Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Binafsi namuona Dr. Slaa kama mtu maarufu zaidi kwenye Kampeni za uchaguzi wa Mwaka huu. Lakini kwa upande wa Pili namuona kama Daudi kwenye simulizi za Biblia aliyemshinda Goliathi, Daudi alikuwa na Kombeo na Jiwe hata akamshinda Goliathi.
Dr. Slaa tayari analo Kombeo (umaarufu wake binafsi) lakini sijui kama jiwe (Chama) atakalotumia kuumuulia Goliathi (CCM) ni imara kiasi cha kuweza kumuua shujaa huyo aliyepigana vita vingi na kushinda.
Isije ikawa jiwe analotaka kulitumia 31/10/2010 ni udongo ulifinyangwa na kuanikwa juani likikutana na matone (kashikashi za uchaguzi) kidogo ya mvua linamong'onyoka.
Dr. Slaa tayari analo Kombeo (umaarufu wake binafsi) lakini sijui kama jiwe (Chama) atakalotumia kuumuulia Goliathi (CCM) ni imara kiasi cha kuweza kumuua shujaa huyo aliyepigana vita vingi na kushinda.
Isije ikawa jiwe analotaka kulitumia 31/10/2010 ni udongo ulifinyangwa na kuanikwa juani likikutana na matone (kashikashi za uchaguzi) kidogo ya mvua linamong'onyoka.