Nimewavulia kofia 'HALOTEL'

Nimewavulia kofia 'HALOTEL'

Mimi niliamua kuwakaushia ,siku weka vocha kwa takribani kama mwaka mmoja hivi - sasa wamei deactivate ,ipo kwenye simu muda wote lkn siwez ifanyia kazi.
 
Mkuu nenda kawashitaki nakumbuka tigo nao walikuwa wameniunga kwenye huduma ya kukopeshwa pasipo kuomba mkopo,mwisho wa picha nilienda makao makuu pale makumbusho nikawasha mziki
Mwisho walinitoa kwenye hiyo huduma
 
Aisee haya majambazi sijui ndo majizi HALOTEL ni kasheshe kwenye simu yangu.

Ipo hivi, wiki mbili zilizopita nilijiunga na kifurushi cha mwezi cha 10,000 nikapata Dakika 800 halotel, 80 mitandao yote, na MB 6500. Sasa cha kushangaza mimi huwa nawasiliana na mchumba wangu na yeye ana halotel tu.

Na ni mara chache sana huwa napiga simu mitandao yote na kwa kipindi cha wiki moja baada ya kujiunga na hiki kifurushi sikumbuki hata kutumia zaidi ya dakika 10 mitandao yote.

CHA KUSHANGAZA
Leo naangalia salio la kifurushi nakuta sina dakika halotel halotel, na sina dakika mitandao yote.. nikacheki mda nilioongea na mpenzi wangu hata jumla dakika miatano kwa wiki nzima hazijafika. Yaani nimechoka mpaka sasa najiuliza sipati majibu.

Nafikiria kuliamsha dude ila napiga huduma kwa wateja siwapati.. Nipo nje ya mji kwa sasa mpwawa nafikiria nikirudi nikaliamshe dude.

ILA KWA WANOTUMIA HUU MTANDAO WA MAJAMBAZI KUWENI MAKINI, HAYO MAJITU NI MAJAMBAZI YA KIMATAIFA YENYE MTANDAO WA SIMU

Pole sana mkuu. Mchumba wako huwa unaongea nae every day?
 
Nilishaachana nao kenge wale we nikiweka airtel 1gb na watch 12 videos ila wao 550mb hâta vidéo moja haiishi
 
Voda kila mteja ana nunua vifurushi kivyake kuna wanaonunua cha tshs 350/=kwa siku tatu wengine tshs 750/= kwa siku 1 yaani ni teble
 
Huduma kwa wateja wao hawana,hata mie walivyoniletea uf"*rauni wao nikapiga weee 10 lakini si kupata ya kuongea na muhudumu kwa mteja. Nimelitupa li line lao. Wezi,sana halotel
Mwenyewe nimeteseka mnoo na nimeshangazwa hamna huduma kwa wateja.. huu mtandao ni mbovu zaidi ya ubovu wenyewe.. Kwa ufupi hawa jamaa wanatakiwa wafutiwe hata leseni ya biashara
 
Hawa halotel ni washenzi sana ujanjaujanja wanatufanyia ni mwingi, utakuta umeweka salio la 2000 unataka kifurishi unaambiwa salio halitoshi, ukiangalia salio unakuta 1900, 100 wanakwambia ni quiz
Hiyo naona pia inanitokea kwenye salio langu maana baada ya kuiunga na kifurushi kilibaki kiasi fulani lakini kila siku nikiangalia salio naona ni tofauti na linapungua.. Haloteli ni majambazi majizi
 
Mimi niliamua kuwakaushia ,siku weka vocha kwa takribani kama mwaka mmoja hivi - sasa wamei deactivate ,ipo kwenye simu muda wote lkn siwez ifanyia kazi.
Hiyo ni kuichoma moto tu ndo dawa yao mpaka waache wizi majambazi yale
 
Back
Top Bottom