Naxria abdalla
Senior Member
- Feb 28, 2025
- 178
- 311
Jaman habari zenu mimi nina changamoto ya presha na nimegundua kutokana na number zangu zinavyojieleza mara inapanda mara inashuka naitaji kuicontroll kabla haijaniletea shida kubwa zaidi iwe kwa dawa au kawaida,naomba kwa upole tu munibariki njia za kuicontroll,plz hii ni serious sana,apo chini daktar amenipa dawa je hizi dawa ndio zile ambazo natakiwa kutumia maisha yangu yote?
Maoni ya Mdau
Maoni ya Mdau
Kama ni presha inayotokana na mazingira ya muda mfupi kama vile msongo wa mawazo (stress) e.g. kazi nyingi mno, matatizo ya kifamilia, chakula, au ugonjwa, etc, presha hii ni ya muda tu na itarudi chini na utaendelea kama kawaida hata bila kutumia dawa.
Lakini kuna tatizo la presha ya kudumu, inayotokana hasa na umri mkubwa na figo kushindwa kufanya kazi vizuri, au matatizo mengine ya kibiologia, presha hii haitibiki na kuisha kwa kutumia dawa ulizopewa. Utatakiwa kutumia dawa hizo maisha yako yote. Usiogope kwani wengi hufanya hivyo. Zingatia matumizi ya dawa na epuka mambo yanayoweza kusababisha presha kupanda kama vile kula vyakula vyenye chumvi nyingi, mafuta mengi, epuka hasira, msongo wa mawazo, etc.