Father Mkananayo
Member
- Sep 6, 2024
- 47
- 89
Kamwene, Ughonile, Mwandila!
Nikiwa kama kijana niliyezaliwa katika familia kubwa ya Watoto 12.
Malezi ya halisi ya kiafrika kutoka jamii ya kabila x nilifundishwwa vyema sana mzee wangu.
Kwanza mzee wangu alihakikisha katika Watoto wake wote wanapata elimu walau ya sekondari kipindi hicho ikiwa ni elimu haswa.
Mzee wangu alihakikisha pamoja na kwamba tunasoma lakini alihimiza sana jembe (kilimo) na hapa alikuwa active mno.
Mtoto yeyote yule aliyonekana mzembe hakusita kumpa kipigo kitakatifu.
Tuliamka saa10 alfajiri kulima kwanza then ndo tuende shule na shule lazima kuwahi namba asubuhi.
Mzee wetu hakuacha kamwe kulima bustani za mboga mboga kwenye bonde letu karibu na nyumbani.
Hivyo kila tukitoka shule jioni saa11 lazima umalizapo kula n kwenda kumwagilia bustani.
Mzee wetu pamoja na kuwa na kazi ya ualimu tu lkn Watoto na familia Kwa ujumla tulikuwa na furaha sana.
Mzee baba yetu licha ya kuwa na watoto 12 wa ndoa pia tuliishi na watoto wa shangazi wachungaji na mara chache vibarua.
Familia yetu ilikuwa na watu wengi idadi mara nyingi ilikuwa haipungui watu27-30.
Mzee alitusisitiza kuishi vizuri na watu wote,kusaidia bila kutalajia kupata faida.
Ikumbukwe kuwa mzee wetu pia alikuwa anamsomesha na watu Baki tu yaani sio ndugu Wala rafiki
Baba Kila alipokuwa anaenda kupokea mshahara alihakikisha harudi mkono mtupu.
Kwanza Ali hakikisha anakuja na matunda kama nanasi,ndizi,na palachichi kipindi hicho sisi huku hatuyajui na vile hayakuwa matamu yalituchukua muda sana kuanza kuyatumia kwani tuliona kama tunakula matope tu hayana ladha Wala utamu wowote.mara chache pia alikuja na mikate. Vilevile hakusahau kuja na mboga kama samaki mkubwa ama nyama.
Maisha yalikuwa sio mazuri sana ni kawaida kulingana na kipato Cha mzee kwani kipindi hicho nadhani alikuwa anapokea 300k ama chini ya hapo.
Mambo makuu 3 niliyoyashudia Kwa mzee wangu.
1:-kusaidia bila kuchoka hata watu wa Nje.
Nakumbuka sisi kipindi tunakua kwenye miaka ya2000 alikuwepo jamaa mmoja hapo kwetu alikuwa anasoma sekondari na alikuwa anasomeshwa na mzee wetu.
Nimekua nikijua ni mtoto halisi wa mzee kumbe alikuja tu kuomba kukaa kwetu na kusoma maana mzee wake alikuwa hataki kabisa asome Bali aoe licha ya kuwa na akili darasani.
Jamaa yule alisomeshwa na mzee wetu Hadi chuo cha ualimu akamaliza na kuajiliwa.
Yule jamaa akiendelea kupiga kitabu Hadi Sasa ni mfanyakazi kitengo Cha juu TRA.
Huyu jamaa ana mkumbuka mzee Kwa mengi sana Kila akipata nafasi hufika nyumbani na zawadi ambazo hata sisi Watoto hatujawahi mpa mzee wetu.
Wengine waliosomeshwa na mzee na kujipata ni afisa kilimo wilayan x mmoja ni nesi na mwingine ni mwalimu Hadi Leo.
Na misadaa mbalimbali Kwa wahitaji.
2:-Kutufundisha kazi Nje na Elimu.
Japo kipindi hicho ukionekana wewe ni mtoto wa mwalimu basi kulikuwa na upekee wake hasa kijijn. Lakini Kwa mzee wangu ilikuwa ni tofauti. Kama nilivyotangulia kuelezea hapo mwanzo tuliamka mapema kulima na jioni kumwagilia.
Hii imenisaidia sana Mimi Hadi hapa nilipo.
3:-Kamwe hakuwahi kumuonyesha mama yetu kiasi Cha Hela anacho pokea😂😂🙌🙌
Tangu najitambua sikuwahi kuona mzee anampiga mama tofauti na kufoka pale inapobidi kama mzee wa kaya!!
Mzee alionyesha kumpenda mama Tena hadharani Hadi Watoto tulijua kabisa mzee ana muelwa sana mother.
Cha ajabu mama pamoja na kulalamika kuwa hajui mmewe kiasi anachopokea Wala hajawahi kuambiwa nk
Mzee Wala hakulitilia maanani jambo Hilo na mama Hadi kufikia kuuliza ni baadhi ya Watoto (wakubwa zetu) walitaka wajue.
Nimejifunza mzee alikuwa sawa sana Kwa hili kwani Hadi Sasa nimepokea Malala mishi mengi sana Kwa wanaume walio waambia wake zao basic salary zao wanajutia mnoo.
(Wachache wataelewa hapa )
LEO HII NAMI NIMEKUWA MTU MZIMA NA NINA FAMILIA.
Nimeanza kuona mzee alikuwa mwamba sana kulisha na kuhudumia familia kubwa kama Ile ambapo Mimi familia ya watu wasio fika hata robo inatoa jsho na Nina kipato zaidi ya mzee!!
Hakika mzee huyu alikuwa mtu na nusu. Kuna muda ukimaliza withdraw Hela inaishia kwenye majukumu tu na unashindwa kununua hata ndizi za buku.
