Ningemshauri huyu dada lakini ndio hatuna mazoea kabisa

Ningemshauri huyu dada lakini ndio hatuna mazoea kabisa

Vishu Mtata

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2019
Posts
20,598
Reaction score
44,425
Huyu dada ni mpangaji mwenzangu hapa Kunecity (DSM). Hii ishu ilianza wiki kadhaa nyuma nilimskia mpanga mwenzangu akiongea na ndugu zake wa kaskazini uko nadhani ni moshi. Alikua anawashawishi kutoa kiasi kadhaa si chini ya laki 5 alianza na mwanamke akamshawishi kwa siku kadhaa uyo bidada akaingia kingi sasa ikabaki kumshawishi baba ake nae ajiunge na iyo biashara. Kiukweli mi sikujua ni biashara gani na wala sikutaka kufatilia nikidhani ni mitikasi ya mjini tu hapa na ukizingatia imekaa kifamilia familia basi ata sikutaka kujua.

Sasa jana jioni ndo nikajua bila hata kutarajia kumbee bwana ni walewale ndugu zetu wa lete watu wako wawili na wao wakileta wawili unapata commision ya million kadhaa na blah blah zao zile. Ayo yote nimeyajua alipokua anamshawishi rafiki yake nae aingie kingi daah nikamsikitia bidada wa watu anamwambia unamjua tajiri namba 2 duniani nae alipitia huku huku aliacha shule akaanza izi biashara mpaka akawa tajiri. Jaman jaman hawa watu wanatumia dawa gani kushawishi watu yani ukimskia uyu dada utadhani yeye ndie mwanzilishi wa hii kampuni X. Anazidi kumshawishi ati atapata offer kibao kutembelea nchi mbalimbali na kulala hoteli za nyota 3 hadi 5 pale akifanya kazi yake vyema na izo offer sio lazima apate yeye zote anaweza kuamua tu nani ambless akalale hoteli aliyoambiwa yeye alale na anamchagua mtu wake yeyote tu wa karibu.

Tatizo sijazoeana na uyu mdada ni salamu tu na kupita ivi walau ningeshauri chochote ila ndo ivo kazama mazima kwa hiyo kampuni kubwa duniani kwa usambazaji wa vitu mbalimbali na kama mjuavyo maisha ya kimjini mjini haya kuingilia mambo ya watu nikaona bora nije kuwapa story wanaJF.

Mimi hawa jamaa nilishawahi kwenda hadi uko ofisini kwako ilikua ni moroco nadhani mwaka juzi wana story nyingi za kufikilika. Nakumbuka niliwatafuta baada ya kupata mawasiliano yao fb nikaambiwa niende uko ofisini kwao basi bna tukaingizwa kwenye kiukumbi hapo hapo ofisini kwao kwasababu tulikua wengi kidogo. Wakatoa ushawishi waoo na shuhuda za uongo na ukweli, mwisho nikaja kugundua kua mule ndani walengwa tupo wachache ila wengi ni wenzao waliojifanya nao ni mala ya kwanza kwenda pale ili ukifika wakati wa kutoa pesa wale wenzao waanze kutoa kwa hamasa na sie walengwa tuhamasike tutoe chap aisee niliwastukia pale nikayeya walikua wanapiga simu mpaka walichoka sasa.

Bidada kauvaa ni suala la muda tu.
 
Kama ana miaka chini ya 35 achana naye, kupoteza ni sehemu ya maisha. Ni kujifunza pia.

Mimi kuna mdada hapa, anajifanya mjuviii anajua kila kitu, mzee wa fursa. Anaona wenzake wote wajinga.

Ameacha kazi ana mwezi sasa, anapelekeshwa na hao GNLD.

Kumshauri mtu aliyeingia huko ni kujitafutia chuki na ubaya, maana ukishaubgia kule unakuwa full radicalized yaani unafanywa msukule.

