Nimezaa nae naogopa kumuacha

Nimezaa nae naogopa kumuacha

Chagua kati ya haya,tafuta cha kukuweka busy na usijishughulishe nae kabisa, siku mmoja mtandike makofi na umwambie heshima ikae kati
mvumilie tu huku ukimbembeleza abadilike na ujifanye zoba haswaa.

Naona ushauri huu nimeupenda democracy ikizidi kwenye mahusiano matokeo yake ndiyo kama haya.
 
Kuhusu kumchapa makofi naona ndo itakula kwangu wanawake nowdays wana msaada mno ukishamchapa makofi utaishia polisi tu naona bora nitafute cha kuniweka busy nimpe ruhusa aende zake

Hivi wewe unaishi nyumbani kwake? Au anaishi nyumbani kwako. Maana inaonyesha bado hujamuoa na usikute mtoto mwenyewe siyo wa kwako. Mwache aende mtoto utamchukua akikua kama kweli wa kwako.
 
Anza kuongea na mkeo muulize kwa upole kwamba atajisikiaje mtoto wake kulelewa na mama wa kambo? au muulize malengo yake hapo mbele ni yapi inawezekana umepanga kwenda kumlipia mahari ila mwenzio hana mpango.

Jaribu pia kumweleza hasara nyingine zitakazotokea baada ya kuachana kutokana na yeye kutobadilika. Majibu atakayokupa yatakupa mwongozo ww, utajua mkeo ana malengo gani na analichukulia kwa uzito gan swala hilo. Asipo badilika basi jaribu kuwatumia marafiki/ndugu myaweke sawa.. ikishindikana hapo mwache na mwanao amlee mpaka akue huku ukitoa matumizi yoote yanayohitajika. wewe endelea na mambo yako.
Maisha ni mafupi sana kuishi kwa stress.
 
Hivi wewe unaishi nyumbani kwake? Au anaishi nyumbani kwako. Maana inaonyesha bado hujamuoa na usikute mtoto mwenyewe siyo wa kwako. Mwache aende mtoto utamchukua akikua kama kweli wa kwako.

Ilifikia hatua hata mimi nikajiuliza ninaoa au naolewa! Hakuna jinsi tena namwacha tu
 
Ilifikia hatua hata mimi nikajiuliza ninaoa au naolewa! Hakuna jinsi tena namwacha tu

Ila uangalie mustakabadhi wa mwanao, bila kusahau sio guarantee kuwa mwanamke utayempenda atampenda na mwanao. So tafakari chukua tahadhari.
 
Iko hivi, mwanamke uliezaa naye bila ndoa, akigundua unapenda Sana mtoto/kulea mtoto kuliko kitu kingine chochote duniani, basi atakuwa anakuzimgua kila wakati.

Ndugu, look for the future, wewe Ni mwanaume, Na wewe ndio unaeoa, muweke sawa kwa maongezi, ikishindikana angalia amani ya moyo wako bwana, maana asilete mbwembwe pasipo Na mbwembwe.
 
Endelea kumvumilia mtu asiye mwaminifu, utakapokuja kusikia mr T Kafa kwa ngoma ndo akili itakuja. Kuna makosa ya kuvumilia ila sio kukosa uaminifu
 
Inaonekana kama kwenye mimba ulileta usumbufu na ulikubali kwa mbinde sana pengine mpaka baada ya vikao vya ndugu...
 
Kwanza kwa nini mmezaa kabla ya ndoa, ulipaswa kukabiliana na hizo changamoto mkiwa tayari kwenye ndoa na sio kuzini....kuna kila dalili kuwa unakabiliana na changamoto huku kisaikolojia upo mguu mmoja ndani mmoja nje, jambo ambalo linakupotezea uwezo.

Kufupisha stori, hizo ndizo changamoto za ndoa, na kama ulifikiri ndoa ni pepo basi wewe na huyo mwenzako ndio mnawajibika kuitengeneza na kamwe usifikiri utaikuta pepo iliyoandaliwa tayari alafu nyie muingie tu.

So, oa huyo mkeo then kabiliana na changamoto zenu, ndoa ndio hivyo ndugu.
 
Kumwaacha sio suluhisho la tatizo, hujui huyo mwingine utakayemfwata naye atakuwa vp?. Msingi tulia naye, tafuta watu wa kuwashaurini na yy akiwepo. Maybe isijekuwa hajatambua thamani ya ndoa, akafikiri mwingine ni bora zaid, akasahau kuwa mahusiano ni uvumilivu. Na ww pia angalia wap umepungua, wap unakosea then rekebisha.
 
Bwanae Baba Nikichwa, Naanastahiri Heshima Kama Mume Nababa, Kama Anakudharau Yanini Kujitesa Mwisho Uwe Mteja Wa Dawa Za Presha Nasukari? Mke Mpumbavu Ndani Nisawa Nakidani Chadhahabu Kwenye Pua Yanguruwe, Tafuta Wahadhi Yako Funga Nae Ndoa, Ndo Ajue Mume Anatakiwa Heshima Si Dharau, Kuzaa Namtu Isiwe Shida, Chukua Hatua Kaka
 
Bwanae Baba Nikichwa, Naanastahiri Heshima Kama Mume Nababa, Kama Anakudharau Yanini Kujitesa Mwisho Uwe Mteja Wa Dawa Za Presha Nasukari? Mke Mpumbavu Ndani Nisawa Nakidani Chadhahabu Kwenye Pua Yanguruwe, Tafuta Wahadhi Yako Funga Nae Ndoa, Ndo Ajue Mume Anatakiwa Heshima Si Dharau, Kuzaa Namtu Isiwe Shida, Chukua Hatua Kaka

Shida huyo mtoto atakuwa na wakati mgumu kwa kupata malez ya upande mmoja, angali wazaz wote wapo. Anapaswa kuangalia tatizo ni nn? Na sio kukimbia tatizo..
Cdhani ka mpaka yy kufikia kuzaa nae ilikuwa bahati mbaya, so ni mabadiliko yalotokea baadae na hivyo inawezekana kabisa kumrudisha ktk tabia/hali ya mwanzo..
 
Yani wewe mleta uzi nadhani hazikutoshi vizuri, mna miaka miwili kwenye mahusiano,umemzalisha mtoto wa watu hata kwao bado hujaenda kumtolea mahari unataka tena akupe k,,usikute matunzo yenyewe magumashi maneno mengi vitendo zero kwanini asikudharau?.jitazame upya kasoro zako ,hakuna mwanamke anayeweza kumletea mwanaume dharau bila sababu.
 
Endelea kuogopa usimiache coz hata utakayeenda kumuoa aweza kuwa na makubwa zaidi ya huyo.
 
yani wewe mleta uzi nadhani hazikutoshi vizuri, mna miaka miwili kwenye mahusiano,umemzalisha mtoto wa watu hata kwao bado hujaenda kumtolea mahari unataka tena akupe k,,usikute matunzo yenyewe magumashi maneno mengi vitendo zero kwanini asikudharau?.jitazame upya kasoro zako ,hakuna mwanamke anayeweza kumletea mwanaume dharau bila sababu.

Asante kwa ushauri wako nimejitazama na sioni shaka kwangu! Kama matunzo ingekuwa magumashi nisingeshangaa kwa anavyovifanya lakin kwa kuwa anapata anachohitaji ndo maana ninashangaa!

Kuchelewa kutoa mahali ni kwa kuwa familia yao ina mgogoro kuhusu nani hasa apokee mahali kwa kuwa baba yake alishatangulia mbele ya haki! Mara ya kwanza tulipoenda kulitokea vurugu kati ya wajomba na baba wadogo! Ningefanya nini kama si kuondoka na changu?
 
Back
Top Bottom