Nimjuavyo Kamanda Patrobass Paschal Katambi tangu mwaka 2010!

Nimjuavyo Kamanda Patrobass Paschal Katambi tangu mwaka 2010!

Makala Jr

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2011
Posts
3,395
Reaction score
1,112
Nawasalimu wanajukwaa wote! Kama alivyowahi kunena George Herbert kwamba, "The best mirror is an old friend". Kutokana na harakati za uchaguzi BAVICHA kushika kasi, nimeona ni vema mkamtambua mmoja kati ya Kamanda anayetajwa kugombea Uenyekiti BAVICHA-Taifa ndugu Patrobass Paschal Katambi. Tulifahamiana tangu mwaka 2010 katika harakati za uchaguzi mkuu jijini Mwanza tukiwa tunahamasisha wapiga kura kuwachagua viongozi kutoka udiwani,ubunge na urais kwa tiketi ya CHADEMA. Mwaka 2011 nilifanya naye kazi ya chama CHADEMA-SAUT akiwa Mwenyekiti, Nicholaus Kirunga akiwa Makamu Mwenyekiti nami nikiwa Naibu Katibu.Mhe.Patrobass ni kiongozi mzuri mwenye kuwasikiliza watu wanapomshauri.Ni katika uongozi wetu tuliivunja ngome ya CCM SAUT na kumweka Kamanda Godlisten Malisa kuwa Rais nami nikiwa Naibu Waziri katika wizara ya mikopo.Tulifanya kazi nzuri na kujenga jina lililowavutia hadi viongozi wa kitaifa.Tulikijenga chama kwa jina na hadhi ya kuwaogopesha CCM, mwenye swali/dukuduku aniulize nitamjibu!
 
Hakika kamanda,hakuna uliloongeza.Nimemfahamu Patrobas 2008,akiwa mweka hazina wa CDM SAUT.2009/2010 hakuwa kiongozi ila binafsi nilifaidi mawazo,miongozo naushauri wake nikiwa kiongozi naye akiwa mwanachama wakawaida.Nimtu wa subira,na tahadhari.
 
Kimsingi wanaotaka kumbeza kamanda PP wajue wanatusaliti vijana wote wa na wana CDM kwa ujumla,jamaa yupo vizuri sana,ni miongoni mwa wanasiasa wachache vijana wanaojua siasa za aina zote,mnyenyekevu na anaefanya kazi kwa kzingatia kanuni,taratibu na katiba,binafsi nimefanya nae kazi kama makamu Mwenyekiti wa CHASO SAUT,CDM pale SAUT ilikuwa katika ubora wake zaidi
 
Nawasalimu wanajukwaa wote! Kama alivyowahi kunena George Herbert kwamba, "The best mirror is an old friend". Kutokana na harakati za uchaguzi BAVICHA kushika kasi, nimeona ni vema mkamtambua mmoja kati ya Kamanda anayetajwa kugombea Uenyekiti BAVICHA-Taifa ndugu Patrobass Paschal Katambi. Tulifahamiana tangu mwaka 2010 katika harakati za uchaguzi mkuu jijini Mwanza tukiwa tunahamasisha wapiga kura kuwachagua viongozi kutoka udiwani,ubunge na urais kwa tiketi ya CHADEMA. Mwaka 2011 nilifanya naye kazi ya chama CHADEMA-SAUT akiwa Mwenyekiti, Nicholaus Kirunga akiwa Makamu Mwenyekiti nami nikiwa Naibu Katibu.Mhe.Patrobass ni kiongozi mzuri mwenye kuwasikiliza watu wanapomshauri.Ni katika uongozi wetu tuliivunja ngome ya CCM SAUT na kumweka Kamanda Godlisten Malisa kuwa Rais nami nikiwa Naibu Waziri katika wizara ya mikopo.Tulifanya kazi nzuri na kujenga jina lililowavutia hadi viongozi wa kitaifa.Tulikijenga chama kwa jina na hadhi ya kuwaogopesha CCM, mwenye swali/dukuduku aniulize nitamjibu!

Ni kweli mimi nafanya naye kazi, huyu patrobass ni kipenzi cha wafanyakazi, kwanza ni mtu wa watu, ni msikivu sana na anapenda sana kutenda haki na mambo yake anayafanya kwa tahadhari sana na kwa umakini mkubwa. Huyu jamaa atawasaidia sana CHADEMA,

Aliwahi kufuatwa na watu wa chama kileee ili ajiunge nao, jamaa aligoma na alikataa kata kata.

kwa ufupi, huyu jamaa anatenda kile anachokiamini.

Pia huyu jamaa hapa kazini hana kundi kwamba hili ni la watu wake au la! wote ni wake.

baada ya kuteuliwa kushika nafasi aliyonayo sasa, malalamiko ya wafanyakaxi yameisha kabisa. kama huamini mtafute mtu yyte unayemfahamu pale sahara umuulize.
 
Nilimjua Patrobas 2011 kipindi kile cha uchaguzi kusema kweli yeye Malisa Godlisten na Odelo ndio walio nishawishi nikaenda kuchukua card ya chadema tawi la saut.Huyu jamaa Yuko vizuri ni hazina hii tuitumie wadau.
 
Last edited by a moderator:
Haya MAKALA Jr ila huwezi kujua content ya kitabu kwa kuangalia cover page tu.
Ila kwa kuwa ulishiba kupitia bakuli la Patrobas na Malisa wewe ukiwa kama waziri mdogo wa mikopo pale CHUONI na mwanaharakati usiyeeleweka eleweka mle darasani kwetu BAPRM na vile vijiwe vyetu vya kisiasa nje ya mwanjonde na pale magazetini basi unaconclude kuwa huyu bwana ni msafi na mzalendo wa ukweli wa kuitetea na kuibeba chadema.
Ila kwa upande mwingine wa mawazo yangu ni kwamba HAFAI KABISA.
Niulize Kwa nini..........!!
 
