Nini iwe ajenda ya wapinzani 2010 - 2015

KAMARADE

Member
Nov 18, 2009
63
3
Wakati tunaelekea katika uchaguzi dalili zinaonyesha kuwa kama vyama vya upinzani havijawa makini na kuweza kuja na ajenda ambayo itawawezesha kuaminiana na pia kujenga imani kwa wapiga kura basi kuna hatari ya upinzani hasa kwa upande wa Tanzania bara kuwa extinct.

Vyama vya upinzani na haswa CHADEMA vilikuwa na kila dalili ya kuweza kupata viti vingi vya ubunge na udiwani zaidi ya miaka ya nyuma hadi miezi ya hivi karibuni ambapo hali inaonyesha kuwa imegeuka kabisa.

Yapo mengi yametokea lakini iongoni mwa makubwa ni lile la ubabe wa CHADEMA kumzima mwanasiasa machahcri na mwenye mvuto kuliko wote nchini Zitto Kabwe kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama chake na pia kuishiwa nguvu kwa hoja ya UFISADI ambayo mwishowe ilikuja kutekwa na kundi la wajanja wa CCM.

Mimi binafsi nawajua wapiga kura wengi tu wakiwemo vijana mbalimbali ambao sio tu walikuwa wameshaamua kupeleka nguvu zao vyuma ya vyama vya upinzani na haswa CHADEMA lakini pia walikuwa tayari wako katika mikakati ya kusimama katika uchaguzi kupitia vyama hivyo. Wengi wao walikuwa ni wasomi na wenye muamko wa hali ya juu. Hivi sasa wengi wao ama wameamua kuachana na siasa ama kujiunga na CCM.

Hali ni mbaya kiasi ya kwamba yawezekana kabisa bunge lijalo likawa na wabunge kichache zaidi kutoka upinzani. Kitakachookoa ni wabunge wa CUF tu kutoka Zanzibar ambao wao wanafaidika na siasa za historia na mgawanyiko wa kijamii bila ya kujali utendaji wa wanaochagua.

Swali linakuja, NINI KIFANYIKE KUOKOA DEMOKRASI YETU AMBAYO BADO IPO KATIKA NGAZI ZA KUTAMBAA LAKINI INA UMUHIMU MKUBWA KWA UJENZI WA TAIFA LETU?

Kwa maoni yangu ni kuwa;

1. Suala la kuungana vyama vya upinzani sio suala la kupenda bali ni suala la kufa na kupona.

2. Vyama vya upinzani vinapaswa kuja na ajenda ambayo inatofautiana na ya kila siku ya kuleta maendeleo. Mfano ni ajenda ya kufanya mabadiliko ya kimfumo yatakayohusisha watanzania wote yatakayoishia katika kupata katiba mpya ambayo ndio itatumika katika uchaguzi ujao ambao unaweza kufanyika katika kipindi cha miaka miwili - mitatu - minne. Kwa hali ilivyo katika vyama vya upinzani ni vigumu kwa watanzania kuamini kuwa wanaweza kufanya vizuri katika ajenda ya MAENDELEO tofauti na ifanyavyo CCM.

3. Kusimamisha watu wapya kabisa katika siasa za urais lakini wana heshima isiyotia shaka miongoni mwa watanzania ambao wataaminika kupewa jukumu la kuijenga upya Tanzania na kuondoka madarakani mara baada ya kipindi kimoja tu cha uongozi.

4. Kuunda serikali ya mseto ambayo ajenda yake itakuwa ni kuhakikisha political reform kwa kipindi kichache na hawa watatoka katika vyama vyote wakiwemo wa CCM.

Ni imani yangu kuwa wakichukua baadhi ya haya bila ya kuacha la wao kuungana kuanzia ngazi ya urais hadi udiwani na hata kutumia chama kimoja kusimamisha wagombea urais watakaoaminika na vyama vyao hata kama hawatakuwa miongoni mwa wanachama wao, basi sio tu wanaweza kuokoa siasa za demokrasia ya vyama vingi lakini hata kujenga upinzani madhubuti wenye kuonge na kusikika.

Kama hawatafanya hivyo, basi tujiandae kuzika upinzani na kuacha njia ya MAFISADI kushika hatamu hapo mwaka 2015 kama ambavyo wanavyojipanga sasa.

Na wengine tuzikumbuke kadi zetu za TANU

Nakaribisha mjadala
 
Kamarade,

Ili Maoni haya uliyoyaita "maoni yangu", ambayo ni uthibitisho kuwa hayakufanyiwa utafiti, nadhani ushauri wako ungelikuwa na nguvu na uzito mkubwa kama ungeliungana na uthibitisho wa takwimu.