Kumshauri kwamba hizo kampuni ni mbaya ni sawa na kumdiss Diamond mbele ya Baba Levo au shabiki yake yoyote, au kumdiss Gwajima, au Kakobe mbele ya waumini wao au kumdiss MAGU mbele ya MATAGA. Hao ni watu wa kuwahurumia na kuwapa muda.

Binafsi nina brother alishawahi kuwa huko, mimi nilimwacha tu, akachoka mwenyewe akaona hailipi akaachana nayo.

Simple.

People with independent minds are very few.

Tena sasa hivi wanabanwa balaa, kila week seminar za kwenda kufundwa kisaikolojia, huku wakiwa limited kiakili wasiwasikilize wengine.

Wanaambiwa, ukijidanganya kuwasikiliza MEDIA au WATU wengine umekwisha. Lengo wawasikilize wao tu, magwiji wa hizo kazi.
 
Sio kampuni X itaje ni Qnet, Smile we care au?? Enewei wajinga ndio wali wao jamaa hawatumii uchawi wowote ila siku zote tapeli anatumia akili kuyashinda madhaifu ya mtu unakuta jitu ukiliambia kuna mchongo wa Million kadhaa domo lnatema udenda kwa tamaa acha wanyooshwe
Mkuu kuna nyingine inaitwa forsage na kuna mulla empire vp mbona wanashiriki wanaleta feedback kuwa zinalipa.
 
Hakuna fedha inayopatikana kirahisi hivyo watu wajiandae ilivyo ili waweze kupata fedha vinginevyo watajiongezea mizigo majumbani mwao kwa kuendekeza dezo.
 
Mkuu kuna nyingine inaitwa forsage na kuna mulla empire vp mbona wanashiriki wanaleta feedback kuwa zinalipa
Mkuu izo mambo huwa zinalipa mwanzo zinapoanza kufahamika ili watu waamini utapeli unaanza ikishakua kubwa ni kama ishu za kina Mr. Kuku mwisho wa siku ni hasara tu
 
Kajaribu kuingia uone moto wake mkuu.
Forsage nilijiunga ila nilikubali nimepigwa 17k ila ni kazi sana kushawishi mtu kujoin japo nilipata mmoja tuu alivyojiunga nikapata sh.6k ila roho iliniuma kwa kuwa ni kama unatapeli watu maana sio kila atakaejiunga atakuwa na power ya kushawushi kama niliyokuwa nayo hivyo ni kama ningekuwa nakula hela za watu.
 
Forsage nilijiunga ila nilikubali nimepigwa 17k ila ni kazi sana kushawishi mtu kujoin japo nilipata mmoja tuu alivyojiunga nikapata sh.6k ila roho iliniuma kwa kuwa ni kama unatapeli watu maana sio kila atakaejiunga atakuwa na power ya kushawushi kama niliyokuwa nayo hivyo ni kama ningekuwa nakula hela za watu.
Hayo makitu hayafai mkuu. Zinaharibu sana target kwenye maisha ya wengi. Hasa wasiokuwa na ufaham kabisa na hiyo kitu.
 
Mstue ndugu yangu utapata dhawabu Kwa Mwenyezi Mungu,na wewe utakujaepushwa Kwa njia ambazo hukutarajia
 
Hivi we unadhani hata kama mngekuwa mmezoeana ndio angekusikiliza? Wakishaanzaga huu ujinga asee hawasikii. Yanaambiwaga watu watakukatisha tamaa usiwasikilize, so unapoanza tu kumshauri anakuweka kwenye lile kundi alilopewa tahadhari kule qnet, na kweli hakusikilizi hata kama ni mumewe!
 
Mstue ndugu yangu utapata dhawabu Kwa Mwenyezi Mungu,na wewe utakujaepushwa Kwa njia ambazo hukutarajia
Suala sio kumshtua je ataeleweka?
Ushauri wa kwanza ni wako mwenyewe.

ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO
 
Back
Top Bottom