Tukiacha mambo ya kuajiri, tuje katika maisha mengine kabisa
Rayvanny enzi anaitwa Raymond unajua alikaa WCB kwa muda gani mpaka anatambulishwa rasmi kama member? Zuchu je?! Unajua alikaa WCB kwa muda gani mpk anakuja tambulishwa rasmi kama member official? Achana na hao
Tuje kwa MBOSSO unajua alisugua benchi kwa muda gani? Mbosso tena alikua WCB wenzake wanaenda show wao wapo tu hata sh 100 ya maji hana, alikua WCB lakini msoto aliokua anaupitia sio wa kawaida na sio kwamba huyo DIAMOND au kina tale walikua hawamuoni, walikua wanamuona daily. Kwanini sasa walikua hawamsaidii kum sign aanze pata pesa zake kupitia muziki wake/kipaji chake?!
Kwani Mbosso/Zuchu, Raymond na wengine wameanza kuonyesha vipaji baada ya kutambulishwa jamvini? Walikua na vipaji vyao tangu hukoo kabla hata ya lebo WCB haijulikani.
Unaweza nisaidia niambia kwanini walikua wanasita kuingiza wasanii wapya kwenye lebo mpaka wajiridhishe nae? Unazijua sheria na taratbu za mpaka kukubaliwa kuwa member wa WCB?? Kama ni msoto basi waulize wasanii wa WCB nini maana ya msoto watakueleza maana yake..
Huo ni mfano HAI ambao ni rahisi sana kueleweka, iko hivi mkuu mtu hawezi kukukabidhi ofisi yake usimamie kama hata huwezi simamia na tatua matatizo madogo madogo tu ambayo unakutana nayo ukiwa katika biashara yake.
Mtu unamkabidhi pikipiki/gari imsaidie katika kufatilia biashara zako, ila chombo cha usafiri anachokitumia yeye kwa zaidi ya asilimia 81 kinapata hitilafu "harekebishi" ana paki hapo, anakwambia kitu flani kimeharibika. Maana yake anataka mimi ndio nitengeneze.
Mtu unamuacha ofisini unasafiri, huku nyuma wanakuja TRA/TFDA wanakuta kasoro ofisini badala a solve tatizo halafu boss akirudi amueleze A B C D, yeye anaacha OFISI inapigwa kufuli wakati alikua ana uwezo wakuchukua hata 50,000 akawapa wale raia wakasepa boss akirudi unamuelezea ilikua hv hv hv, ila anakubali ofisi ifungwe halafu anarudi kulala nyumbani kwasababu anajua boss haupo na ofisi imefungwa.
Mkuu hamna mwajiri yuko tayari ajiri au muachia mwajiriwa ofisi aisimamie kama huyo muajiriwa hajielewi, kujielewa si tu katika utendaji kazi bora, ila kuna mambo mengi sana yanayoweza kukuonyesha huyu mtu anajielewa.
Mwajiri bora si yule anaetoa mshahara mkubwa, ingekua hivyo basi wahindi wasingekua wanalalamikiwa kila siku kuna vitu extra ambavyo mwajiri anataka avione kwa mwajiriwa wake lakini waajiriwa wengi wame-focus kwenye mishahara, ukitaka mfanyakazi afanye kazi sanaaa, atumie akili yake 99% kazini mlipe mshahara mkubwa jambo ambalo si sawa mfanyakazi anaekuwa bora kwasababu ya mshahara anaopokea huyo si mfanyakazi.
Biashara zina ups n down, vipi siku kampuni ikifilisiwa kabisa boss ukashindwa lipa hata wafanyakazi mishahara unafkiri kuna mfanyakazi ataebaki na wewe hapo? Mimi kuna wakati nachelewesha mishahara makusudi kabisa, sio kwamba nakuwa sina hela ya kulipa raia ila nachelewesha makusudi nione hali zao wangapi watamudu.
Kwahiyo mkuu hamna mwajiri anapenda kutesa wafanyakazi wake, HAKUNA ila kuna vitu waajiri wenye future wanatamani kupata wafanyakazi CREAM, unajua kuna wafanyakazi halafu kuna ile CREAM ya wafanyakazi ambao mpaka unampata mfanyakazi cream unaweza kaa kwenye biashara katika miaka mi 5 ukampata m 1.
Kuna vitu vingi mkuu ila mimi nataka tu ufahamu hamna boss anapenda tesa wafanyakazi wake labda huyo boss awe na mapepo tu.