Nini hasa maana ya katiba ya wananchi (ikawa)

Mkandara

JF-Expert Member
Mar 3, 2006
15,772
8,958
Tumekuwa tukisoma na kusikia vyombo vya habari, vyama vya siasa na taasisi za kijamii wakitumia hili neno KATIBA YA WANANCHI hadi kufikia kundi moja la wajumbe wa bunge maalum la katiba kuunga Umoja wao na kujiita UKAWA. Tatizo la neno hili lipo ktk matumizi yake, na weredi umetofautiana sana baina ya Wananchi wenyewe, wanazuoni na wanasiasa na kwa sababu tofauti. Aidha maana hizi zimetumika kwa kuzingatia umuhimu wa katiba yenyewe na utunzi wake ama kutokana na tofauti za wananchi wenyewe ktk ufuasi wa vyama vyao vya kisiasa na upinzani wa kiutawala.

1. Wapo wanaoita mchakato wa katiba hii unalazimika kufuata rasimu yenye Maoni ya wananchi kuwa hii ndio maana halisi ya neno hili na imeungwa mkono kwa idadi kubwa ya wasomi na wanasiasa ambao wameunda umoja huo wa UKAWA kushinikiza rasimu ya Warioba iwe ndio framework ya uandishi wa katiba Mpya. Haya ndio matakwa ya wananchi na lazima yafuatwe..Na sababu kubwa ya kukubaliwa kwake ni kutokana na ukusanyaji wa mawazo ya wananchi wa bara na visiwani ambao walipendekeza mabadiliko makubwa ktk muundo wa serikali, mfumo wa Utawala, Utaifa na mengineyo mengi ambayo wananchi wenyewe walipendekeza kuwa ndiyo yawe mwongozo wa nchi yao.

2. Na wapo wanazuoni ambao wanaamini maana halisi ya Katiba ya Wananchi ni Katiba itokaynayo na wananchi wenyewe, katiba ambayo inayowagusa, inawahusu raia wote pasipo kujali tofauti zao za kijamii kwa kuzingatia matabaka waliyomo ili kuimarisha umoja na Utaifa wao. Katiba ya wananchi ni mwongozo unao wahakikishia wananchi kuwa UHURU na HAKI zao zinalindwa. Katiba ndio sheria mama ya Taifa (Fundamental law), yanye mamlaka ya juu kisheria (supreme legal Authority) hivyo raia wote ktk makabila na matabaka yao, vyombo vya serikali, majeshi, vyama vya siasa, vyombo na taasisi za Umma na mashirika yote binafsi na ya serikali wote kwa ujumla wao wanalazimika KUTII katiba hiyo kama mwongozo wao (a basic norm of conduct) na wote wanawajibika ktk kuheshimu na kuhakikisha katiba hiyo inatekelezeka. Katiba hii haitungwi kwa Mawazo ya wananchi wote ama walio wengi bali ni katiba unayogusa hisia na kuwalinda wananchi wote na Uhuru wa nchi yao..

Imenilazimu kuandika mada hii ili kupanua fikra zetu ktk weredi wa neno hili na matumizi yake hasa baada ya kuwasoma baadhi ya Wanasiasa na Wasomi tena wengine wanasheria wakisema hakuna haja wala haraka ya kuipata katiba Mpya isipokuwa kinachotakiwa zirekebishwe baadhi ya Ibara za kisiasa ktk katiba wanayodai imepitwa na wakati ili kuwezesha uchaguzi ujao uwe wa wazi, haki na usawa kwao wao. Tena inaonyesha wako karibu kufikia muafaka wa kuahirisha katiba ya wananchi ili kulinda maslahi ya wanasiasa wa pande zote mbili ambao hawawajibiki kwa wananchi isipokuwa kwa vyama vyao vya siasa.

Sasa leo hii hiyo KATIBA YA WANANCHI ilosiwamiwa kwa nguvu zote inaonekana kutupwa pembeni na maswala ya muafaka wa kisiasa kuchukua nafasi kusema kweli imesikitisha sana, yaani madai yote ya wananchi iwe kwa mtazamo wa kwanza ama wa pili unawekwa pembeni kupisha uwekekano wa uchaguzi ujao pasipo kupata ridhaa ya wananchi wenyewe ambao pengine (who knows) wapo radhi kwao uchaguzi ujuao uahirishwe hadi hapo katiba yao itakapo patikana kwanza.

Maoni yenu wana Jamii..
 
UKAWA NDIO HABARI YA MUJINI....hamtaki mezeni wembe au mwagianeni tindikali


UKAWA ndio dawa ya MAGAMBA!
 
