Nimewavulia kofia 'HALOTEL'

Nimewavulia kofia 'HALOTEL'

Aisee haya majambazi sijui ndo majizi HALOTEL ni kasheshe kwenye simu yangu.

Ipo hivi, wiki mbili zilizopita nilijiunga na kifurushi cha mwezi cha 10,000 nikapata Dakika 800 halotel, 80 mitandao yote, na MB 6500. Sasa cha kushangaza mimi huwa nawasiliana na mchumba wangu na yeye ana halotel tu.

Na ni mara chache sana huwa napiga simu mitandao yote na kwa kipindi cha wiki moja baada ya kujiunga na hiki kifurushi sikumbuki hata kutumia zaidi ya dakika 10 mitandao yote.

CHA KUSHANGAZA
Leo naangalia salio la kifurushi nakuta sina dakika halotel halotel, na sina dakika mitandao yote.. nikacheki mda nilioongea na mpenzi wangu hata jumla dakika miatano kwa wiki nzima hazijafika. Yaani nimechoka mpaka sasa najiuliza sipati majibu.

Nafikiria kuliamsha dude ila napiga huduma kwa wateja siwapati.. Nipo nje ya mji kwa sasa mpwawa nafikiria nikirudi nikaliamshe dude.

ILA KWA WANOTUMIA HUU MTANDAO WA MAJAMBAZI KUWENI MAKINI, HAYO MAJITU NI MAJAMBAZI YA KIMATAIFA YENYE MTANDAO WA SIMU
ULIAMBIWAAA KIFURUSHII N CHAFAMILIA MPAKA UFEE

ANGALIA TAR ULIOJIUNGA ONGEZA SIKU 30. IMEPITAA WELA KINGINE PUNGUZA MUNKARI
 
Nami yamenikuta jana nimenunua muda wa maongezi 10,000 kupitia NMB mobile cha ajabu NMB wameniambia huduma imekamilika na msg ninayo lakini hakukuwa na salio kwenye simu hadi hii leo. Nimepigwa bumbuazi sielewi kilichotokea
 
ULIAMBIWAAA KIFURUSHII N CHAFAMILIA MPAKA UFEE

ANGALIA TAR ULIOJIUNGA ONGEZA SIKU 30. IMEPITAA WELA KINGINE PUNGUZA MUNKARI
Ina maana mi sjui mwezi una siku ngapi mpaka nije kulalamika? Kuwa serious kidogo mkuu.. mi sio mtoto mdogo kuleta hizi tuhuma hapa
 
wew umetumwa na tigo kama sikosei itakuwa ni airtel inawezekana ni voda labda Zantel au TTCL
 
Huduma kwa wateja wao hawana,hata mie walivyoniletea uf"*rauni wao nikapiga weee 10 lakini si kupata ya kuongea na muhudumu kwa mteja. Nimelitupa li line lao. Wezi,sana halotel
 
HALOTEL Mb zinapepea sana
Mimi Nina laini zote
Hapa nawatathmin Zantel nao niwaone mbwembwe wakizingua pia nawahama.
 
Hawa halotel ni washenzi sana ujanjaujanja wanatufanyia ni mwingi, utakuta umeweka salio la 2000 unataka kifurishi unaambiwa salio halitoshi, ukiangalia salio unakuta 1900, 100 wanakwambia ni quiz
 
Back
Top Bottom