Ninahitaji kufahamu kuhusu biashara ya mabondo ya Samaki

Ninahitaji kufahamu kuhusu biashara ya mabondo ya Samaki

Hii biashara imejificha sana, mnunuzi mkubwa wa mabondo ni wachina. Nimekaa ukerewe nikiichunguza hii biashara na namna inavyofanyika..
▪️Bondo lina pesa kuliko samaki mwenyewe
▪️licha ya kuuzwa kwa bei kubwa, serikali hawangaiki na hiyo biashara.
▪️Tafuta mnunuzi mkubwa, wewe kusanya mabondo kutoka kwa wakaushaji wadogo
 
Mabondo ndio manini tena???
Swim bladder au air bladder - ni kiungo katika mwili wa samaki.
1744305014464.png
 
Mkuu hii biashara japo siijui sana, ila nimetembelea viwanda vingi au vyote vya mabondo kwa Mwanza. Vyote ni vya wachina. Na soko liko huko kwao. Upatikanaji wa uhakika wa bondo ni visiwa vilivyopo lake Victoria, lakini wavuvi wengi huwa wanawauzia wachina na si waswahili kwa sababu wachina wananunua bei nzuri na pia wanawapa wavuvi mikopo mikubwa tu ili wawe na uhakika wa supply ya bondo.
Kuna processing pia ambayo inafanyika, sijajua sana wanaweka madawa gani, zinakaushwa na kusafirishwa kwenda China. Hii ni USD business, dollar kama zote.

Ukitaka kuingia ufanye vizuri tafuta mbia mchina maana soko liko kwao, hapa hamna soko.
Haya ni maelezo ya samaki aina ya sangara from lake Victoria. Sijajua kwa upande wa samaki wa baharini.
 
Mkuu hii biashara japo siijui sana, ila nimetembelea viwanda vingi au vyote vya mabondo kwa Mwanza. Vyote ni vya wachina. Na soko liko huko kwao. Upatikanaji wa uhakika wa bondo ni visiwa vilivyopo lake Victoria, lakini wavuvi wengi huwa wanawauzia wachina na si waswahili kwa sababu wachina wananunua bei nzuri na pia wanawapa wavuvi mikopo mikubwa tu ili wawe na uhakika wa supply ya bondo.
Kuna processing pia ambayo inafanyika, sijajua sana wanaweka madawa gani, zinakaushwa na kusafirishwa kwenda China. Hii ni USD business, dollar kama zote.

Ukitaka kuingia ufanye vizuri tafuta mbia mchina maana soko liko kwao, hapa hamna soko.
Haya ni maelezo ya samaki aina ya sangara from lake Victoria. Sijajua kwa upande wa samaki wa baharini.
kwahiyo nikiwa nanunua kwa wavuvi inabidi niwe napeleka kuuza kwenye viwanda vyao hao wachina na hakuna soko jingine
 
pia kuhusu usafirishaji inabidi niyakaushe kwanza ndipo naenda kuwauzia au wananunua yakiwa fresh wanakausha wao
Ukiweza kuyafikisha yakiwa fresh ni sawa wanayachukua, na yaliyokauka pia wanachukua. Wengi wanayakausha sababu ya kuogopa kuharibika especially kama kuna distance toka hapo anapoyatoa mpaka anakoenda kuuza, Au wakati wanakusanya yawe mengi kabla ya kuyapeleka kwa mchina
 
Ukiweza kuyafikisha yakiwa fresh ni sawa wanayachukua, na yaliyokauka pia wanachukua. Wengi wanayakausha sababu ya kuogopa kuharibika especially kama kuna distance toka hapo anapoyatoa mpaka anakoenda kuuza, Au wakati wanakusanya yawe mengi kabla ya kuyapeleka kwa mchina
 
anhaa sawa,kwenye kuyakausha hapo kuna utaalamu au kemikali inayotumika au ni kwa kutumia mwanga wa jua tu
 
Mimi nipo huku kwenye ukanda wa ziwa tanganyika,huku pia kuna sangara lakini kama unavojua hili ziwa lina maji chumvi ,hicho kinaweza kua kikwazo kwenye hii biashara,namaanisha samaki wa kwenye maji chumvi mabondo yao pia yananunulika ?
 
Mimi nipo huku kwenye ukanda wa ziwa tanganyika,huku pia kuna sangara lakini kama unavojua hili ziwa lina maji chumvi ,hicho kinaweza kua kikwazo kwenye hii biashara,namaanisha samaki wa kwenye maji chumvi mabondo yao pia yananunulika ?
Sina uhakika sana na mabondo ya huko kiongozi, nina idea kidogo na mabondo kwa lake Victoria, ngoja waje wenye ujuzi na ziwa Tanganyika, hawawezi kukosekana humu
 
Mimi nipo huku kwenye ukanda wa ziwa tanganyika,huku pia kuna sangara lakini kama unavojua hili ziwa lina maji chumvi ,hicho kinaweza kua kikwazo kwenye hii biashara,namaanisha samaki wa kwenye maji chumvi mabondo yao pia yananunulika ?
Kumbe Lake Tanganyika lina maji ya chumvi, ndio nafahamu leo.
 
Back
Top Bottom