Ninatamani sana niwe naye lakini tayari ana mpenzi wake

Swenailie

JF-Expert Member
Feb 15, 2016
240
229
Wapendwa,

Nimekuja mnishauri nini cha kufanya.

Mimi ni msichana nina umri wa miaka 26 sasa. Niko kwenye uhusiano ila pamoja na yote kuna kijana nilimuona tangu 2011 akanivutia sana nimemfatilia kila siku naona nazidi kumpenda.

Ninapojitahidi tuwe karibu anaipotezea na mimi sijafunguka sana maana naogopa atanichukuliaje pia najua wazi anauhusiano hicho ndicho kikubwa zaidi kinanifanya nisimuweke wazi ninavojiskia juu yake.

Mimi pia nina mahusiano na ninamuheshimu sana mwenzangu anaenipenda ila ukweli moyo wangu hauko kwake. Nimekaa nae miaka mitatu katika mahusiano nikiamini nitampenda ila ndo hivo tena moyo umekataa.

Japokuwa nafanya kila namna kutomkatisha tamaa ajue nampenda ila kweli moyoni hayumo. Kama unavyoona umri unaenda naogopa kumuacha huyu anaenipenda nisipate mwingine wa kuja kufanya nae maisha ila ukweli ni kwamba moyo wangu uko kwingine.

Wakati mwingine najikuta naumia kwa sababu ya hili. Kibaya zaidi huyu ninayempenda hana mda wowote na mimi najaribu kumtumia message kwenye mtandao wa kijamii ananijibu short sana hadi naumia.

Niambieni nifanyeje.
 
asante Ndugu hilo ndilo ninalojitahid ila nashindwa nakuwa napretend miaka mitatu sasa. na tunampango wa kuwa mke na mume mwakani ila kila nikitafakari najiskia kujijutia moyo unakotaka kwenda.
 
Kama una hisi yeye ni Furaha yako,,,mpe ukweli uwe na Amani Moyoni!


Kweli itakuweka huru!

Kumbuka kuna kukubaliwa na kukataliwa!
Tegemea moja wapo!

Akizingua uje kwangu haha
 
Kisambo,
hahhaahha sasa atawezaje kunielewa na anamtu mwingine. namjua hadi huyo mtu. naninaogopa kuwa chanzo cha kuharibu uhusiano wao. maana hata mm naelewa inavouma kuskia mtu anampenda mtu wake. isitoshe kutompenda sana huyu nilienae haimaanishi nikimkuta na mtu nisiumie. sasa nahisi hata kwake pia anamtu itakuaje nikimwambia hivo. ila hali inanibaki hivi hivi kuwa nampenda.
 
Ushauri huu hapa ni rahisi sana
Jitahidi usimfuatilie huyo unayempenda ikiwezekana kata mawasiliano .Hii itakusaidia kurudisha hisia kwa akupendae.Na wala usithubutu kumwambia hisia zako kwani utajishushia hadhi na unawezakuwa mtumwa wa ngono.
Sisi wanawake hatujui kupenda tunakubali mapenzi.Wanaume hawajui kupendwa wanajua kupenda na wanatakaga wapende kwanza then mwanamke ukubali mapenzi na kumheshimu akupendae.
Mfikirie huyo uliye naye utampenda tuu.Fikiria mambo mazuri aliyokufanyia na umheshimu.Jihadhari usije ukapoteza wote wawili.
 
Unapendwa bado huridhiki. Wenzio wanaitafuta hiyo chance hawaipati. Baki na jamaa jifunze kumpenda mambo yatakuwa sawa.

Miaka mitatu ni mingi hujampenda tu?
 
MPENDE ANAYEKUPENDA ASIYEKUPENDA..........................UNAMJUA kwanini asije kwako tulia wewe 26 ndo unakimbiza ivo ndoa inaelekea kukimbia mbawa umri ushaenda omba Mungu kama ni wako atakuja kama ni huyo mpende mwenzio acha tamaa za kijinga ndo mwanzo wa kuruhusu shetani katika ndoa yako
 
dada yangu funga macho yako na uhisikilize nafsi yako.............................
nadhani jibu utakua nalo tayari
 
Thanks wote. Kuwaeleza sio vibaya na ninajifunza mengi kupitia comments zenu
 
we endelea kupoteza muda wako na unaona Umri wako unavyokuacha nyuma, tena sema tu huyo jamaa yako anayekupenda wakati wewe humpendi hajasoma saikolojia, kama angekuwa mtaalam wa saikolojia angetambua kuwa humpendi na angekuacha faster.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom