Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 1,914
- 6,033
Paul Pogba ni mmoja ya wachezaji waliotarajiwa makubwa wakati akiwa anakua. Alitajwa kuwa na kipaji kikubwa na uwezo mkubwa wa kucheza kama kiungo.
Akatoka Man Utd baada ya kukosa nafasi akaenda zake Juventus na kukiwasha. Baada ya misimu kadhaa akarudi zake Man Utd kwa usajili wa rekodi ya dunia.
Baada ya misimu sita Pogba akarudi zake Juve huku akiwatuhumu Man Utd kwa kutomthamini.
Lakini tangu ameenda Juve kwa mara ya pili ni kama majeraha yamemuandama na amecheza mechi chache sana.
Pogba sasa ana miaka 30, haimbwi tena, Juve wanafikiria kuvunja mkataba naye, yaani mambo hovyo kabisa. Kuna kipindi alihusishwa na tuhuma za uchawi lakini skendo ikapotea.
Ni wapi alipokosea Pogba? Mchezaji ambaye alitabiriwa makubwa ikiwemo kuchukua ballon d’or
Akatoka Man Utd baada ya kukosa nafasi akaenda zake Juventus na kukiwasha. Baada ya misimu kadhaa akarudi zake Man Utd kwa usajili wa rekodi ya dunia.
Baada ya misimu sita Pogba akarudi zake Juve huku akiwatuhumu Man Utd kwa kutomthamini.
Lakini tangu ameenda Juve kwa mara ya pili ni kama majeraha yamemuandama na amecheza mechi chache sana.
Pogba sasa ana miaka 30, haimbwi tena, Juve wanafikiria kuvunja mkataba naye, yaani mambo hovyo kabisa. Kuna kipindi alihusishwa na tuhuma za uchawi lakini skendo ikapotea.
Ni wapi alipokosea Pogba? Mchezaji ambaye alitabiriwa makubwa ikiwemo kuchukua ballon d’or