Nimlaumu nani, baba au mama?

Nimlaumu nani, baba au mama?

SAYARI DUNIA

Member
Joined
Jul 19, 2015
Posts
54
Reaction score
17
Nimekaa na baba yangu kwa miaka 19, lakini kumbe ni baba mlezi, hiyo imekuja baada ya baba ya halisi kujitokeza nikiwa form 'vi' nakunileza kila kitu kunihusu, ila tatizo mama hajaniambia chochote mpaka sasa.

USHAURI KWA WADAU JAMANI SIJUI NIBAKI KWA BABA MLEZI AU NIENDE KWA BABA HALISI.
 
Unauhakika gani anayokueleza huyo unaesema ni baba yako mzazi ni kweli?na hana lengo la kukuvuruga?alikuwa wapi siku zote mpka asubiri uwe mtu mzima ndio aje?Umepata shida gani kwa baba yako wa sasa?acha kudanganyika dogo,kazana na masomo,achana na hayo mambo,sio size yako.
 
Hakuna wa Kubla ya kabla ya kujua mazingira yaliyopelekea hali hiyo
 
Baba wa mtoto ajuaye mama pekee kama mama ako alikuambia huyo unaeishi naye ndo baba ako...we unamwamini vp huyo mwingine?
 
alikuwa wapi siku zote aje atokee leo ukiwa tayar unaanza kutengeneza future yako?? vip mama anajua hilo?? mama zetu ndo hutambua baba halisi wa mtoto ukiona inakua ngumu kueleweka mshirikishe mama anaweza akawa na majibu juu ya jibu lako. usikimbilie kumhukum mtu tambua anything happens for a reason there must be a reason behind why mama hakukuambia siku zote hizo na utakapo ujua ukweli usimlaum mtu wote ni wazazi wako na kipi kimekufanya ukaamini faster faster kwamba huyo ndio baba yako mzazi?? mjini shule ndugu akili za kuambiwa + na zako jibu utapata.
 
Anayejua furaha yako na huzuni zako , ukiumwa yu pembeni yako , anajua madhaifu yako na kukukanya kwa upendo ufuate njia zilizo sahihi , amekupa upendo wa mzazi halisi pasipo wewe kujua tofauti yoyote ndiye baba yako ,Huyo tapeli aliyekuja sasa na kujionesha kuwa ndiye baba yako alikuwa wapi siku zote .Hivi moyo wako unafungukaje na kuanza kumpenda mtu kama huyo kweli twatofautiana miaka 19?
 
Binafsi upendo ungeongezeka kwa baba mlezi maana ni wa peke hajaonesha ubaguzi au kinyongo cha kulea mtoto asiye wake unless alikuwa hajui kama mtoto si wa kwake .Lakini bado bond mliyonayo ni strong kwakweli
 
Baki mwenyewe na roho yako Son. Wote wawili wanaweza kuwepo kwenye maisha yako harmoniously. The only one who can disturb that is you
 
Huyo anayekuja kujitokeza leo umekuwa mtu mzima anakutakia nini ! Hata kama walikuficha je huyu baba mlezi aliwahi kukunyanyasa ...mpaka usijione kuwa na hadhi ya mwanae! kama sivyo mwambie ahasante baba kujitokeza ....mpende baba yako aliyekulea ! Kumbuka hta punda ana watoto ...je mahusinao yao yakoje !/
Nimekaa na baba yangu kwa miaka 19, lakini kumbe ni baba mlezi, hiyo imekuja baada ya baba ya halisi kujitokeza nikiwa form 'vi' nakunileza kila kitu kunihusu, ila tatizo mama hajaniambia chochote mpaka sasa.

USHAURI KWA WADAU JAMANI SIJUI NIBAKI KWA BABA MLEZI AU NIENDE KWA BABA HALISI.
 
Uchungu wa mwana haujuae ni mlezi. Hata na kichaa anaweza weka mbegu
 
Nimekaa na baba yangu kwa miaka 19, lakini kumbe ni baba mlezi, hiyo imekuja baada ya baba ya halisi kujitokeza nikiwa form 'vi' nakunileza kila kitu kunihusu, ila tatizo mama hajaniambia chochote mpaka sasa.

USHAURI KWA WADAU JAMANI SIJUI NIBAKI KWA BABA MLEZI AU NIENDE KWA BABA HALISI.

Wewe una uhakika gani kama huyo aliyejitokeza ndio baba yako halisi? Umefanya vipimo vya DNA? Kama mama yako hajakwambia chochote kuhusu baba yako basi ujue ana sababu za kwa nini yeye ameamua kufanya hivyo. Je umejiuliza kwa nini mama yakohajakwambia kuhusu baba yako hadi hivi sasa? Je kwa nini usimuulize mama yako kuhusu baba yako ili upate maelezo na ukweli kutoka kwake? Na kwa nini uwatenge baba yako na mama yaako waliokulea hadi hivi sasa unajiona umekua na unaona baba yako aambaye hakushiriki katika malezi yako ni bora kuliko hao wazazi wako waliokulea? Naamini ukiyatafakari maswali haya kwa makini, yatakusaidia kukupa mwelekeo wa nini cha kufanya. Nakutakia kila la heri katika maamuzi yako.
 
huyo baba mlezi ana alama gan usoni kusema huyu sio baba mzazi?
 
Samahani...naomba nikuambie in a very polite way...

"Una akili kweli wewe?

Miaka yote 19 alikuwa wapi?????

Hivyo vichwa vina matumizi gani? Kufugia nywele???
 
tulia baba yako ni huyo aliyekulea basi.. huyo anayejifanya mzazi sa hizi alikuwa wapi siku zote?
 
Nimekaa na baba yangu kwa miaka 19, lakini kumbe ni baba mlezi, hiyo imekuja baada ya baba ya halisi kujitokeza nikiwa form 'vi' nakunileza kila kitu kunihusu, ila tatizo mama hajaniambia chochote mpaka sasa.

USHAURI KWA WADAU JAMANI SIJUI NIBAKI KWA BABA MLEZI AU NIENDE KWA BABA HALISI.

Baba yako ni baba yako tu atabaki kuwa hata kama hajakulea
 
alikuwa wapi siku zote aje atokee leo ukiwa tayar unaanza kutengeneza future yako?? vip mama anajua hilo?? mama zetu ndo hutambua baba halisi wa mtoto ukiona inakua ngumu kueleweka mshirikishe mama anaweza akawa na majibu juu ya jibu lako. usikimbilie kumhukum mtu tambua anything happens for a reason there must be a reason behind why mama hakukuambia siku zote hizo na utakapo ujua ukweli usimlaum mtu wote ni wazazi wako na kipi kimekufanya ukaamini faster faster kwamba huyo ndio baba yako mzazi?? mjini shule ndugu akili za kuambiwa + na zako jibu utapata.

Bibi aliwahi kuniambia kuhusu baba yangu halisi ila nilipuuzia ndiyo maana ss ninaamini huenda ikawa.
 
Back
Top Bottom