Ha ha ha, umeona eeh?Vijana wanajikana wenyewe! Mtoa post
Why?Mbowe akiachia ngazi kama M/Kiti CDM inakufa asbuhi kweupeeeee
Kwa hiyo mnaiiga CCM?Nani anaweza kumkosoa magufuli? Ccm haina wenyewe?
Kutokana na jinsi ninavyofuatilia comment zako wewe ni mwanasheria/wakili msomi inafaa sana uwe mwanachama wa chadema, au mojawapo wa vyama vya upinzani ili uwe huru kusaidia wanyonge wanaonyanyasika ndani ya taifa letu.Kwasasa, na tangu kuzaliwa kwangu, sina chama.
Kwa hiyo Sacco's inasajiliwa na msajili wa vyama vya siasa? Au kama ni Sacco's akitoka mbowe haitakuwa tena Sacco's?
Kijana mzuri kabisa. Jambo moja zuri ni kumuacha Mhe. Mbowe akaandaa mrithi wake ili wakati Magufuli anaondoka madarakani ( 2025) na kwenye uongozi wa chama chake naye aondoke. Watu wapya waingie kwenye shughuli za kisiasa.Ningekuwa mwanachama wa CHADEMA ningefanya mambo mbalimbali. Kwanza, ningetambua kuwa CHADEMA ni chama 'chenye wenyewe'. Yaani, katika CHADEMA kuna waanzailishi wake na ndiyo wenye chama chao. Hivyobasi, ningekuwa na wajibu wa kulijua hilo; kuwatii na kuwaheshimu wenyechama chao na kuwa na mipaka katika kujadili na kutoa maoni yangu.
Pili, ningejiuliza, kwa kuwa kwangu CHADEMA nimechangia/nimefanya nini la kukumbukwa? Yaani, nimechangia kipi hasa katika kuifikisha CHADEMA ilipo sasa. Si kinyume chake, yaani, nimepata nini tangu nikiwa CHADEMA hadi sasa. Utii wangu na kupambana kwangu kama mwanachama wa CHADEMA vingejikita katika kipimo cha mchango wangu.
Tatu, ningemsifu Mwenyekiti wa sasa wa CHADEMA Freeman Mbowe kwa mchango wake, hasa wa kiuongozi, hata kuifikisha CHADEMA ilipo. Ningemsifu kwa kushiriki tangu kuanzishwa kwa CHADEMA chini ya Mzee Edwin Mtei hadi kupata Wabunge na hatimaye kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Nimgemsifu katika falsafa zake za 'kiuanaharakati' zilizokiinua chama. Ningewaomba wanachama wenzangu tumuandalie zawadi nzuri Mwenyekiti wetu kumpongeza kwa mafanikio yaliyofikiwa tangu awe Mwenyekiti. Mwisho mwishoni, ningewaomba wanachama wenzangu tumshauri Mwenyekiti Mbowe asigombee tena Uenyekiti mwakani. Tungemfanyia sherehe baab-kubwa!
Nne, ningejenga hoja na wenzangu ya kuwa makini katika kupokea wanachama toka vyama vingine ambao huhamia hasa wakati wa uchaguzi mkuu. Hawa huhamia kimaslahi kuliko kupendezwa na Ilani, Itikadi na Falsafa za chama. Baada ya uchaguzi, hata kama wameshinda katika nafasi wanazoaminiwa, huwa na ukakasi katika kusema na kutenda kwao.
Tano, ningewashauri wanachama wenzangu na viongozi wetu wa CHADEMA KUJIKITA KATIKA MAMBO MAWILI MAKUBWA. La kwanza ni ujenzi wa Ofisi kuanzia Makao Makuu hadi huko kwenye ofisi za Wilaya. La pili, ni kuendelea kujitangaza, hata kama ni kimyakimya, hasa katika sehemu za vitongoji na vijiji. Baadaye, tujikite ngazi kwa ngazi kwa uchaguzi wa S/Mitaa, Udiwani na Ubunge.
Hakika, ningekuwa mwanachama wa CHADEMA, ningeyafanya hayo.
Hamia ccm sasa, huu ndio muda wanagawana madaraka, mzee kasema kama upo nje ya ccm hawezi kukuteuwa.Kwasasa, na tangu kuzaliwa kwangu, sina chama.
Kwa point zipi kwamba asigombee tena? Wewe ndio wale wale wa CCM wanaolalamika kuwa Mbowe ndie anaeiua CHADEMA na hawamtakiNingekuwa mwanachama wa CHADEMA ningefanya mambo mbalimbali. Kwanza, ningetambua kuwa CHADEMA ni chama 'chenye wenyewe'. Yaani, katika CHADEMA kuna waanzailishi wake na ndiyo wenye chama chao. Hivyobasi, ningekuwa na wajibu wa kulijua hilo; kuwatii na kuwaheshimu wenyechama chao na kuwa na mipaka katika kujadili na kutoa maoni yangu.
Pili, ningejiuliza, kwa kuwa kwangu CHADEMA nimechangia/nimefanya nini la kukumbukwa? Yaani, nimechangia kipi hasa katika kuifikisha CHADEMA ilipo sasa. Si kinyume chake, yaani, nimepata nini tangu nikiwa CHADEMA hadi sasa. Utii wangu na kupambana kwangu kama mwanachama wa CHADEMA vingejikita katika kipimo cha mchango wangu.
Tatu, ningemsifu Mwenyekiti wa sasa wa CHADEMA Freeman Mbowe kwa mchango wake, hasa wa kiuongozi, hata kuifikisha CHADEMA ilipo. Ningemsifu kwa kushiriki tangu kuanzishwa kwa CHADEMA chini ya Mzee Edwin Mtei hadi kupata Wabunge na hatimaye kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Nimgemsifu katika falsafa zake za 'kiuanaharakati' zilizokiinua chama. Ningewaomba wanachama wenzangu tumuandalie zawadi nzuri Mwenyekiti wetu kumpongeza kwa mafanikio yaliyofikiwa tangu awe Mwenyekiti. Mwisho mwishoni, ningewaomba wanachama wenzangu tumshauri Mwenyekiti Mbowe asigombee tena Uenyekiti mwakani. Tungemfanyia sherehe baab-kubwa!
Nne, ningejenga hoja na wenzangu ya kuwa makini katika kupokea wanachama toka vyama vingine ambao huhamia hasa wakati wa uchaguzi mkuu. Hawa huhamia kimaslahi kuliko kupendezwa na Ilani, Itikadi na Falsafa za chama. Baada ya uchaguzi, hata kama wameshinda katika nafasi wanazoaminiwa, huwa na ukakasi katika kusema na kutenda kwao.
Tano, ningewashauri wanachama wenzangu na viongozi wetu wa CHADEMA KUJIKITA KATIKA MAMBO MAWILI MAKUBWA. La kwanza ni ujenzi wa Ofisi kuanzia Makao Makuu hadi huko kwenye ofisi za Wilaya. La pili, ni kuendelea kujitangaza, hata kama ni kimyakimya, hasa katika sehemu za vitongoji na vijiji. Baadaye, tujikite ngazi kwa ngazi kwa uchaguzi wa S/Mitaa, Udiwani na Ubunge.
Hakika, ningekuwa mwanachama wa CHADEMA, ningeyafanya hayo.
andiko lako lina ukakasi , hao wenye chadema unaowataja kwenye namba 1 yako ni akina nani ?
Asante Mkuu,najitahidi nionekane.Unausaka uteuzi kwa nguvu lakini uonekani. pole sana.
Wa Ufipa Mkuu
Kotekote MkuuHongera basi! Ila posho yatoka Lumumba siyo?