Poleni na majukumu wana MMU, naomba niende kwenye Mada moja, kwa Moja Nina mahusiano na mwanaume mmoja, Mimi ni mfanyakazi Na mwenzangu ni mfanyakazi pia,mishahara yetu haitofautiani Sana japo yeye ananizidi kidogo, Cha kushangaza toka nimekuwa nae kwenye mahusiano haishi kulalamika hana hela(sina tabia ya kumuomba hela)amekuwa na tabia ya kunililia shida kila siku,kosa akiona hela nyingi kwenye pochi lazima aombe, niliwahi kuzungumza nae kuhusu tabia yake na future yetu akadai ana majukumu huko kwao ndo maana hela yake haikai. Ana mpango wa kwenda kutoa posa mwaka kesho,naombeni ushauri wenu jamani niko njia panda, huyu mtu akinioa ataihudumia familiar ipasavyo kweli? Tatizo lake jingine sio mpambanaji kabisa, hata ukimuomba ushauri wa jambo la kujenga majibu yake ni zero,naombeni ushauri wenu jamani huyu mwanaume kweli atanifaa iwapo tutaingia nae kwenye ndoa?