Laiti Kma CCM Wakikbali Kuwa Maoni Yenye Serikali 3,2,1 Yote Ni Ya Wananchi Wakafanya MARIDHIANO Katiba Mpya Inawezekana
 
Tumekuwa tukisoma na kusikia vyombo vya habari, vyama vya siasa na taasisi za kijamii wakitumia hili neno KATIBA YA WANANCHI hadi kufikia kundi moja la wajumbe wa bunge maalum la katiba kuunga Umoja wao na kujiita UKAWA. Tatizo la neno hili lipo ktk matumizi yake, na weredi umetofautiana sana baina ya Wananchi wenyewe, wanazuoni na wanasiasa na kwa sababu tofauti. Aidha maana hizi zimetumika kwa kuzingatia umuhimu wa katiba yenyewe na utunzi wake ama kutokana na tofauti za wananchi wenyewe ktk ufuasi wa vyama vyao vya kisiasa na upinzani wa kiutawala.

1. Wapo wanaoita mchakato wa katiba hii unalazimika kufuata rasimu yenye Maoni ya wananchi kuwa hii ndio maana halisi ya neno hili na imeungwa mkono kwa idadi kubwa ya wasomi na wanasiasa ambao wameunda umoja huo wa UKAWA kushinikiza rasimu ya Warioba iwe ndio framework ya uandishi wa katiba Mpya. Haya ndio matakwa ya wananchi na lazima yafuatwe..Na sababu kubwa ya kukubaliwa kwake ni kutokana na ukusanyaji wa mawazo ya wananchi wa bara na visiwani ambao walipendekeza mabadiliko makubwa ktk muundo wa serikali, mfumo wa Utawala, Utaifa na mengineyo mengi ambayo wananchi wenyewe walipendekeza kuwa ndiyo yawe mwongozo wa nchi yao.

2. Na wapo wanazuoni ambao wanaamini maana halisi ya Katiba ya Wananchi ni Katiba itokaynayo na wananchi wenyewe, katiba ambayo inayowagusa, inawahusu raia wote pasipo kujali tofauti zao za kijamii kwa kuzingatia matabaka waliyomo ili kuimarisha umoja na Utaifa wao. Katiba ya wananchi ni mwongozo unao wahakikishia wananchi kuwa UHURU na HAKI zao zinalindwa. Katiba ndio sheria mama ya Taifa (Fundamental law), yanye mamlaka ya juu kisheria (supreme legal Authority) hivyo raia wote ktk makabila na matabaka yao, vyombo vya serikali, majeshi, vyama vya siasa, vyombo na taasisi za Umma na mashirika yote binafsi na ya serikali wote kwa ujumla wao wanalazimika KUTII katiba hiyo kama mwongozo wao (a basic norm of conduct) na wote wanawajibika ktk kuheshimu na kuhakikisha katiba hiyo inatekelezeka. Katiba hii haitungwi kwa Mawazo ya wananchi wote ama walio wengi bali ni katiba unayogusa hisia na kuwalinda wananchi wote na Uhuru wa nchi yao..

Imenilazimu kuandika mada hii ili kupanua fikra zetu ktk weredi wa neno hili na matumizi yake hasa baada ya kuwasoma baadhi ya Wanasiasa na Wasomi tena wengine wanasheria wakisema hakuna haja wala haraka ya kuipata katiba Mpya isipokuwa kinachotakiwa zirekebishwe baadhi ya Ibara za kisiasa ktk katiba wanayodai imepitwa na wakati ili kuwezesha uchaguzi ujao uwe wa wazi, haki na usawa kwao wao. Tena inaonyesha wako karibu kufikia muafaka wa kuahirisha katiba ya wananchi ili kulinda maslahi ya wanasiasa wa pande zote mbili ambao hawawajibiki kwa wananchi isipokuwa kwa vyama vyao vya siasa.

Sasa leo hii hiyo KATIBA YA WANANCHI ilosiwamiwa kwa nguvu zote inaonekana kutupwa pembeni na maswala ya muafaka wa kisiasa kuchukua nafasi kusema kweli imesikitisha sana, yaani madai yote ya wananchi iwe kwa mtazamo wa kwanza ama wa pili unawekwa pembeni kupisha uwekekano wa uchaguzi ujao pasipo kupata ridhaa ya wananchi wenyewe ambao pengine (who knows) wapo radhi kwao uchaguzi ujuao uahirishwe hadi hapo katiba yao itakapo patikana kwanza.

Maoni yenu wana Jamii..

Siku nyingine unakuja na hoja nzuri za kizalendo; Lakini wakati mwingine unakuja na pumba nzito za ACT!.
 
Tumekuwa tukisoma na kusikia vyombo vya habari, vyama vya siasa na taasisi za kijamii wakitumia hili neno KATIBA YA WANANCHI hadi kufikia kundi moja la wajumbe wa bunge maalum la katiba kuunga Umoja wao na kujiita UKAWA. Tatizo la neno hili lipo ktk matumizi yake, na weredi umetofautiana sana baina ya Wananchi wenyewe, wanazuoni na wanasiasa na kwa sababu tofauti. Aidha maana hizi zimetumika kwa kuzingatia umuhimu wa katiba yenyewe na utunzi wake ama kutokana na tofauti za wananchi wenyewe ktk ufuasi wa vyama vyao vya kisiasa na upinzani wa kiutawala.