Kwa mkono wako umethibitisha pia kuwa "mimi binafsi ninawajua wapiga kura wengi", uwingi ni relative. Hujatuambia wapiga kura hao ni wa chama gani, age group gani, eneo gani. Takwimu za namna hii ndio ingelituonyesha usahihi na uimara wa maoni yako ili tushawishike kuyapokea na kuyatekeleza yote au baadhi yake.

Hoja ya Katiba, na ya kuungana kwa vyama, kwa mimi niliyefika Wilaya zote za Tanzania, ninaielewa matatizo yake kwa Watanzania wa kawaida. Mtu ambaye anakimbilia kikombe cha chumvi kuuza haki yake ya kura sidhani kama anaona umuhimu wa "Katiba" katika maisha yake.

Tunahitaji kuwasaidia kwa kutoa elimu, na kwa hali ya sasa ni lazima lugha zetu zishuke kutoa elimu ya uhusiano wa Katiba na maisha yao. Lakini huu si wakati wa kuzungumzia tena mabadiliko ya kawaida, kwa kuwa kama unafahamu mchakato wa kubadilisha Katiba, basi saa hizi ungelitupa ushauri bora zaid kuliko wa Katiba.

Kama kwa bahati mbaya hufahamu, basi ni vema nikakueleza tu kuwa ajenda hiyo kwa sasa haiwezekani, haina tija, na kwa wananchi wengi wakati wa Kampeni ni sawa na kuwaeleza maisha mazuri ya Washingtone, yaani japo kweli marekani ina maisha mazuri, lakini wanachohitaji watanzania wengi ni namna gani watatoka katika hali ya sasa.

Hivyo ajenda yeyote, itakayowapa matumaini ya haraka kutoka hapa walipo itakuwa ndio ajenda zenye tija. Kuhusu vyama kuungana, nadhani niliisha kutoa elimu ya kutosha katika Forum hii sina sababu ya kuirudia. Msimamo wa Chadema ni pale panapokuwa na Chama Makini na serious cha kuungana nacho, basi tutaungana nao.

Lakini tumeisha kujeruhiwa sana, na nadhani sisi tuliojeruhiwa ndio tunaoelewa maana ya kujeruhiwa, kuliko mtu mwingine yeyote anayetazama kutoka nje.Pamoja na hayo tunashukuru sana kwa maoni yako, inatusaidia kuwa focused zaidi.
 
Hapa hoja ya msingi kati ya alizotoa mtoa mada ni suala la kusimamisha wagombea wapya na wanaojua cha kufanya. CUF hapana jipya, NCCR wajipange sana, TLP siwahesabu, CCJ sijui wana lipi. wengine wasindikizaji. Kimebakia CHADEMA. Inabidi waje na WAZO JIPYA, NIA MPYA ili kuhakikisha yale mawazo mbadala waliyosoma bungeni yanaingia katika vitendo. Siri ya haya mambo ni kuwa na kiongozi mwenye sudi. Nasikitika kuwa ccm inatumia mbinu ya vyama vingi kuligawa bunge na wananchi. Tatizo jingine linalofanya upinzani kushindwa kupenya ni siasa hapa nchini kufanywa sehem ya ajira hivyo kuwa ni jambo la kufa na kupona. Mabadiliko ya dhati hapa nchini yataanzia bungeni na wala si kwingine ila ili mabadiliko haya yatokee, safu ya urais kwa upinzani LAZIMA iwe na nguvu ya hoja. Suala la Dr. Slaa kuwania urais au la ni mtihani mwingine. Kwa upande mmoja litachochea kuchaguliwa kwa wingi wabunge toka upinzani lakini kwa upande mwingine mchango wake tunaweza kuukosa. Kwa namna ya tatu inawezekana mawili hapo juu kupatikana - urais na wabunge. Hapa ni suala la kujipanga na kujitoa (mfano wa sadaka) tu. Kila la heri, CHADEMA
 
Nini agenda?
Wapinzani hawana budi kukaa na kubuni mikakati, kwanza wamfahamu adui yao, mbinu na udanganyifu wa kila aina wanaoutumia! Upo ukweli kuwa vyama vya upinzani vimekuwa vikipeleka majeshi yake bila hasa kumfahamu adui yao. Katika karne hii ya Science na Technology kinatakiwa something etraordinary kuwangoa ss em!

Ni chama kilichosheheni mbwa mwitu wajanja na wazoefu wa kuwinda! Kuwakabili unahitaji kuwa mwindaji mjanja pia! Ujue mahali pa kutega, kupiga na uwe mlenga shabaha kweli kweli!
Moja ya mbinu ambayo wapinzani hawana budi kuitumia ni kuwaelimisha watanzania! Wanatakiwa kuwaanika chama tawala! Ubabaishaji, unafiki wa watawala hawa wa kijani na njano! Watanzania wengi hawajui/ hawana idea of what we are capable off kama taifa! Hawajui nini tunapoteza ama kuibiwa chini ya chama hiki cha kijani na njano! Wapinzani hawana budi kuuwasha moto wa uzalendo ndani ya watanzania! Hawana budi kuwakumbusha kuwa sisi ndio waamuzi wa Tanzania ya kesho ya watoto wetu!

Leo hii uzalendo umekufa, watwana na watoto wao ndio wanaojishibisha na kujilimbikizia! Hatuhitaji kuingia barabarani na mapanga na mishale na mikukuki kudai haki zetu. Ila kama mwananchi wa kawaida angetambua nguvu alio nayo ya kura yake na jinsi ilivyo ya muhimu katika kuamua hatima ya maisha yake na ya Taifa hili kwa ujumla, bila shaka asingeipoteza kwa nusu kilo ya chumvi au kipande cha kigodoro! Lakini nani yuko tayari kupiga mbiu hii!! Je wapinzani wako tayari kuipiga mbiu hii? Maneno yana nguvu kuliko bomu la nyukili kinachohitajika kuufunua ukweli huu kwa watanzania!
 
Dr.Slaa,
Mkuu nimekusikia na kweli umewahi kueleza matatizo ya kuunganisha vyama vya Upinzani. Lakini pamoja na matatizo yaliyowahi kutokea nakumbuka mlisema kuungana haiwezekani kwa sababu kila chama kina ITIKADI yake hivyo kuunganisha isingewezekana isipokuwa mshikamano baina ya vyama kama ilivyokuwa baina yenu na CUF.

Nakumbuka pia mlijaribu huo mshikamano hadi kufikia kuandamana pamoja kupinga aidha hukumu ya Zitto bungeni au yalihusiana na Ufisadi, - sikumbuki vizuri. Matatizo yaliyokuja kujitokeza ilioonyesha wazi mshikamano wenu haukuwa Official, vyama hivi havikuwa na muafaka kimaandishi kiasi kwamba kila mmoja wenu alijaribu kuvuta pale inapowezekana kuachiana sehemu ambazo kila chama kilipo kuwa na nguvu zaidi ikageuka na kuwa kila mgombea mwenye nafasi ya ushindi ashukue jimbo..Mfano mkubwa ni mgogoro wa kiti cha Mbeya vijijini..

Mimi kwa ushauri wangu, bado mnahitajiana sana... Hata ukifikiria vipi hili sii swala la mzaha hata kidogo kwani kama alivyosema Kamarade sisi watu wa nje tunaona,tunasikia na kunusa zaidi yenu kwani tupo karibu zaidi na jamii zote. Tunao jamaa ambao wako tayari kujiunga na vita dhidi ya CCM lakini sio ktk halki iliyopo ambapo utengano bado utatumaliza..

Mkuu wangu pamoja na jitihada zako wewe binafsi,Zitto na viongozi wanachama wa Chadema hapa JF kutufahamisha mengi yanayohusiana na chama hiki bado wengi hao hawana IMANI na chama kutokana na aidha viongozi au pengine sii waumini wa mrengo wa KATI.. Tumewaona kina Mwanakijiji, Rev.Kishoka, Nyani Ngabu na wengine wengi wakisema wazi kwamba wao sii wanachama wa chama chochote cha siasa kwa sababu hadi sasa hakijatokea chama chenye dhamira hasa ya kupambana na matatizo ya wananchi..

Hotuba yako leo Bungeni ni mfano mmoja tu wa jinsi gani Upinzani wanaweza kushirikiana kwa pamoja ikiwa wanaweza kufahamu adui yao ana plan kitu gani na jinsi gani ya kurudisha mapigo...Na hakika wale woote wanaosita kujiunga na vyama vya Upinzani wamekupa salute, yet wanashindwa kujiunga na Chadema, CUF na vyama vinginevyo..Sababu kubwa ni kwamba vyama vyote hivi kila kimoja wapo kina mapungufu ya kiutawala ndani ya chama.

