Nimsaidie mama angu au mpenzi Wangu ?

Nimsaidie mama angu au mpenzi Wangu ?

Digital Marketer

Senior Member
Joined
May 1, 2019
Posts
112
Reaction score
149
Wakuu naombeni ushauri.

Nina simu mbili, zote za ni Smart.

Mama na mpenz wangu wana simu za button.

Wote waniomba hiyo simu kwa wakati mmoja.

Nampenda sana mpenz wangu kiukweli ni kama rafiki yangu.

Na amekua wa msaada mkubwa kwenye badiliko la maisha yangu.

Kwa upende wa pili mama ni mama tu.

Nipo njia panda nifanyeje?
 
Kosa lako ulivyomuita kuwa ni mpenzi na si mke,mpe mama hiyo simu...hasa kama amekuomba..huyo mpenzi ambae hata hamuijui kesho yenu mpotezee..sana sana ataitumia kutumiana picha za utupu na ampendae uje utushirikishe msiba wa kusalitiwa hapa!
 
Wakuu naombeni ushauri....
Nina simu mbili, zote za ni Smart.....

Mama na mpenz wangu wana simu za button......

Wote waniomba hiyo simu kwa wakati mmoja.....

Nampenda sana mpenz wangu kiukweli ni kama rafiki yangu.....

Na amekua wa msaada mkubwa kwenye badiliko la maisha yangu......

Kwa upende wa pili mama ni mama tu.....

Nipo njia panda nifanyeje ??

Mama ndiye wa muhimu na ni wajibu wako kumpa hiyo simu hata kama hakukuomba ili mradi anahitaji. Kumlinganisha mpenzi na mama yako ni kukosa adabu kwa mzazi.

Mpenzi anaweza kukutema wakati wowote, lakini mama ni mama tu.
 
Hili nalo la kuombea ushauri? Ndio maana wamama wengine wanatupa watoto walah
Yaani kama ulikuwa mawazoni mwangu mkuu...
Hivi unaanzaje kuomba ushauri kwa jambo la wazi kama hilo.
Yaani ni sawa na kuuliza ni nani bora baina ya hao wawili!!.
 
Wanawake huu uzi watapita kimya kimya atajitokeza mmoja tu mwenye haiba za kiume...

Ndugu mleta uzi hakuna wa kufanana na mama yako !!!
Mama alikutafuta akakutafutia
Mke/mpenzi wako mmetafutana na mtatafuta wote

Nashangaa ni kwanini mpaka sasa hujampa mama yako mzazi hiyo simu umerogwa wewe
 
Angekuwa mkeo ningeshauri umpe lakini simu mpe mama,sababu bado hujaoa
 
Kwa haraka harka chance ya kuishi miaka mingi ni ya mpenzi wako mpe mzazi wako aenjoy wakati uliobakia, uyo mpenzi wako utamnunulia siku ingine tena wakati unamkabidhi unamkaza alafu unaweka na vidukuzii
 
Gawa simu zote kwa hao watu na wewe ununue nyingine
 
Mweleze mpenzi wako kuwa Mama aliomba Simu kabla yake hivyo awe mvumilivu.

Ila mwambie utatafutia nyingine na hapo ndio itakuwa kipimo sahihi cha kwanza Kama anafaa kuja kuwa Mke.

Na ili uoyeshe matunda ya umilivu wake kweli umnunulie ili uwe Mwanaume maana sifa ya Mwamaume ni kutekeleza majukumu yanayo kuzunguka ndio sifa kuu.
 
Jisaidie wewe mwenyewe kwanza, mana haupo sawa, Na usikute hata kwa huyo mpenzi wako huko peke yako! kama huamini hilo dukua hiyo simu then mpe huyo mpenzi wako, ukidukua utaona kila kitu kinachoendelea, kama kesho yake hujamnyang'anya huyo mpenz wako hiyo simu!
Kitu kingine hebu mjaribu mwambie huyo mpenzi wako kua mama ameihitaji hiyo simu, kama ataonyesha ubinafsi na kuitaka yeye basi ujue hafai huko mbeleni kua mke.
 
Back
Top Bottom