Sasa leo hii hiyo KATIBA YA WANANCHI ilosiwamiwa kwa nguvu zote inaonekana kutupwa pembeni na maswala ya muafaka wa kisiasa kuchukua nafasi kusema kweli imesikitisha sana, yaani madai yote ya wananchi iwe kwa mtazamo wa kwanza ama wa pili unawekwa pembeni kupisha uwekekano wa uchaguzi ujao pasipo kupata ridhaa ya wananchi wenyewe ambao pengine (who knows) wapo radhi kwao uchaguzi ujuao uahirishwe hadi hapo katiba yao itakapo patikana kwanza.

Maoni yenu wana Jamii..
Mkuu Mkandara, naomba nianze na sahihisho kidogo la lugha, ni weledi na sio weredi!.

Tanzania tangu tulipopata uhuru wetu, hatukuwahi kupata fursa ya kujitungia katiba yetu, hivyo hii ilikuwa ni fursa adimu ya sisi kama Watanzania kujitungia katiba yetu ambayo ndio ingekuwa katiba ya wananchi.

Utungwaji wa katiba is a process, ili kupata katiba ya wananchi, the process ilipaswa ianzie kwa wananchi, botom-top, na sio hii iliyoanzia kwa watawala na kuipeleka kwa wananchi, top-botom!, hivyo kwa process hii tulio anza nayo, hata tukitunga katiba nzuri kiasi gani, haiwezi kuwa ni katiba ya wananchi.

Watanzania walihitaji kupata "katiba bora", ili kupata katiba bora, ni lazima mchakato ungefuata kanuni za uundaji wa katiba bora "constitutional making process" uliowashirikisha wananchi kutoka mwanzo, lakini huu mchakato unaondelea, umeanzia juu kwa JK kutupa zawadi ya sadaka ya katiba mpya, hivyo kitakachopatikana hapa sio "katiba bora", bali "bora katiba!".

We had a chance kupata katiba bora, ila wale tuliowategemea, kutupigania kuelekea upatikanaji wa hiyo "katiba bora", walituangusha (Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge Mbele!")
na kuwa ni sehemu ya ule ule mchakato wa kuelekea kupata "bora katiba" haswa baada ya kulainishwa na jiuce, chai na vitafunwa!, hivyo wakatuingiza chaka na kuibarika process nzima ya kupata "bora katiba!", halafu leo process iko katikati kuelekea kupata "bora katiba!", then eti wanasita na kujidai eti sasa ndio wanataka "katiba bora!", no way!, no turning back!, tuwalazimishe waendelee na mchakato, tupata hiyo "bora katiba", halafu mbele ya safari, Mungu bariki, utakuja kufikia wakati, tutapata :katiba bora!.

Kwangu mimi, the process was wrong since day one, (Prof. Shivji Aukosoa Mchakato wa Katiba Mpya!)
kama walikubali, then hayo ni maji waliisha yavulia nguo, ni lazima wayaoge!.

Ili kupata "katiba bora" ya kiukweli, the process ingeanzia kwa wananchi (Mchakato Huu wa Katiba, ni Umasikini Wetu!)

  1. Kufanya a national convention, kuweka "Dira ya Taifa" kuwa jee tunataka kuunda taifa la aina gani?!.
  2. Baada ya kupata "dira", ndipo out hiyo national convention, ndipo tungeunda tume ya kukusanya maoni ya wananchi, wanataka nini ili kuitekeleza hiyo "dira!".
  3. Baada ya maoni kupatikana, wananchi wangewateua wawakilishi wao, kuunda bunge la katiba, "constituent assembly", ambao ndio wangekuwa na "peoples mandate" kuwaundia katiba!.
  4. Baada ya bunge la katiba, kutoa "katiba ya wananchi", then katiba hiyo ingerudishwa kwa wananchi kuipigia kura ya ndio ili kuipatia "peoples legitimacy!"
  5. Katiba hiyo iliyopatikana ndio ingekuwa "katiba bora", "katiba ya wananchi!".