Binafsi washikaji wangu wengi sana ni members wa NCCR au CUF kuliko Chadema (kijiwe cha K tea shop - downtown, Honeypot - Sinza, Mzalendo pub, Level 8, Savannah..na sehemu nyingi ambazo nimekuwa nikitembelea woote wanazo sababu za kutojiunga na vyama vinginevyo kutokana na MTU au WATU wanaokiongoza chama hicho..Na sidhani kama naweza kutaja kwa uhakika idadi yao ila naelewa kwa uhakika ni wengi wasomi ambao kwa usomi wao sidhani kama kuna sababu ya kutaja Umri wao..

Katika mtiririko wa mapugufu ya vyama hivi na kwa bahati mbaya mnakuwa nje ya gumzo kama hizi za mjini sii rahisi kwenu kujua mapungufu haya. Waswahili wanasema kila mume ni rijali nyumbani kwake, na hakuna mwanamme anayekubali kuwa yeye ni dhaifu..siri ya Urijali wa mwanamme aujuaye ni mwanamke...Waondio wanajua taste ya mume sii wewe wala mimi.

Kwa hiyo unapoambiwa haya mapungufu hata kama wewe huyaoni. Nakuombeni yafanyieni kazi kwani October haiko mbali na hakika imechukua zaidi ya miaka 20 toka tuwe na demokrasia bado hatujapata chama mbadala. Ushindi wa CCM na hasa JK kwa asilimia 80 (2005) ni aibu kwa demokrasia na hakika sii kwa sababu vyama vyenu haviuziki isipokuwa siasa za Tanzania zimeanza kuwa za nasaba..

Kama zilivyo dini na madhehebu yake. Inapofikia kuwa na dini zaidi ya 30 huwazushia kazi kubwa muumini kuchagua dini ya kweli..na ndio maana imefikia siku hizi watu wanazaliwa waislaam au wakristu na hawataki kusumbua akili zao tena ila kuhangaika na kuweka chakula mezani. Matokeo yake sooote tunafanya haramu na uzito wa mafundisho unapotea..ndivyo inavyotokea ktk kujiunga na vyama vya siasa nchini. Mtu hajui faidi au hasara ya kujiunga CCM,Chadema au CUF zaidi ya kutazama familia yake..

Mkuu tupo ktk njia panda, tunaweza kuanza mwanzo mpya kwa kuungana ili kumwondoa CCM hata kama wapo Mapandikizi... Maadam wanajulikana double agent wanaweza sana kusaliti hata mwajitri wao hasa pale wanapofahamu wameshikwa pabaya...Let them be there wapeni kazi nzito na za hatari zaidi tuwaone kama wataweza. Wakishindwa kwa kuhofia nafasi zao au payroll yao wataingia mitini wenyewe... Time is now mkuu wangu mkipoteza mwaka huu 2010, believe me miaka ijayo vijana hawa ulokuwa nao leo watahamia CCM kwa sababu nao wanajipanga kila mwaka kuhakikisha Ushindi unapatikana by all means necessary!.
 
Kamarade,

Ili Maoni haya uliyoyaita "maoni yangu", ambayo ni uthibitisho kuwa hayakufanyiwa utafiti, nadhani ushauri wako ungelikuwa na nguvu na uzito mkubwa kama ungeliungana na uthibitisho wa takwimu.

Kwa mkono wako umethibitisha pia kuwa "mimi binafsi ninawajua wapiga kura wengi", uwingi ni relative. Hujatuambia wapiga kura hao ni wa chama gani, age group gani, eneo gani. Takwimu za namna hii ndio ingelituonyesha usahihi na uimara wa maoni yako ili tushawishike kuyapokea na kuyatekeleza yote au baadhi yake.

Hoja ya Katiba, na ya kuungana kwa vyama, kwa mimi niliyefika Wilaya zote za Tanzania, ninaielewa matatizo yake kwa Watanzania wa kawaida. Mtu ambaye anakimbilia kikombe cha chumvi kuuza haki yake ya kura sidhani kama anaona umuhimu wa "Katiba" katika maisha yake.

Tunahitaji kuwasaidia kwa kutoa elimu, na kwa hali ya sasa ni lazima lugha zetu zishuke kutoa elimu ya uhusiano wa Katiba na maisha yao. Lakini huu si wakati wa kuzungumzia tena mabadiliko ya kawaida, kwa kuwa kama unafahamu mchakato wa kubadilisha Katiba, basi saa hizi ungelitupa ushauri bora zaid kuliko wa Katiba.

