Watanzania wengi bado wapo katika hali ya tahayari kufuatia kufuatia maamuzi ya kamati kuu ya CHADEMA (CC) kuwafukuza wanachama wake watatu ambao walikuwa na majina makubwa ndani ya chama hicho. Ni wazi kuwa CHADEMA haikumuangalia mtu usoni, ikarusha lungu lake bila kujali linamwangukia nani.
Nikiwa kama mwanachama wa CHADEMA, kwanza naunga mkono maamuzi ya CHADEMA kwa ujumla wake kwa kuwa yanajaribu kukitofautisha na vyama vingine vinavyolinda zaidi uenzetu badala ya kusimamia sheria na taratibu za uongozaji wa chama na pia katiba ya vyama vyao. Katika hili, CHADEMA imetuaminisha kwamba hata ikishika dola, itakuwa tayari kumuwajibisha yeyote atakayethibitika kwenda kinyume na miiko ya uongozi, atakayeisaliti nchi, kuitia aibu na hata kutusababishia hasara au kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa vyenye kuisababishia umaskini nchi yetu na watu wake. Katika hili nakipongeza CHADEMA chama changu.
Pamoja na pongezi hizi, bado naona kwamba maamuzi haya yalikuwa ni ya haraka, na pengine yalitokana na mihemuko ya baadhi ya wanachama. Nasema hivi kwa sababu, katika ushiriki wa MM, M1 na M3 katika uandaaji wa waraka wa siri 2013, mmojawao ambaye ni Kitila Mkumbo alikubali makosa mara moja baada ya waraka huu kugunduliwa, alikuwa tayari kuachia ngazi kama sehemu ya uwajibikaji kwa kosa alilofanya, na hata pale alipotakiwa kwenda mbele ya kamati kujitetea, alifanya hivyo tofauti na wenzake walivyofanya ambao waliamua kutoroka na hata kukimbilia mahakamani. Ni dhahiri kwamba yeye kwa nafasi yake aliyajutia makosa yake na akaonyesha nia ya kutubu na kuendelea kukitumikia chama chake. Tayari Dr. Mkumbo ameshaaminiwa na chama kwa mambo mengi na makubwa, na kwa hakika ameshawekeza vya kutosha kwa ajili ya chama, ilitosha kumsamehe na kumpa onyo.
Nikitazama nyuma, katika utumishi wake ndani ya chama; tofauti na wenzake yeye hajawahi kuwa na kashfa yoyote wala kushiriki kwa namna yoyote kukihujumu chama. Kwa mfano ukimtazama mtu kama Mwigamba, tayari alishawahi kutofautiana na chama kiasi cha kufikia kuondolewa katika nafasi yake ya uhasibu kule makao makuu. Wakati Zitto ameshajihusisha mara kadhaa katika vitendo vyenye kutiliwa shaka ikiwemo kuendesha kikundi cha PM7 ambacho kilifanya kazi ya kuwachafua viongozi kwa nia ya kumjenga Zitto. Lakini Mkumbo hatukuwahi kumsikia kujihusisha na lolote.
Ninawaza ya kwamba kama chama hiki kilikuwa tayari kumsamehe Ben Saanane, ambaye alikuwa ndiye master planner wa mkakati mzima wa kumpindua Mbowe na Slaa kwa faida ya Zitto, hasa baada ya kukosa nafasi BAVICHA, ni kwa vipi kimeshindwa kumsamehe Kitila ambaye alishiriki kuedit tu waraka huu wa kuwaangusha akina Mbowe?
Bado ninaona kwamba Kitila ana mapenzi mema na chama hata kama kwa sasa amekata tamaa na kutamani mbadala wa CCM na CHADEMA. Nafikiri yaanzishwe mazungumzo kati ya chama na Kitila ili kuona ni namna gani anaweza kurudi chamani na ikiwezekana atimize ndoto zake za kuwa mbunge wa Singida kupitia CHADEMA na apewe onyo ili akitumikie chama kwa uaminifu kwa mjibu wa katiba ya chama.
Nina matamanio makubwa ya kuona Kitila anarudi CHADEMA. Kama NCCR mageuzi walimsamehe Kafulila, ni kwa vipi CHADEMA washindwe kumsamehe Kitila na ukizingatia kuwa ni kosa lake la kwanza? Ni lazima tutambue kwamba kama binadamu tuna mapungufu yetu, and we are prone to mistakes. Haitashangaza sana iwapo itatokea kwamba hawa hawa wanaosimama kwenye CC ya CHADEMA na kutoa hukumu kali dhidi ya watu ambao wapo tayari kutubu na kujirekebisha wakafanya madudu makubwa kushinda haya.
Sijamsemea Zitto na Mwigamba kwa kuwa tayari walishakuwa na kashfa za utovu wa nidhamu ndani ya chama kiasi cha kustahili adhabu, lakini Mkumbo hatukuwahi kumsikia katika hayo.
Nawaombeni viongozi wa CHADEMA mpunguze hasira, na kutoa nafasi ya mazungumzo na mwanazuoni huyu, na ninamwomba sana Dr. Kitila apunguze hasira, ajirudi na kukubali mazungumzo na viongozi wa CHADEMA. Waswahili husema kosa moja haliachi mke, nami nasema kosa moja la Kitila lisitufanye tukose mchango wake mhimu kwa chama.
