Nini kifanyike Wizara ya Viwanda na Biashara?

Nini kifanyike Wizara ya Viwanda na Biashara?

TinyMonster

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2009
Posts
242
Reaction score
154
Ni wizara muhimu sana katika nchi kama ingekuwa ni timu ya mpira tungesema ndio namba 6, maana ukivuruga viwanda na biashara wizara nyingine na taasisi za serikali haziwezi kujiendesha kutokana na ukweli kwamba makusanyo ya kodi yakikwama kutokana na biashara kutokuwa nzuri uchumi unayumba.

Ni mara ya tatu JPM anabadili waziri, lakini nini hasa ni tatizo? Waziri mpya Bwana Bashungwa ambaye nae ni mwanajamvi mwenzetu hapa JF anatakiwa afahamu na kubadili kitu gani?
 
Anatumia ID gani au wewe ndio bashungwa mwenyewe?
 
Ni kwa nini asingekuja yeye mwenyewe na ID yake,ili tunapojadili tuende sambamba na kumuuliza maswali juu ya mtazamo na maono yake yeye?
 
Ni kwa nini asingekuja yeye mwenyewe na ID yake,ili tunapojadili tuende sambamba na kumuuliza maswali juu ya mtazamo na maono yake yeye?
Unamjua Dr Mary Mwanjelwa, Professor Anna Tibaijuka
Hao Ni Members Humu Kuna Siku Walisign In
Hiyo Siku Thread Zao Ndani Ya Saa Moja
Page Ikafika 50
 
Unamjua Dr Mary Mwanjelwa, Professor Anna Tibaijuka
Hao Ni Members Humu Kuna Siku Walisign In
Hiyo Siku Thread Zao Ndani Ya Saa Moja
Page Ikafika 50
Walikuwa wanachangia lakini?au walifungua na kusepa?
 
Unamjua Dr Mary Mwanjelwa, Professor Anna Tibaijuka
Hao Ni Members Humu Kuna Siku Walisign In
Hiyo Siku Thread Zao Ndani Ya Saa Moja
Page Ikafika 50
Page 50 ndani ya lisaa!? nenda MMU au kuleeeee uone ndani ya lisaa wanajaza page ngapi.
 
Mimi sijaelewa mtazamo wa mkuu kwenye wizara hii kwa saabu kamtumbua waziri na kumpandisha mtendaji wake kampeleka TRA, bado nna kizunguzung hapa
 
Ni kwa nini asingekuja yeye mwenyewe na ID yake,ili tunapojadili tuende sambamba na kumuuliza maswali juu ya mtazamo na maono yake yeye?

Hayupo active kivile ila ni Mwana JF toka enzi hizo hajawa mbunge
 
- asome kwa makini 'duties and responsibilities'
- asiwe mwoga kumwambia ukweli JPM, akijifanya mramba miguu kama kabudi itakula kwake
- asiwe na majibu mepesi na ya mzaha kwenye mambo muhimu, maswala ya kuita cherehani kiwanda na kuwataka wakulima wale korosho zao ajiepushe nayo
- ajaribu ku 'acknowledge' matatizo yaliyopo ambayo yamesababishwa na sera mbovu za serikali
- ashirikiane na mawaziri wenzake kupunguza ukiritimba na usumbufu wanaoupata wanaofungua biashara mpya
- kwakua amekua waziri asituone sisi wengine 'mbuzi tu'
- pale wizarani atakutana na 'vibabu' vyenye akili za kijamaa na kikoloni awenavyo makini, yeye ni kijana akawe mbunifu na mwenye kuweza kuhamasisha na kuwapa motisha watumishi walio chini ya wizara yake
- atembelee taasisi zilizo chini ya wizara yake mara kwa mara

NB. Hapo viwanda na biashara mawaziri wanakuja wanapita lakini naibu waziri eng. Stella yupo ni mzoefu, atakupa mawili matatu msikilize.
 
Waziri ndiye kiongozi mkuu wa wizara. Hivyo basi kwa kuwa inafahamika kuwa mazingira ya biashara siyo magumu mageuzi yanahitajika.

Ni waziri anayepaswa kutuongoza kufanya mapitio ya mifumo yetu na taratibu za kufanya biashara na uwekezaji wa viwanda.

Inahitaji mtu mwenye maono na guts za kufanya marekebisho. Vinginevyo akifanya Business As Usual zile kero zilizotajwa juzi zitamtafuna siku moja.
 
Back
Top Bottom