Mchakato huu uliopo

  1. Umeanza bila dira wala mwelekeo, tunataka nini?!. Kwenda kuwauliza wananchi wasiojua lolote kuhusu katiba, na bila dira ya tunataka taifa la namna gani, kila mtu atasema lake na hayo ndio matokeo ya Tume ya Warioba kuja na rasimu ya serikali tatu iliyoegemea maoni ya walio wachache, kisha walio wengi kutishia kuikataa au kuyapindua!.
  2. Rais JK alipata wapi "peoples mandate" kututeulia tume ya Warioba bila any "national convention" Watanzania tunataka nini?!. Hiyo Tume ya Warioba ni Tume ya JK na matokeo ni Katiba ya JK na sio katiba ya watu!.
  3. Wajumbe wa bunge la katiba wameteuliwa na JK, amepata wapi mandate ya kututeulia wajumbe wa "constituent assembly?!, "peoples mandate", iko wapi?!. (Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna Alyetumwa na Wananchi!)
    Hata hao wabunge na wajumbe wa BLW, tuliwachagua kutuwakilisha kwenye baraza la kutunga sheria na sio kwenda kututungia katiba, hivyo wajumbe wote wa bunge maalum, hakuna hata mmoja aliyeteuliwa na wananchi kwenda kutungia katiba, hivyo hawana "peoples mandate!" kututungia katiba, hivyo katiba yoyote itakayotungwa na bunge hili, no matter how good it might be, kama haiwezi kuwa "katiba bora" au "katiba ya wananchi" , bali kitakacho patikana hapo ni "bora katiba!.
  4. Nimesisitiza kwa vile katiba itakayopatikana ni "bora katiba", then chochote kitakachopatikana tukipigie kura ya ndio, kwa sababu japo tulitaka "katiba bora", ili kitakachopatikana ni "bora katiba",
  5. "if you can't get what you want, then just take what you get!", then afadhali tuikubali hiyo "bora katiba" maana ndio "nusu shari" kuliko kuikataa maana tutaendelea na katiba iliyopo ambayo ndio " shari kamili!". "Heri nusu shari"..., na "moja shika sii kumi nenda rudi". Tuipigie kura ya ndio hiyo "bora katiba", tujipatie "bora katiba!", tusonge mbele na "bora katiba" mpaka tutakapokuwa tayari kupata "katiba bora!.
Pasco.
 

Tanzania tangu tulipopata uhuru wetu, hatukuwahi kupata fursa ya kujitungia katiba yetu, hivyo hii ilikuwa ni fursa adimu ya sisi kama Watanzania kujitungia katiba yetu ambayo ndio ingekuwa katiba ya wananchi.

Utungwaji wa katiba is a process, ili kupata katiba ya wananchi, the process ilipaswa ianzie kwa wananchi, botom-top, na sio hii iliyoanzia kwa watawala na kuipeleka kwa wananchi, top-botom!, hivyo kwa process hii tulio anza nayo, hata tukitunga katiba nzuri kiasi gani, haiwezi kuwa ni katiba ya wananchi.

Watanzania walihitaji kupata "katiba bora", ili kupata katiba bora, ni lazima mchakato ungefuata kanuni za uundaji wa katiba bora "constitutional making process" uliowashirikisha wananchi kutoka mwanzo, lakini huu mchakato unaondelea, umeanzia juu kwa JK kutupa zawadi ya sadaka ya katiba mpya, hivyo kitakachopatikana hapa sio "katiba bora", bali "bora katiba!".
Katiba ya Japan imetungwa na wanasheria 12 kutoka Marekani, imewafaa na ni moja ya nchi inayosifika kwa demokrasia Asia na duniani.

Si lazima katiba itoke kwenye vikao vya shina, matawi, wiloaya, mikoa na taifa.
Refferrendum ndiyo itakayoamua. Process inaweza ikatofautiana na ikaleta katiba nzuri tu, tena kwa bei rahisi.

Katiba ya US haikuwa hata na refferrendum, ni wanasheria wawili tu ndiyo waliyoiandika na ikakubaliwa na wawakilishi tu.

Sidhani kuwa kila kitu ni lazima tukaririshwe, tutalumbana mpaka 2020, ila hiyo isitunyime tumke huru ya uchaguzi, mgombea binafsi na mawaziri wasio wabunge.
We can have that tommorrow.
 
Huwezi kulikimbia bunge wakati hata hayo yanayosemwa maoni ya "wananchi" hayajaanza kujadiliwa.

Huwezi kutaka kukabiliana na changamoto za kitaifa huku ukitanguliza hisia dhaifu za kisiasa kutatua changamoto za kitaifa.

Kuzikimbia changamoto ni udhaifu wa kiwango cha juu kisiasa hasa ikichukuliwa kuwa, katiba itakayopitishwa bungeni lazima ikapigiwe kura na wananchi wote wenye haki kisheria. Kama wabunge watapitisha masuala ambayo yako nje ya matakwa ya wananchi, basi wananchi wataikataa katiba mpya kwenye sanduku la kura kwa sababu wananchi ndiyo wenye kauli ya mwisho kwenye Mchakato wa Katiba.

Kwa nini baadhi ya wabunge wa bunge maalum la katiba wanataka kufanya kazi ya wananchi kabla hata Rasimu ya Katiba haijapita bungeni. Ukiangalia hata historia ya katiba mbali mbali za nchi mbali mbali zilizopata mafanikio. Katiba inatungwa na watu wachache na inapitishwa na wananchi wengi. Wanasiasa wa Tanzania wanataka kutunga katiba na vile vile waipitishe wao wenyewe.

Kuna baadhi ya watu wanadai eti hawataki kuwa sehemu ya maamuzi mabaya ya kitaifa kwenye bunge Maalum la katiba ambalo wanadai "limejaa wanaCCM" lakini hao hao wanahudhuria kwenye bunge la Jamhuri wa Muungano ambalo kwa asilimia kubwa lina wabunge wa tiketi ya CCM. Kama hoja ni kujaa wanaCCM kwenye bunge Maalum la Katiba, kwa nini hizo hoja wasiziweke pia kwenye bunge la Jamhuri ya Muungano na wakasusia mijadala yote ya bunge la JMT.

Hizi kelele za kusema "wananchi wengi" hazina hata msingi wa hoja katika mantiki ya idadi ya wananchi nchini. Kama Rasimu ya Katiba yenye kurasa 106 imeandikwa kwa misingi ya maoni ya watu wengi kama tunavyoaminishwa, kwa nini hizo hoja ziwe tu kwenye sura mbili kati ya sura 17 na ibara 271?. Kwa nini sura 15 zilizobakia zisiwe pia katika misingi ya wengi waliotoa maoni?. Kwa nini kuna political cherry picking kwa suala hili la kitaifa.
 
Kwani Tofauti Kati Ya Mtazamo Wa Kwanza Na Wapili Ni Ipi, Mi Mbna Sioni Tofauti
 
Katiba ya Japan imetungwa na wanasheria 12 kutoka Marekani, imewafaa na ni moja ya nchi inayosifika kwa demokrasia Asia na duniani.

Si lazima katiba itoke kwenye vikao vya shina, matawi, wiloaya, mikoa na taifa.
Refferrendum ndiyo itakayoamua. Process inaweza ikatofautiana na ikaleta katiba nzuri tu, tena kwa bei rahisi.

Katiba ya US haikuwa hata na refferrendum, ni wanasheria wawili tu ndiyo waliyoiandika na ikakubaliwa na wawakilishi tu.

Sidhani kuwa kila kitu ni lazima tukaririshwe, tutalumbana mpaka 2020, ila hiyo isitunyime tumke huru ya uchaguzi, mgombea binafsi na mawaziri wasio wabunge.
We can have that tommorrow.

Mkuu unachosema ni sahihi, ya kuwa katiba inaweza kuundwa na watu wa chache wenye taaluma ya sheria hii nakubaliana nawe. Lakini hilo halitakubalika kwa hii nchi chini ya utawala wa dhalimu na shetani ccm. Kwani watakapo kuja na katiba isiyokidhi haja za huyu shetani wataikataa. Kama walivyofanya sasa. Tatizo ni ccm muda wote wanawaza ulaji.
 
Kwa sasa mimi sitaki kusikia kitu katiba mpya tena nataka katiba ya zamani kuendelea kutumika make wanasiasa hawa wa ukawa wanataka kufanya katiba ni sehemu ya kutafuta umarufu badala ya kujadili katiba tunamuomba rais avunje bunge halafu baada ya miaka hamsini ijayo ndiyo tuangalie hii katiba iliyopo kama inamatatizo kama haina tunasongambele ujinga wa wanasiasa kufanya hii ni sehemu ya kuuza sura wakome hii nchi siyo yao peke yao kwanza katiba siyo hitaji namba moja la watanzania tunataka maji,afya ,umeme na mengine mengi ya msingi ila siyo katiba.
 

Mkuu Mkandara, naomba nianze na sahihisho kidogo la lugha, ni weledi na sio weredi!.

Tanzania tangu tulipopata uhuru wetu, hatukuwahi kupata fursa ya kujitungia katiba yetu, hivyo hii ilikuwa ni fursa adimu ya sisi kama Watanzania kujitungia katiba yetu ambayo ndio ingekuwa katiba ya wananchi.

Utungwaji wa katiba is a process, ili kupata katiba ya wananchi, the process ilipaswa ianzie kwa wananchi, botom-top, na sio hii iliyoanzia kwa watawala na kuipeleka kwa wananchi, top-botom!, hivyo kwa process hii tulio anza nayo, hata tukitunga katiba nzuri kiasi gani, haiwezi kuwa ni katiba ya wananchi.

Watanzania walihitaji kupata "katiba bora", ili kupata katiba bora, ni lazima mchakato ungefuata kanuni za uundaji wa katiba bora "constitutional making process" uliowashirikisha wananchi kutoka mwanzo, lakini huu mchakato unaondelea, umeanzia juu kwa JK kutupa zawadi ya sadaka ya katiba mpya, hivyo kitakachopatikana hapa sio "katiba bora", bali "bora katiba!".

We had a chance kupata katiba bora, ila wale tuliowategemea, kutupigania kuelekea upatikanaji wa hiyo "katiba bora", walituangusha (Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge Mbele!")
na kuwa ni sehemu ya ule ule mchakato wa kuelekea kupata "bora katiba" haswa baada ya kulainishwa na jiuce, chai na vitafunwa!, hivyo wakatuingiza chaka na kuibarika process nzima ya kupata "bora katiba!", halafu leo process iko katikati kuelekea kupata "bora katiba!", then eti wanasita na kujidai eti sasa ndio wanataka "katiba bora!", no way!, no turning back!, tuwalazimishe waendelee na mchakato, tupata hiyo "bora katiba", halafu mbele ya safari, Mungu bariki, utakuja kufikia wakati, tutapata :katiba bora!.

Kwangu mimi, the process was wrong since day one, (Prof. Shivji Aukosoa Mchakato wa Katiba Mpya!)
kama walikubali, then hayo ni maji waliisha yavulia nguo, ni lazima wayaoge!.