Mungu ibariki Tanzania!
Mungu ibariki CHADEMA!
Nikiwa kama mwanachama wa CHADEMA, kwanza naunga mkono maamuzi ya CHADEMA kwa ujumla wake kwa kuwa yanajaribu kukitofautisha na vyama vingine vinavyolinda zaidi uenzetu badala ya kusimamia sheria na taratibu za uongozaji wa chama na pia katiba ya vyama vyao. Katika hili, CHADEMA imetuaminisha kwamba hata ikishika dola, itakuwa tayari kumuwajibisha yeyote atakayethibitika kwenda kinyume na miiko ya uongozi, atakayeisaliti nchi, kuitia aibu na hata kutusababishia hasara au kujiingiza kwenye vitendo vya rushwa vyenye kuisababishia umaskini nchi yetu na watu wake. Katika hili nakipongeza CHADEMA chama changu.
Pamoja na pongezi hizi, bado naona kwamba maamuzi haya yalikuwa ni ya haraka, na pengine yalitokana na mihemuko ya baadhi ya wanachama. Nasema hivi kwa sababu, katika ushiriki wa MM, M1 na M3 katika uandaaji wa waraka wa siri 2013, mmojawao ambaye ni Kitila Mkumbo alikubali makosa mara moja baada ya waraka huu kugunduliwa, alikuwa tayari kuachia ngazi kama sehemu ya uwajibikaji kwa kosa alilofanya, na hata pale alipotakiwa kwenda mbele ya kamati kujitetea, alifanya hivyo tofauti na wenzake walivyofanya ambao waliamua kutoroka na hata kukimbilia mahakamani. Ni dhahiri kwamba yeye kwa nafasi yake aliyajutia makosa yake na akaonyesha nia ya kutubu na kuendelea kukitumikia chama chake. Tayari Dr. Mkumbo ameshaaminiwa na chama kwa mambo mengi na makubwa, na kwa hakika ameshawekeza vya kutosha kwa ajili ya chama, ilitosha kumsamehe na kumpa onyo.
Nikitazama nyuma, katika utumishi wake ndani ya chama; tofauti na wenzake yeye hajawahi kuwa na kashfa yoyote wala kushiriki kwa namna yoyote kukihujumu chama. Kwa mfano ukimtazama mtu kama Mwigamba, tayari alishawahi kutofautiana na chama kiasi cha kufikia kuondolewa katika nafasi yake ya uhasibu kule makao makuu. Wakati Zitto ameshajihusisha mara kadhaa katika vitendo vyenye kutiliwa shaka ikiwemo kuendesha kikundi cha PM7 ambacho kilifanya kazi ya kuwachafua viongozi kwa nia ya kumjenga Zitto. Lakini Mkumbo hatukuwahi kumsikia kujihusisha na lolote.
Ninawaza ya kwamba kama chama hiki kilikuwa tayari kumsamehe Ben Saanane, ambaye alikuwa ndiye master planner wa mkakati mzima wa kumpindua Mbowe na Slaa kwa faida ya Zitto, hasa baada ya kukosa nafasi BAVICHA, ni kwa vipi kimeshindwa kumsamehe Kitila ambaye alishiriki kuedit tu waraka huu wa kuwaangusha akina Mbowe?
Bado ninaona kwamba Kitila ana mapenzi mema na chama hata kama kwa sasa amekata tamaa na kutamani mbadala wa CCM na CHADEMA. Nafikiri yaanzishwe mazungumzo kati ya chama na Kitila ili kuona ni namna gani anaweza kurudi chamani na ikiwezekana atimize ndoto zake za kuwa mbunge wa Singida kupitia CHADEMA na apewe onyo ili akitumikie chama kwa uaminifu kwa mjibu wa katiba ya chama.
Nina matamanio makubwa ya kuona Kitila anarudi CHADEMA. Kama NCCR mageuzi walimsamehe Kafulila, ni kwa vipi CHADEMA washindwe kumsamehe Kitila na ukizingatia kuwa ni kosa lake la kwanza? Ni lazima tutambue kwamba kama binadamu tuna mapungufu yetu, and we are prone to mistakes. Haitashangaza sana iwapo itatokea kwamba hawa hawa wanaosimama kwenye CC ya CHADEMA na kutoa hukumu kali dhidi ya watu ambao wapo tayari kutubu na kujirekebisha wakafanya madudu makubwa kushinda haya.
Sijamsemea Zitto na Mwigamba kwa kuwa tayari walishakuwa na kashfa za utovu wa nidhamu ndani ya chama kiasi cha kustahili adhabu, lakini Mkumbo hatukuwahi kumsikia katika hayo.
Nawaombeni viongozi wa CHADEMA mpunguze hasira, na kutoa nafasi ya mazungumzo na mwanazuoni huyu, na ninamwomba sana Dr. Kitila apunguze hasira, ajirudi na kukubali mazungumzo na viongozi wa CHADEMA. Waswahili husema kosa moja haliachi mke, nami nasema kosa moja la Kitila lisitufanye tukose mchango wake mhimu kwa chama.
Mungu ibariki Tanzania!
Mungu ibariki CHADEMA!
Last edited by a moderator: