HATUA YA NNE NI KUSEMA KWA HERI
Hii ni hatua ngumu sana kukutana nayo kwani ni hatua ambayo unakubali na kumwambia kwa heri Yule amekuacha.
Hapa ni hatua ambayo unakubali kwamba ni kweli mahusiano yamefika mwisho.
Hapa una admit kwamba huyu mtu hayupo tena katika maisha yangu na sasa natakiwa kuendelea mwenyewe.
Hata hivyo wapo ambao hujikuta wanakwamba wakifika hapa kwani wakati mwingine huamini sasa kwa heri na baada ya wiki mbili anarudi tena kuwaza kama inawezekana wakarudiana kitu ambacho hata aliyemuacha hana mpango kabisa.
Kumbuka ukitaka kuwa mtu huru na uweze kuendelea mbele jambo la msingi katika hatu hii ni wewe
KUMSAMEHE.
Andika kwenye karatasi yale unaamini mpenzi wako amekukosea na yasome na kuomba Mugu akusamehe na yeye pia umsamehe.
Bila kusaheme inakuwa ni sababu muhimu sana ya kuzuia Baraka zako kwwa mahusiano yajayo na mahusiano yako wewe na Mungu.
Tunaweza kusaheme kwa sababu Mungu anatusamehe.
Inawezekana wakati upon a mpenzi wako kulikuwa na maeneo muhimu ambayo mlikuwa mnaenda pamoja inaweza kuwa ni kanisa, hotel, viwanja na sehemu za vacation na tangu mmeachana ukizikumbuka hizo sehemu unajisikia uchungu sana.
Kama unapotembelea hizo sehemu unajisikia hofu na uchungu kitu cha msingi kufanya ni wewe kwenda na rafiki zako/yako na ziombee kwa Jina la Yesu.
Mungu atakupa amani na utajisikia raha kuwepo hizo sehemu tena.
HATUA YA TANO NA SITA KUJIJENGA NA MATUMAINI MAPYA
Kwenye hatua hizi mbili sasa unaweza kuiongelea future huku ukiwa na matumaini mapya.
Hata hivyo tunatakiwa kukumbuka kwamba kukiwa na tukio la kuachana huwa kunakuwa na matokeo ya aina tatu kwa aliyeathirika.
Kwanza unaweza kubadilika na kuwa maisha mazuri zaidi, pia unaweza kubadilika na kuwa na maisha ya ovyo kabisa au tatu unaweza kubadilika na kurudi katika maisha yako kama kawaida.
Mara nyingi huwa ngumu sana kuwa na mabadiliko ya kuwa na maisha mazuri kama umekataliwa, umeachwa, upo dumped au rejected hata hivyo ukisimama vizuri na kumwangalia Mungu na kuitopoteza focus ya kuwa positive katika mtazamo wako unaweza kuwa na maisha bora tena na yenye Baraka