Kama kwa bahati mbaya hufahamu, basi ni vema nikakueleza tu kuwa ajenda hiyo kwa sasa haiwezekani, haina tija, na kwa wananchi wengi wakati wa Kampeni ni sawa na kuwaeleza maisha mazuri ya Washingtone, yaani japo kweli marekani ina maisha mazuri, lakini wanachohitaji watanzania wengi ni namna gani watatoka katika hali ya sasa.

Hivyo ajenda yeyote, itakayowapa matumaini ya haraka kutoka hapa walipo itakuwa ndio ajenda zenye tija. Kuhusu vyama kuungana, nadhani niliisha kutoa elimu ya kutosha katika Forum hii sina sababu ya kuirudia. Msimamo wa Chadema ni pale panapokuwa na Chama Makini na serious cha kuungana nacho, basi tutaungana nao.

Lakini tumeisha kujeruhiwa sana, na nadhani sisi tuliojeruhiwa ndio tunaoelewa maana ya kujeruhiwa, kuliko mtu mwingine yeyote anayetazama kutoka nje.Pamoja na hayo tunashukuru sana kwa maoni yako, inatusaidia kuwa focused zaidi.

Du...kazi ipo. Tunapambana na uhodhi wa CCM katika nyanja zote za utawala kumbe kuna wengine wameshahodhi ajenda za "Upinzani/mabadiliko". Kwa heshima na taadhima Dr Slaa nadhani kuna umuhimu ukachukua muda kureflect mtazamo wako kuhusu masuala haya kama unashawishiwa na maslahi/manufaa ya taifa letu ama umeegemea zaidi katika matamanio binafsi na maumivu unayokumbana nayo katika harakati za kuchochea mabadiliko nchini mwetu.


omarilyas
 
Dr. Slaa,

With all due respect, I have to be honest and frank to you that I do not think Opposition at the current state has any idea or effective plans to run the country efficiently or plan for the future thoroughly.

I have read your speeches and your comments here at JF and even though they may sound impressive and it is easy for one to fall in love with you, however when it comes to implementation, and follow through of what you articulate, either you are a lone ranger in the field or you are being blindsided by the reality of what you claim to be first hand on the ground.

It has beena common thing for majority of your peers even here at JF to claim that we the Rev, kishoka and others who are critical are not on the ground to see the realities. well just like Mwewe above the skies, we can see the ground at a wider scope than the chicken who sees the next grasshoper or leaves to the limited horizon, not knowing that further ahead there is trouble waiting.

The opposition needs to be open minded and think outside the box and start incorporatng free ideas being catapulted on its way if it wants to be effective.

One person has quoted your statement stating that your preference si to be opposition, then if that is true, you will always put yourself at disadvantage of taking charge to lead Tanzania and demonstrate to watanzania that you can walk the talk.

As per Kamarade inquiry, you trully need to value his input regardless of what we know about your strategies collectivelly with CUF or CHADEMA by itself or as Dr. Slaa himself. It will be very naive and a tragic mistake if you will dismiss his ideas as unresearched and unscientific as you have used the temr while responding to an issue I raised before.

I have a simple task that I will ask for it to be your focus for the next 5 years. Focus on taking control of TAMISEMI at any cost. You will have upper hand of monitoring voter's registration, first hand knowledge of managing local government budgets andprojects and most of all inject accountability frol streets, wards, kata, tarafa all the way to wilaya and Mikoa where you can track and enforce not only accountability but efficiency and follow up ot track daily progress of Manendeleo ya wananchi actively and you will definately have an upper hand and say on many things and not a sole Mbunge who is a single vote on the district level!

Common opposition wake up and smell the coffee!
 
Wakuu,

Naoma mniwie radhi kwa kuchepuka kwa muda mrefu bila ya kuendele na mjadala huu niouanzisha hapa mwanzoni. Naendelea kupitia mjadala wa kuhusu CHADEMA ambao Mwanakijiji ameuanzisha katia thread mbili tofouti ili niunganishe na mjadala huu na kujibu maswali na kujaribu kuchanganua mikanganyo kadhaa inayojitokeza. Hata hivyo hadi sasa naelekea kukubaliana na msimamo wa mwanakijiji ambao ingawa unaweza kuonyesha kukinza maslahi ya CHADEMA kwa muda huu wa uchaguzi lakini bado wana nafasi ya kuweza kurekebisha mambo na kufaidika zaidi na mahitaji ya nyakati hizi.
 
Back
Top Bottom