Mkuu naomba unitoe matongotongo kwenye kipengele cha pili,ikiwa uingizaji wa bidhaa nyingi nchini husababisha kushuka kwa thamani ya pesa yetu,Sasa kwanini Kanchi km Burundi wanaotutegemea kwa kila kitu Pesa yao ipo juu kuliko yetu?,halikadhalika Rwanda huko ndo usiseme.Fafanua mkuu!.
Sijaufatilia uchumi wa Burundi na Rwanda lakini hizi zinaweza kuwa sababu..
'Balance of payment' ni tofauti ya malipo kati ya vitu tunavyoagiza na tunavyouza, yawezekana Burundi inatutegemea baadhi ya vitu lakini vitu husika vikawa gharama yake ndogo sana na wenyewe wakawa wanajizalishia vitu muhimu vyote, inawezekana nchi husika wana mfumo mzuri wa kubana matumizi yake, mfano labda Burundi wameshajenga mtandao wao wa miundombinu kama barabara au hawana lakini hawajengi lakini Tanzania inatumia pesa nyingi kusambaza mtandao wa barabara hivyo japo hujaona bidhaa iliyoingia lakini ujenzi husika ni zaidi ya kuingiza tani na tani za bidhaa. Unaweza kua unaishi mjini hivyo ukaona ni pato kubwa linalozalishwa lakini ujue pato hilo tunagawana na sehemu kubwa sana ya Tanzania ambayo uzalishaji wake ni hafifu sana au ni karibu na hakuna tofauti na nchi kama Burundi.