Ninayo mengi mno Wacha tu niishie hapa.
Nikiwa kama kijana niliyezaliwa katika familia kubwa ya Watoto 12.
Malezi ya halisi ya kiafrika kutoka jamii ya kabila x nilifundishwwa vyema sana mzee wangu.
Kwanza mzee wangu alihakikisha katika Watoto wake wote wanapata elimu walau ya sekondari kipindi hicho ikiwa ni elimu haswa.
Mzee wangu alihakikisha pamoja na kwamba tunasoma lakini alihimiza sana jembe (kilimo) na hapa alikuwa active mno.
Mtoto yeyote yule aliyonekana mzembe hakusita kumpa kipigo kitakatifu.
Tuliamka saa10 alfajiri kulima kwanza then ndo tuende shule na shule lazima kuwahi namba asubuhi.
Mzee wetu hakuacha kamwe kulima bustani za mboga mboga kwenye bonde letu karibu na nyumbani.
Hivyo kila tukitoka shule jioni saa11 lazima umalizapo kula n kwenda kumwagilia bustani.
Mzee wetu pamoja na kuwa na kazi ya ualimu tu lkn Watoto na familia Kwa ujumla tulikuwa na furaha sana.
Mzee baba yetu licha ya kuwa na watoto 12 wa ndoa pia tuliishi na watoto wa shangazi wachungaji na mara chache vibarua.
Familia yetu ilikuwa na watu wengi idadi mara nyingi ilikuwa haipungui watu27-30.
Mzee alitusisitiza kuishi vizuri na watu wote,kusaidia bila kutalajia kupata faida.
Ikumbukwe kuwa mzee wetu pia alikuwa anamsomesha na watu Baki tu yaani sio ndugu Wala rafiki
Baba Kila alipokuwa anaenda kupokea mshahara alihakikisha harudi mkono mtupu.
Kwanza Ali hakikisha anakuja na matunda kama nanasi,ndizi,na palachichi kipindi hicho sisi huku hatuyajui na vile hayakuwa matamu yalituchukua muda sana kuanza kuyatumia kwani tuliona kama tunakula matope tu hayana ladha Wala utamu wowote.mara chache pia alikuja na mikate. Vilevile hakusahau kuja na mboga kama samaki mkubwa ama nyama.
Maisha yalikuwa sio mazuri sana ni kawaida kulingana na kipato Cha mzee kwani kipindi hicho nadhani alikuwa anapokea 300k ama chini ya hapo.
Mambo makuu 3 niliyoyashudia Kwa mzee wangu.
1:-kusaidia bila kuchoka hata watu wa Nje.
Nakumbuka sisi kipindi tunakua kwenye miaka ya2000 alikuwepo jamaa mmoja hapo kwetu alikuwa anasoma sekondari na alikuwa anasomeshwa na mzee wetu.
Nimekua nikijua ni mtoto halisi wa mzee kumbe alikuja tu kuomba kukaa kwetu na kusoma maana mzee wake alikuwa hataki kabisa asome Bali aoe licha ya kuwa na akili darasani.
Jamaa yule alisomeshwa na mzee wetu Hadi chuo cha ualimu akamaliza na kuajiliwa.
Yule jamaa akiendelea kupiga kitabu Hadi Sasa ni mfanyakazi kitengo Cha juu TRA.
Huyu jamaa ana mkumbuka mzee Kwa mengi sana Kila akipata nafasi hufika nyumbani na zawadi ambazo hata sisi Watoto hatujawahi mpa mzee wetu.
Wengine waliosomeshwa na mzee na kujipata ni afisa kilimo wilayan x mmoja ni nesi na mwingine ni mwalimu Hadi Leo.
Na misadaa mbalimbali Kwa wahitaji.
2:-Kutufundisha kazi Nje na Elimu.
Japo kipindi hicho ukionekana wewe ni mtoto wa mwalimu basi kulikuwa na upekee wake hasa kijijn. Lakini Kwa mzee wangu ilikuwa ni tofauti. Kama nilivyotangulia kuelezea hapo mwanzo tuliamka mapema kulima na jioni kumwagilia.
Hii imenisaidia sana Mimi Hadi hapa nilipo.
3:-Kamwe hakuwahi kumuonyesha mama yetu kiasi Cha Hela anacho pokea😂😂🙌🙌
Tangu najitambua sikuwahi kuona mzee anampiga mama tofauti na kufoka pale inapobidi kama mzee wa kaya!!
Mzee alionyesha kumpenda mama Tena hadharani Hadi Watoto tulijua kabisa mzee ana muelwa sana mother.
Cha ajabu mama pamoja na kulalamika kuwa hajui mmewe kiasi anachopokea Wala hajawahi kuambiwa nk
Mzee Wala hakulitilia maanani jambo Hilo na mama Hadi kufikia kuuliza ni baadhi ya Watoto (wakubwa zetu) walitaka wajue.
Nimejifunza mzee alikuwa sawa sana Kwa hili kwani Hadi Sasa nimepokea Malala mishi mengi sana Kwa wanaume walio waambia wake zao basic salary zao wanajutia mnoo.
(Wachache wataelewa hapa )
LEO HII NAMI NIMEKUWA MTU MZIMA NA NINA FAMILIA.
Nimeanza kuona mzee alikuwa mwamba sana kulisha na kuhudumia familia kubwa kama Ile ambapo Mimi familia ya watu wasio fika hata robo inatoa jsho na Nina kipato zaidi ya mzee!!
Hakika mzee huyu alikuwa mtu na nusu. Kuna muda ukimaliza withdraw Hela inaishia kwenye majukumu tu na unashindwa kununua hata ndizi za buku.
Ninayo mengi mno Wacha tu niishie hapa.