Washawasha
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 16,652
- 13,077
Wanajamv, heshima mbele kama tai. Jamani naomba kuuliza hv kumjua hali jirani yako ni umbea au? maana cc kidini tunatakiwa tuwapende majirani zetu kama tunavyojipenda na bado Twanga pepeta wakaimba nyimbo kuhusu jirani. Sasa mie nilikohamia sasa nimezungukwa na ngozi nyeupe tupu,lkn kama kawa cwabagui naishi nao vzuri lkn leo nimepigwa na butwaa baada ya kumsalimia mmoja kati ya majirani zangu nikabahatika kumuuliza hv: MIMI:Jirani salama lkn? Nilikuona ukitokea hospital vipi unaumwa au? Akanijibu. JIRANI:mie mwenyewe nimekuona unatokea makaburini kwani umekufa au? Kwa kweli ckumjibu ila iliniuma sana mpaka nikajiuliza Jamani nimemkosea nn huyu jamaa au kwasababu mie ni Black?