Nini hasa siri ya kuachwa kwa ole medeye.?

Nini hasa siri ya kuachwa kwa ole medeye.?

Mimi ni Mmasai lakini huyu bwana Medeye ni miongoni mwa watu ambao aina ya Siasa zake mimi zinaniboa sana!

Kabla ya huyu Mwehu kuwa Mbunge na hatimae Waziri,,Arusha hatukuwahi kuwa na Siasa za Kikabila.
Mfano; Tangia nchi yetu ipate uhuru mbunge wa Arusha kutoka kabila la Wenyeji(Mmasai) ni mmoja tu nae aliitwa Ole Saibulu!Lakini kwa miaka mingine yote Wabunge walikua ni makabila tofauti.

Baada ya Ole Saibulu tulimpata mbunge alieitwa,,Mbagga(Mpare Ccm) na baadae akafuatiwa na Kinana(Msomali Ccm),,akaja Makongoro Nyerere(Mzanaki Nccr),,akafuatiwa na Felex Mrema(Mchagga Ccm) na sasa Godbless Lema (Chadema)

Miaka yote wakati wote niliowataja wakiwa wabunge,hatukuwahi kushuudia Siasa za Ukabila isipokuwa wakati ule tu Marehemu Ole Saibulu alipojaribu kufanya siasa za ukabila akaondolewa na Mwl Nyerere wakati huo akiwa Rais na mwenyekiti wa Ccm!

Kinachosikitisha ni kwamba Wachagga wanapokua viongozi kwa kupitia Ccm,,sio kosa ila wakiwa Viongozi kupitia Chadema ndipo inapokua Nongwa!

Hata sasa Meya(Wa kichina) kupitia Ccm Gaudens Limo ni mchagga lakini Ole Medeye haoni hilo isipokuwa anamuona tu Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema kuwa ndie mchagga!

Kwa ujumla nimefarijika sana kutokana na mh Kikwete kumuacha ktk baraza la mawaziri bwana Olemedeye. Hongera sana Kikwete pamoja na wapenda Usawa wote!
 
Kuna watu wamemlaumu na
kumbeza Rais katika uteuzi wake
wa Baraza la mawaziri.
Wakuu, baraza la mawaziri ni hitaji
la kikatiba. Wawe mizigo au
wasiwe mizigo lakini sio utashi wa
Rais. Ni ngumu sana kufanya kazi
bila kuwa na mawaziri. Kwaiyo kwa
kukidhi hitaji la katiba ambalo Rais
hana option anajaza cabinet
miongoni mwa wale
tuliomchagulia. Sasa wengine
tulimpeleka Ole Sendeka, wengine
Lusinde, Wengine tulimpeleka Maji
Marefu, wengine tulimchagua Idd
Zungu, sasa rais anachagua humo
humo,
Na uteuzi wa Baraza la mawaziri
pamoja na factors zingine
hupaswa kuwa la Kitaifa. Kwaiyo
uiano wa mawaziri kimikoa
wanayotoka ni muhimu sana.
Otherwise utajikuta huna cabinet
ya kitaifa. Kaondoka Nchimbi wa
Ruvuma kaingia Jenista wa
Ruvuma. Amefariki Mzee wetu
Mgimwa wa Iringa amekuja
Mgimwa mwingine wa Iringa. Yule
mkabila wa Ngorongoro katoka
amekuja Tetele sijui Telele nae ni
wa jamii ya wafugaji. Rais hachagui
hovyo jamani...Na ninaamini ni
moja kati ya kazi ngumu sana rais
aliyonayo kupanga safu ya
Mawaziri. Kwa kuzingatia uwiano
huo kawapata hao. Otherwise kwa
dodoma Nkamia angeachwa
angeteuliwa Lusinde na kadhalika
na kadhalika. Mnyonge
mnyongeni....

kama hivyo ndivyo.,nani amemreplace Kagasheki kutoka kagera? Nani mbadala wa matayo david kutoka upareni?
 
Una hoja ila ni nyepesi. nasema hivi kwa sababu katika uteuzi tukiangalia atokako mtu basi itabidi tuangalie pia kabila lake,dini hata rangi pia twaweza kufikia huko. Waziri haendi kufanya kazi kwa ukanda wake tu bali kwa taifa zima. Hivyo cha kuangalia ni uwezo na uadilifu. Na kama J.K ametumia kigezo hicho cha atokako mtubasi atakuwa kakosea na kupotoka pakubwa.