Last edited by a moderator:
Haya MAKALA Jr ila huwezi kujua content ya kitabu kwa kuangalia cover page tu.
Ila kwa kuwa ulishiba kupitia bakuli la Patrobas na Malisa wewe ukiwa kama waziri mdogo wa mikopo pale CHUONI na mwanaharakati usiyeeleweka eleweka mle darasani kwetu BAPRM na vile vijiwe vyetu vya kisiasa nje ya mwanjonde na pale magazetini basi unaconclude kuwa huyu bwana ni msafi na mzalendo wa ukweli wa kuitetea na kuibeba chadema.
Ila kwa upande mwingine wa mawazo yangu ni kwamba HAFAI KABISA.
Niulize Kwa nini..........!!



mkuu kwa nini hafai? tufafanulie ili tumjue vizuri sote ni wadau!
 
Last edited by a moderator:
Chitemo: Mimi naamini binadamu asiyefaa hapa duniani hayupo ila binadamu mwenye dharau na majivuno ya kuwaona wengine hawafai yupo. Hivyo sina haja ya kumuuliza kwanini mtu fulani unasema hafai hali najua una dharau. Umesema niliELEWEKA ELEWEKA hapa sijui ulilenga nini? Nilitimiza wajibu wangu kwa kujituma na sikufisadi mali wala mawazo ya mtu tangu nilipokuwa Naibu Katibu wa CHASO-SAUT, Naibu Waziri wa Mikopo na hata nilipochaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi SAUTSO nilifanya kazi kwa uaminifu mkubwa.Na Kamanda Patrobass alikuwa ni sehemu ya matunda ya utendaji wangu wa kazi.Kila binadamu ana mapungufu yake ya kawaida kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu.Mimi kwa ukaribu na mahusiano makubwa niliyokuwa nayo na Patrobass Paschal ana uwezo mkubwa wa kuongoza na kupeleka mbele gurudumu la demokrasia ndani ya CHADEMA na taifa kwa ujumla.Lakini pia ni dhahiri atahitaji wasaidizi bora ili kutekeleza majukumu yake vizuri in terms of delegation of power.
 
Last edited by a moderator:
Mandingo; Umenena ukweli mtupu, mtu kama anaweza sharti apewe fursa kwa ustawi wa taasisi.
 
Last edited by a moderator:
huyu kijana anafaa kuliongoza hilo baraza. bavicha inataka mtu kama katambi.
 
Haya MAKALA Jr ila huwezi kujua content ya kitabu kwa kuangalia cover page tu.
Ila kwa kuwa ulishiba kupitia bakuli la Patrobas na Malisa wewe ukiwa kama waziri mdogo wa mikopo pale CHUONI na mwanaharakati usiyeeleweka eleweka mle darasani kwetu BAPRM na vile vijiwe vyetu vya kisiasa nje ya mwanjonde na pale magazetini basi unaconclude kuwa huyu bwana ni msafi na mzalendo wa ukweli wa kuitetea na kuibeba chadema.
Ila kwa upande mwingine wa mawazo yangu ni kwamba HAFAI KABISA.
Niulize Kwa nini..........!!

jamaa nimewahi kuonana nae mara moja pale ofisi za star tv ni mtu asiyekuwa na makuu na nitofauti na watu wengi wenye wadhifa sehemu fulani na kuongea na watu wa kawaida kama jinsi jamaa alivyo.
Nakumbuka baada ya kujitambulisha jamaa alinikosoa kidogo ila aliniruhusu kuingia na kuonana na mtu niliokuwa na ahadi nae,nikiwa natoka jamaa alinichangamkia mim kwa upande wangu nilijiongeza na kujua ile ilikuws ni sehemu ya kazi.
Hivyo kwa upande wangu napingana na wanaomkosoa kutokana na yeye kufanya kazi kampuni inayomilikiwa na member wa CCM,wakati mwingine tunafanya kazi tusizopaswa kufanya kutona na hali iliyopo kwa wakati husika
 
Last edited by a moderator:
Hongera sana wote mliochaguliwa lkn nia njema au nikutafuta mkate wenye siagi? CHADEMA isipokua makini yaweza baki historia iliyokufa na si historia hai. BAVICHA ndo nguzo na msingi wa chama kosa likifanyika hapo ndo baaasi.
 
Tunataka asiwe muoga na pia awe kichwa ngumu zaidi ya kamanda heche mpiganaji
 
Kila anayemjua patrobas basi atajua chadema imepata kiongozi hasaaa....jamaa ana quality za kiongozi...visionary, determination, focus na ni mtu was kuheshimu kanuni na sheria, humble na msikivu mno....!!!

Sisi tuliosoma Saut mwanza na kushuhudia utendaji wake ni dhahiri kabisa ataifanyia mengi chadema na taifa......!!!

Sifa ya kukilinda na kukitetea chama kwenye kipind ka hiki inamfanya aaminike zaidi katika familia ya chadema
 
Awe mwaminifu daima hadi kifo.
-yaani awe kama mimi ambaye nilizaliwa kichadema,ninaishi kichadema chadema na siku nikifa naamini nitazikwa kichadema kwa nyimbo na mapambio ya kiukombozi.
-kamamda patrobas mungu akubariki na akuonyeshe miujiza katika muda wa uongozi wako wote.
 
ahsante Mungu leo nimefurahi sana kwa habari hii, nimekumbuka siku nilivyotamani akipata nafasi ya kuwa president wa Chuo, ila jina lake likaondolewa, leo nimefurahi sana..... Best wishes brother.... Patrobas.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom