Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Kila baada ya mita kama 100 kuna askari watatu au wanne, full combat wakiwa na mitutu. Wenyewe wanyarwanda wanatembea tu bila hofu, lakini mimi imenikera sana kuishi maisha ya mashaka namna hii.
Nimeuliza wenyeji wanasema kuna tetesi za mashambulizi kutoka kwa majenerali waliokimbia Rwanda, na eti kuna milipuko ya guruneti, ambayo kwa bahati nzuri haijatokea tangu nimefika hapa.
Inavyoelekea bajeti ya ulinzi ya nchi hii ni balaa tupu maana hata kama wanawalipa mishahara kidogo hawa wajeshi, ni wengi mno na pia kuna dalili ya kuzagaa wapelelezi wengi mitaani. Ukitembea unapigwa macho ya udadisi karibu na kila mtu kiasi imani inakutoka.
Haya sio maisha, tuombe Mungu yasitokee kwetu.
Nimeuliza wenyeji wanasema kuna tetesi za mashambulizi kutoka kwa majenerali waliokimbia Rwanda, na eti kuna milipuko ya guruneti, ambayo kwa bahati nzuri haijatokea tangu nimefika hapa.
Inavyoelekea bajeti ya ulinzi ya nchi hii ni balaa tupu maana hata kama wanawalipa mishahara kidogo hawa wajeshi, ni wengi mno na pia kuna dalili ya kuzagaa wapelelezi wengi mitaani. Ukitembea unapigwa macho ya udadisi karibu na kila mtu kiasi imani inakutoka.
Haya sio maisha, tuombe Mungu yasitokee kwetu.