Uzoefu lakini wa huko nyuma unaonyesha baadhi ya watu walishika nyadhfa wakapendelea kwao tu n hilo liko wazi! Hivi unafikiri miundombinu hafifu mikoa ya Lindi na Mtwara au kule Kigoma, Rukwa ni bahati mbaya? Ni upendeleo ambao kwa nyakati fulani ulikuwepo na wote tunakumbuka. Hivyo bila kujali dini, ila balance kama ambayo hufanyika inasaidia kidogo! Nami kwa hili nimpongeze mh. Rais na wasaidiz/washauri wake kulijua hili.
 
Heard of clip....na yule wa mifugo ambaye haonekani jimboni...bad timing to OM....
 
Huyu ndio chimbuko la migogoro mingi Wizara ya ardhi
 
Katajwa kwenye kasheshe ya wakulima na wafugaji kule Kiteto. Kuliletwa hapa JF hata clip ya mikutano aliyoandaa na kuhudhuria na wafugaji kabla ya kutoke mauaji kule. Inaelekea alijisahau akadhani ni waziri wa wafugaji wa kabila lake
 
Mulugo alijiamini sana, nini kimemtoa?
 
kwasababu ya kumuunga mkono lowasa lakini haijalishi manake lowasa atagombea urais 2015 kwa ticket ya chadema
 
badala ya kuuliza kwanini ameachwa , hebu jiulize kwanini aliteuliwa ?
aliteuli kwasababu ukurugenzi wake wa director of administration wizara ya ardhi uliasisiwa na sponsor mkuu alipokuwa wizara ya ardhi kama wizara kama sikosei
 
Sidhani kama alikuwa au alishawahi kuwa "a minister material" zaidi ya kujua kucheza karata zake kwa wakati muafaka. Nasema hivyo maana naamini ni product ya Lowasa 100% na mwanafunzi mzuri wa Lowasamania. Ukifuatia jinsi anavyojua kujipenyeza (lobbying) basi ni haki yake kudondoka once a master is destroyed. Haya ya ukabila yamerahisisha safari yake ya kuondoka katika baraza la mawaziri bali the real issue ni ile connection yake na EL na jinsi alivyoingia kwenye cabinet kwa mgongo wa huyu bwana bila ya kuwa na uwezo kiutendaji. EL angekuwapo au kama bado angekuwa strong, I bet Medeye angekuwa kwenye cabinet panga pangua. He is smart but hopeless. Hana uwezo kiutendaji bali mzuri wa kuzunguka wenziwe na kuonekana mtendaji until you come to know him properly. Uliza watu waliofanya naye kazi hasa maboss wake kam Ole Kambaine na Col. Nalingingwa! If they have anything good to say about him then is about his ability to assassinate your character to facilitate his way up, full stop!

Kwa wanaomjua huyu Mh. watakubaliana na mimi kuwa is a master of lobbying, he is a prolific and full time lobbyist. Katika maisha yake yote, mpaka anapata uwaziri, ni watu wengi tu wamekuwa victims wa tabia yake hiyo. Alifikiri na bado anafikiri EL anauwezo wa kumkingia kifua kama ilivyotokea katika miaka ya huko nyuma kwa kutumia migongo ya wakubwa wengine, maana EL wamejuana hivi karibuni tu. Waliofanya naye kazi watakwambia jinsi alivyowatumia wakubwa wake kusariti wengine ili aonekane anafaa kwao na kisha kuwasariti hao wakubwa wake walioingia mkenge na kuwaacha wakisaga meno huku jamaa akisonga mbele kwa spidi ya ajabu. Haya ni malipo ya tabia yake mbaya maana you can cheat some people for some time but you can not cheat all people all the time.


Mabadiliko ya baraza la mawaziri yameleta sura mpya lakini pia yamewaondoa baadhi ya waliokuwepo. Mmoja kati ya walioondolewa bila kutarajiwa ni mh.ole medeye aliyekuwa naibu waziri wa wizara ya ardhi ,nyumba na maendeleo ya makazi. Je ni nini kilichomfanya naibu waziri huyu kuachwa. Je ni zile tuhuma kuwa anafanya siasa za ukabila arusha? Au ni 'kuonekana ikiwa bega kwa bega' na 'kujionyesha waziwazi' akimuunga mkono mh.lowasa?...lakini pia pengine ni 'kuperfom' chini ya kiwango?..(ingawa mimi binafsi siamini kama hiyo inaweza kuwa ni sababu,kwani kuna wale 'mizigo' wamepeta)...ni nini siri hasa ndugu zangu?
 
Back
Top Bottom