Ili kupata "katiba bora" ya kiukweli, the process ingeanzia kwa wananchi (Mchakato Huu wa Katiba, ni Umasikini Wetu!)

  1. Kufanya a national convention, kuweka "Dira ya Taifa" kuwa jee tunataka kuunda taifa la aina gani?!.
  2. Baada ya kupata "dira", ndipo out hiyo national convention, ndipo tungeunda tume ya kukusanya maoni ya wananchi, wanataka nini ili kuitekeleza hiyo "dira!".
  3. Baada ya maoni kupatikana, wananchi wangewateua wawakilishi wao, kuunda bunge la katiba, "constituent assembly", ambao ndio wangekuwa na "peoples mandate" kuwaundia katiba!.
  4. Baada ya bunge la katiba, kutoa "katiba ya wananchi", then katiba hiyo ingerudishwa kwa wananchi kuipigia kura ya ndio ili kuipatia "peoples legitimacy!"
  5. Katiba hiyo iliyopatikana ndio ingekuwa "katiba bora", "katiba ya wananchi!".

Mchakato huu uliopo

  1. Umeanza bila dira wala mwelekeo, tunataka nini?!. Kwenda kuwauliza wananchi wasiojua lolote kuhusu katiba, na bila dira ya tunataka taifa la namna gani, kila mtu atasema lake na hayo ndio matokeo ya Tume ya Warioba kuja na rasimu ya serikali tatu iliyoegemea maoni ya walio wachache, kisha walio wengi kutishia kuikataa au kuyapindua!.
  2. Rais JK alipata wapi "peoples mandate" kututeulia tume ya Warioba bila any "national convention" Watanzania tunataka nini?!. Hiyo Tume ya Warioba ni Tume ya JK na matokeo ni Katiba ya JK na sio katiba ya watu!.
  3. Wajumbe wa bunge la katiba wameteuliwa na JK, amepata wapi mandate ya kututeulia wajumbe wa "constituent assembly?!, "peoples mandate", iko wapi?!. (Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna Alyetumwa na Wananchi!)
    Hata hao wabunge na wajumbe wa BLW, tuliwachagua kutuwakilisha kwenye baraza la kutunga sheria na sio kwenda kututungia katiba, hivyo wajumbe wote wa bunge maalum, hakuna hata mmoja aliyeteuliwa na wananchi kwenda kutungia katiba, hivyo hawana "peoples mandate!" kututungia katiba, hivyo katiba yoyote itakayotungwa na bunge hili, no matter how good it might be, kama haiwezi kuwa "katiba bora" au "katiba ya wananchi" , bali kitakacho patikana hapo ni "bora katiba!.
  4. Nimesisitiza kwa vile katiba itakayopatikana ni "bora katiba", then chochote kitakachopatikana tukipigie kura ya ndio, kwa sababu japo tulitaka "katiba bora", ili kitakachopatikana ni "bora katiba",
  5. "if you can't get what you want, then just take what you get!", then afadhali tuikubali hiyo "bora katiba" maana ndio "nusu shari" kuliko kuikataa maana tutaendelea na katiba iliyopo ambayo ndio " shari kamili!". "Heri nusu shari"..., na "moja shika sii kumi nenda rudi". Tuipigie kura ya ndio hiyo "bora katiba", tujipatie "bora katiba!", tusonge mbele na "bora katiba" mpaka tutakapokuwa tayari kupata "katiba bora!.
Pasco.
Mkuu heshima yako na natanguliza shukran zangu za dhati ktk sahihisho ili kuleta maana kamili ya kile nilichokusudia, Ila ujue miye Mkerewe hizo R sii katika maandishi tu bali zipo ulimini....hahaha !

Swala la KATIBA BORA kusema kweli mkuu wangu nakubaliana na wewe sana tu hasa pale swala la DIRA linapokosekana toka mwanzo. Huu ngogoro wa serikali 2 au 3 ni matokeo ya kukosekana kwa DIRA hivyo hata kama tukiwa na serikali 2 au 3 bado mfumo wa utawala usokuwa na dira utaendeleza yale yale sawa na kuongeza idadi ya mikoa au wilaya (muundo wa serikali toka mikoa 17 hadi utitiri) lakini haibadilishi kasi ya maendeleo ktk uzalishaji ama pato la wananchi isipokuwa ni katika misingi ya kugawana maskini. Mimi naamini kabisa tuwe na serikali 2 au 3 haiwezi kubadilisha kitu ikiwa nchi haina DIRA ili kuweza kubadilisha MFUMO wa UTAWALA na MILIKI kwa niaba ya wananchi wake (Katiba).

Sijaona mbele sii kwa sababu tu ya ukiukwaji wa taratibu za utunzi wa katiba bali hata hapa walipofikia leo sidhani kama tungeweza ipata hiyo Bora Katiba ilotokana na huu upofu, uziwi na ukaidi wa kujua kwingi kulikoondoa maarifa. Sisi ni sawa na kaa walovuliwa baharini na kuwekwa mktk kapu, hata tukianzia chini basi kwa kila atakaye panda juu lazima ushushwe chini japo ilikuwa ndio njia ya sote tutoke. Hivi Ndivyo Tulivyo na haya yanayotokea sii maajabu bali isingekuwa tofauti na ukweli huu maana sisi tunataka kuandika Katiba hii kutokana na chuki ya chama tawala badala ya kutambua mapungufu ya Kikatiba yapo ktk Utekelezaji wake.

Sijawahi kupima ubora wa katiba za nchi tofauti zilizoundwa kwa taratibu tofauti nikaijua ipi ilokuwa bora zaidi isipokuwa tu nachoweza kusema ni kwamba KATIBA BORA ni ile inayowalenga wananchi sawa na serikali bora ni ile inayotanguliwa na kufahamu mahitaji ya wananchi wake, kutambua mapungufu ya kifikra na kisera ktk mazingira waliyopo ya kisiasa na kiuchumi, kuheshimu mila na desturi kiasi kwamba ikatunga falsafa na sera zake ambazo wananchi wengi wakazikubali na kuichagua serikali hiyo iwaongoze kufikia matumaini walopewa.

Kwa maana nyingine, naamini sii lazima katiba ya chama chochote cha Siasa lazima itungwe na wanachama wake wote ama wengi ili kuhalalisha Ubora ulotokana na kukusanya mawazo yao, bali kinachotakiwa ni watunzi ama waandishi kutambua TAIFA lao linahitaji mwongozo upi na njia zipi ili kuwaletea Wananchi maendeleo pasipo kugharimu UTU wao ambao ndio siri ya UHURU walopigania. Na katika Utekelezaji wa falsafa na sera walozichagua, ndipo tunakuta kinyume chake yaani wananchi ndio wanakuwa responsible na Utekelezaji wa dhana hiyo ili kulijenga TAIFA lao! (Ask not what your country can do for you, ask what you can do for your country} huu ni mrazamo wangu.

Sasa aidha falsafa hiyo iwe imetokana na wananchi kuchangia mawazo yao ama imetokana na kundi la watu wachache, Ubora wake utajulikana ukisha wekwa ktk utekelezaji na kama haitekelezaki, basi hizo hiyo falsafa na sera hazifai japo ziliwavutia na kuleta maana zaidi ya nyinginezo. Sisi sote tunaweza dhani kwa kukisia Ubora wa falsafa ama sera ya chama fulani lakini kwa upana wake Ubora wake hutegemea kwanza uongozi utakao shika madaraka maana kiongozi mmoja chini ya falsafa na sera hizo hizo anaweza kuwa na mapungufu, udhaifu ama fisadi kinyume cha mwongozo ulokubaliwa, pia wananchi wanaweza kuwa sababu ya kutokuwa tayari kushiriki kikamilifu ktk utekelezaji wa falsafa na sera hiyo kutokana na kukosekana mtaji wa wananchi (human capital), na ukakuta wanasiasa wakikashifu sera mbovu za chama!

Hivyo hata tunapochagua chama cha kutuongoza iwe CCM au Chadema, wananchi hufikiria (kwa dhana) ama kukubali kwamba falsafa na sera hizi ndizo zinaridhisha na kukubaliwa na wananchi wengi lakini ukweli wa ubora wake huja kupimwa ktk utekelezaji wake. Kwa maana hii hata kama Katiba hii ingetokana na wananchi (from bottom to the top) ama kwa njia hii ya toka juu kwenda chini, mwisho wake ni kwamba wananchi ndio watakuwa na sauti ya mwisho, watakuwa na jukumu la Kupitisha ama kuikataa katiba hiyo japo bado sijaelewa utaratibu gani utatumika ktk wananchi kuipitisha katiba yenye kurasa kibao ingesomeka vipi kiurahisi na wananchi.. Hivyo kweli katiba isingepita pasipo ridhaa ya wananchi ambao kama ulivyosema asilimia kubwa ni mbumbumbu, hawajui tofauti ya katiba bora na bora katiba, wala hawajawahi kusoma hata katiba hii iliyopo na kuelewa mapungufu yake isipokuwa kwa kutazama mwendo wa utawala wa CCM, sijui mwanzo ama mwisho upi ulokuwa mzuri.

Kilichonishinda kuelewa mimi leo hii ni pale hawa wabunge wa hili bunge la Katiba wanapoanza wao kubishana juu ya muundo wa serikali kila mmoja wao akitumikia hisia zake za UZAWA pasipo wao wote kujua mwisho wa siku wananchi watapitisha katiba hiyo ikiwa ndani ya serikali 2 au 3 maana walochangia mapendekezo ya rasimu hii kwenye muundo wa serikali ni kundi la watu walokuwa na kero zao. sasa najiuliza, Hivi kweli Kero za wananchi husababisha utunzi wa katiba mpya ama kero hutokana na wananchi kutoridhika na Utawala uliopo? Hivi kweli wananchi wa bara na visiwani wameitaka katiba mpya kutokana na KERO zao ama imetokana na MAPUNGUFU ya katiba iliyopo kulingana na mahitaji ya TAIFA letu ama hii katiba imetumiwa tu kama njia ya kuzigawa Tanganyika na Zanzibar pasipo kufanyika referundum maana wasemavyo wabunge hawa wa baraza maalum hili la katiba ni kwamba ikisha pitishwa na bunge lao, ndio IMETOKA!..

