya kumuingizia kipato mjini pale, gari aliyonunua imekuwa chanzo cha umasikini wake.

Tafakari mkuu.
 
Kipimo cha elimun ya mtu ni matendo yake kama ilivyosemwa awali.

Kwa mfano, Andrew Chenge ni mwanasheria (wanaojiita "wasomi"). Kasoma mpaka Harvard.

Lakini habari ya "vijisenti tu" imeonesha hajaelimika.


Its too low!!

Kusema ni vijisenti was just a comparison...

Wewe unavyosemaga una hela nyingi au unafanya shoping ya hela nyingi sana ni kuto kuelimika?

Sikutegea analysis hii toka kwako..

Again its too low!!
 
ASanteeeee! mmetutia moyo hata sisi wa darasa la saba
japo hatukutajwa na mtoa maada safiiii
tutakutana hukuhuku uswazi wewe na mi masters yako
una ki rav4 cha mkopo wenzio tuna 7 au 4 tuna enda show room
na kulipa cash!


Hizo ni kauli za wivu na majuto...

inaonesha hukuishia la saba kwa kupenda isipokuwa elimu ilikushinda na hapa unajifariji bure nani kakwambia kila mtu aliyesoma anatumia gari ya mkopo?

Elimu inatupa channels.. fursa kibao na madili kibao watu tunamiliki magari yasiyolingana na mishahara yetu na hatukukopa hapa utasemaje??

Ni vizuri ungechangia kuonesha uwezo na si kukandya tuu waliosoma...
 
Its too low!!

Kusema ni vijisenti was just a comparison...

Wewe unavyosemaga una hela nyingi au unafanya shoping ya hela nyingi sana ni kuto kuelimika?

Sikutegea analysis hii toka kwako..

Again its too low!!

It's too low like a Lamborghini, I never learned to fly.

Ukitegemea chochote kutoka kwangu hujanielewa bado, you can't put me in a box.

Vijisenti ilikuwa comparison na nini? Katika nchi ambayo wakulima wengi tu hawamake hata $1000 kwa mwaka, kuita half a million quid zilizopo Jersey Island "vijisenti" ni dharau ya hali ya juu.

Andrew Chenge kama mwanasiasa wa nchi yenye watu maskini ambayo GDP per capita yake haifiki hata $ 2,000 kwa mwaka kuita quid nusu milioni "vijisenti" ni matusi yaliyokimbilia kufuru.

Paul "Kishamapanda" Bomani alikuwa na hela ndefu kuanzia kabla ya uhuru, lakini huwezi kukuta rekodi anasema hela ambayo wananchi wa kawaida wanaona ni utajiri kuwa vijisenti.

S. S Bakhressa ana pesa mpaka Forbes inamfahamu lakini huwezi kumsikia akisema hela kiasi hiki ni "vijisenti".

I can't recall even Mengi being this immodest.

Mimi sijawahi kusema nina hela nyingi.

Nilijibu tuhuma kwamba watu wa diaspora tunashindwa kulipa $ 6,000 kufanikisha maziko. Nikasema lumping all diaspora together is not fair, kwani mimi nishachangia mshkaji $2,500 katika matatizo ya kawaida tu yaliyohitaji $10,000 na nikasema pia kwamba safari yangu ya mwisho kuja bongo tiketi na mazagazaga mengine ya zawadi nimetumia in excess of $ 18,000. Sikusema hizo ni vijisenti.

Na hata ningesema, mimi nishakata leseni ya kuwa "court jester" cum "Shakesperean Fool" hapa JF.Kiranga is a singularity, an unorthodox beast, an ungodly behemoth, hajawahi kusema kaelimika wala kujifanya anaweza kufanya kazi ya kuwawakilisha wananchi.

Huwezi kuanza kum compare Kiranga na Chenge, mtu aliyepanda jukwaani kuomba kura za wananchi kwa unyenyekevu wote, halafu anaenda kukufuru hivyo.

Habari kama hii ni mfano mmoja tu wa mtu aliyesoma mpaka kafika Harvard, lakini hajaelimika kuishinda hubris na ego yake.

Na unaweza kukutana na kibabu Lushoto huko kila kinachoongea inafaa kiandikwe chini kama methali. Hajasoma shule lakini kaelimika kutokana na kuwa mwanagenzi wa maisha.
 


Kusema vile ni kukosa elimu maadili au busara?

Kuna uhusiano gani hapo?

Wewe unavyojitapa kufanya shopping ya $ 18000 ktk ulimwengu ambao kuna waneba box wenzio hawana hata uwezo wa kujigharamia nauli kurudi kwao si dharau/ kebehi au ubinafsi?

Chenge alisema kila mtu ana viwango vyake hata Mimi kuna hela naiona ndogo na nyingine naona nyingi hivyo kusema 1bn ni vijisenti katika bahari ya wenye 1000bn its just a comparison!!

Dharau si kipimo cha kumtambua msomi sababu hata wazungu walotuletea usomi wanadharau ngozi nyeusi.....

Think big kiranga!!
 

Kusema vile ni kukosa elimu, maadili na busara.

Mimi sikujitapa, nimesema ukweli wa kitu ambacho nimekifanya ili ku clear the record baada ya sisi watu wa ughaibuni kuambiwa kwamba tumeshindwa kulipa $6,000. Nikaonyesha kwamba anga zangu hiyo ni hela ya kulipwa na watu wawili tu.

Halafu unapoendelea kuni lambast kwa kutumia $18,000 zangu mwenyewe, ambazo sijamuibia mlipa kodi wa Tanzania, ambazo nishakwambia huwezi kunilinganisha mimi na Chenge kwa kuwa mimi na Chenge hatuwezi kuwekewa standard moja ( mimi si msomi, Chenge ni Harvard alumni, mimi.sijaomba kutumikia watu, Chenge ni mbunge na.mqenyekiti wa kamati ua maadili ya CCM at the time.etc)

It seems like this.point was lost on you.

Chenge anapoongea publicly hana uhuru wa kusema kila mtu ana viwango vyake, anatakiwa kuwa very thoughtful about the feelings of his constituents, mimi sina constituents kwenye public space. Kusema kwamba Chenge anaweza kusema kila mtu ana standards zake ni kutoelewa role ya Chenge kama a public servant.

Kusema wazungu ndio wametuletea usomi ni kudhihirisha ujinga wako.

Dharau, hususan kwa a public servant, is a form of intellectual insecurity and ignominy.

I don't only think big, I think beyond the 11nth spatial Kaluza-Klein string theory manifold.

Big is not even the word.
 

Wewe acha ubishi chenge kusema vijisenti kunaondoa vipi usomi wake? Hii kauli imekuvunjia heshima...

Ninakiri na nitakiri bila woga wala aibu elimu niliyosoma walileta wazungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…