Hata sijui sababu ni nini, maana kama ni kula nakula vizuri tu na mke wangu anajitahidi kunipikia mapochopocho mpaka basi lakini mwili wangu hauridhiki sijui kwanini, yaani nimekuwa na maumbile madogo wala sinenepi kabisaa mpaka ndugu zangu wanahisi kwamba huenda mke wangu hanipi chakula na ndio maana sinenepi kumbe binti wa watu anajitahidi kukalangiza lakini mwili wangu huu hauna shukurani.
Hebu nisaidieani, sababu hasa ya kukosa kwangu siha ni nini?
platozoom namaanisha maumbile yangu ya mwili ni madogo, sinenepi wala nini, wakati nakula vizuri tu
tatizo mke wangu analaumiwa sana na ndugu zangu, eti hanipi chakula na yeye hana amani kabisa
Julius amekaa Ikulu for 23 yrs hajawahi ever kuwa mnene, ama Kitambi !
Unadhani Maria hakua akimpa chakula ? Au alikua hajui makaangizo? Na akiwa (head of state) ungetegemea mwili wake uweje? Thn check aliyemfatia aliingia na body ya kawaida, lakini alimaliza muda wake akiwa kama Tembo.
acha uroho ni mbaya sana ndo maana unenepi na makulalamika..
Sasa wanamlaumu mkeo kwani kabla hujaoa ulikua mnene??ndugu wengine hovyo kweli!