Ningekuwa mwanachama wa CHADEMA....

Ningekuwa mwanachama wa CHADEMA....

Karani wa Mahakama au Baraza la Ardhi,Kodi na kadhalika
Kuna mtu ana division two ya 10 points HKL ana umri wa miaka 32,anapenda sheria anafanya kaz ingine, anataka kusoma unamshauri asome dip au degree open university

muosha rungu
 
Namba 5, hawawezi kujenga ofisi wakati wanajua Chadema ni chama cha kupita tu kitakufa. Jana nilikuwa na Mwanachadema mmoja pale Mwanza anasema kwa sasa Chadema kimebaki kuwa kikundi cha kusaidiana ktk ugonjwa na misiba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mtu ana division two ya 10 points HKL ana umri wa miaka 32,anapenda sheria anafanya kaz ingine, anataka kusoma unamshauri asome dip au degree open university

muosha rungu
Kwa ufaulu huo,aweza kusoma degree kwenye vyuo mbalimbali nchini.
 
Ningekuwa mwanachama wa CHADEMA ningefanya mambo mbalimbali. Kwanza, ningetambua kuwa CHADEMA ni chama 'chenye wenyewe'. Yaani, katika CHADEMA kuna waanzailishi wake na ndiyo wenye chama chao. Hivyobasi, ningekuwa na wajibu wa kulijua hilo; kuwatii na kuwaheshimu wenyechama chao na kuwa na mipaka katika kujadili na kutoa maoni yangu.

Pili, ningejiuliza, kwa kuwa kwangu CHADEMA nimechangia/nimefanya nini la kukumbukwa? Yaani, nimechangia kipi hasa katika kuifikisha CHADEMA ilipo sasa. Si kinyume chake, yaani, nimepata nini tangu nikiwa CHADEMA hadi sasa. Utii wangu na kupambana kwangu kama mwanachama wa CHADEMA vingejikita katika kipimo cha mchango wangu.

Tatu, ningemsifu Mwenyekiti wa sasa wa CHADEMA Freeman Mbowe kwa mchango wake, hasa wa kiuongozi, hata kuifikisha CHADEMA ilipo. Ningemsifu kwa kushiriki tangu kuanzishwa kwa CHADEMA chini ya Mzee Edwin Mtei hadi kupata Wabunge na hatimaye kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.

Nimgemsifu katika falsafa zake za 'kiuanaharakati' zilizokiinua chama. Ningewaomba wanachama wenzangu tumuandalie zawadi nzuri Mwenyekiti wetu kumpongeza kwa mafanikio yaliyofikiwa tangu awe Mwenyekiti. Mwisho mwishoni, ningewaomba wanachama wenzangu tumshauri Mwenyekiti Mbowe asigombee tena Uenyekiti mwakani. Tungemfanyia sherehe baab-kubwa!

Nne, ningejenga hoja na wenzangu ya kuwa makini katika kupokea wanachama toka vyama vingine ambao huhamia hasa wakati wa uchaguzi mkuu. Hawa huhamia kimaslahi kuliko kupendezwa na Ilani, Itikadi na Falsafa za chama. Baada ya uchaguzi, hata kama wameshinda katika nafasi wanazoaminiwa, huwa na ukakasi katika kusema na kutenda kwao.

Tano, ningewashauri wanachama wenzangu na viongozi wetu wa CHADEMA KUJIKITA KATIKA MAMBO MAWILI MAKUBWA. La kwanza ni ujenzi wa Ofisi kuanzia Makao Makuu hadi huko kwenye ofisi za Wilaya. La pili, ni kuendelea kujitangaza, hata kama ni kimyakimya, hasa katika sehemu za vitongoji na vijiji. Baadaye, tujikite ngazi kwa ngazi kwa uchaguzi wa S/Mitaa, Udiwani na Ubunge.

Hakika, ningekuwa mwanachama wa CHADEMA, ningeyafanya hayo.
39923951_2182251265390183_9105782042813005824_n.jpg

Choo cha Wagonjwa katika Zahanati ya Namalembo huko Mtwara, katika hali ya kutia huruma, ile hali tunatumia mabilioni kurudia chaguzi zisizo za lazima na zisizo na maana.
 
Unacopy uandishi wa Zitto huku ukijiita msomi wa Chuo cha Kata Udsm

Mtaumbuka sana sana sana, Msomi Kama wewe Tafuta aina ya uandishi sio wa kuiga toka kwa Zitto kabwe, Pole sana mkuu

Kila Sehemu kuna wenyewe hata Udsm ina wenyewe,

Ccm mpya ina wenyewe

Ccm ya kinana Ilikuwa na wenyewe

Kila ofisi Kuna wenyewe.

Mbona Wewe Unafanya kazi zaidi ya miaka Saba Kwanini usiache kazi uruhusu damu changa

Unaogopa nini? Acha kazi hapo Udsm uuze maharage kwa mtogole
kamanda umeandika nini..hapa.. total.confusion
 
Nani anaweza kumkosoa magufuli? Ccm haina wenyewe?
aaahah kwa hiyo umekubaliana na uzi huu。safi kabisaaa..ni bora wewe kuliko wale wengine ambao wangeanza kupiga mayowe..
 
Back
Top Bottom