Haya, alivyosema ndugu yetu MwanaDiwani, ikiwa hawa wabunge wetu wamekwamia katika sura 2 kati ya sura 17 zenye Ibara 271, tokana na fikra na utashi wao iwe wa kichama au ubinafsi, hivi kweli kuna mategemeo ya kuipata Katiba Mpya wakati wowote ule ilihali tumeona wabunge hawa wote sii wawakilishi wa wananchi? Hata kesho wakiacha swala la serikali 2 au 3 wakiingia sura nyingine ya madaraka watakwama kwa sababu madaraka hayawezi kugawanywa pasipo kuwepo muundo wa serikali ambazo hawakubaliani = Watakesha tena kwa matusi ya kuitana majina! Binafsi yangu kama mwananchi nasema sioni tofauti baina ya Ntarahamwe na Al Shabab! na wanachotakiwa ni wakue kifikra waache fitna zao na ambition zao nyuma maana katiba bora haitangulii na kuwahakikishia maslahi ya vyama vyao ktk uchaguzi ujao

lazima wafikirie kwa mapana zaidi maana katika hali hii hata wakirudi bungeni na nyodo zao za Utanganyika na Uzanzibar, watajikuta ktk maswala mazito ya sheria za uchaguzi nazo zitaleta matatizo kwa sababu Ubunge wa mjumbe yeyote wa UKAWA ataitaka Tanganyika yake na mwingine ataitaka Zanzibar yake hivyo bado swala la kugawanyika litajitokeza kama linavyoendelea ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano, ambako wazi wazi wabunge hutupiana vishoka vya Utanganyika na Uzanzibar kutokana na mfumo mbaya wa Mambo yasokuwa ya Muungano (kugawana umaskini) kuwa ndiyo sababu kubwa ya mtafaruku uliopo. Sasa naposikia viongozi wetu na hasa hawa wasomi wanaposema bora waweke kando swala hili la Muundo wa serikali bado nashindwa kuelewa watazungumzia mambo yapi yawe ya Muungano na yapi yasiwe ya Muungano ikiwa rasimu imependekeza mambo 7 tu yawe ya serikali ya JMT kwa kufuata mfumo wa serikali 3!
 
Huwezi kulikimbia bunge wakati hata hayo yanayosemwa maoni ya "wananchi" hayajaanza kujadiliwa.

Huwezi kutaka kukabiliana na changamoto za kitaifa huku ukitanguliza hisia dhaifu za kisiasa kutatua changamoto za kitaifa.

Kuzikimbia changamoto ni udhaifu wa kiwango cha juu kisiasa hasa ikichukuliwa kuwa, katiba itakayopitishwa bungeni lazima ikapigiwe kura na wananchi wote wenye haki kisheria. Kama wabunge watapitisha masuala ambayo yako nje ya matakwa ya wananchi, basi wananchi wataikataa katiba mpya kwenye sanduku la kura kwa sababu wananchi ndiyo wenye kauli ya mwisho kwenye Mchakato wa Katiba.

Kwa nini baadhi ya wabunge wa bunge maalum la katiba wanataka kufanya kazi ya wananchi kabla hata Rasimu ya Katiba haijapita bungeni. Ukiangalia hata historia ya katiba mbali mbali za nchi mbali mbali zilizopata mafanikio. Katiba inatungwa na watu wachache na inapitishwa na wananchi wengi. Wanasiasa wa Tanzania wanataka kutunga katiba na vile vile waipitishe wao wenyewe.

Kuna baadhi ya watu wanadai eti hawataki kuwa sehemu ya maamuzi mabaya ya kitaifa kwenye bunge Maalum la katiba ambalo wanadai "limejaa wanaCCM" lakini hao hao wanahudhuria kwenye bunge la Jamhuri wa Muungano ambalo kwa asilimia kubwa lina wabunge wa tiketi ya CCM. Kama hoja ni kujaa wanaCCM kwenye bunge Maalum la Katiba, kwa nini hizo hoja wasiziweke pia kwenye bunge la Jamhuri ya Muungano na wakasusia mijadala yote ya bunge la JMT.

Hizi kelele za kusema "wananchi wengi" hazina hata msingi wa hoja katika mantiki ya idadi ya wananchi nchini. Kama Rasimu ya Katiba yenye kurasa 106 imeandikwa kwa misingi ya maoni ya watu wengi kama tunavyoaminishwa, kwa nini hizo hoja ziwe tu kwenye sura mbili kati ya sura 17 na ibara 271?. Kwa nini sura 15 zilizobakia zisiwe pia katika misingi ya wengi waliotoa maoni?. Kwa nini kuna political cherry picking kwa suala hili la kitaifa.
Duh
 
Back
Top Bottom