Nimewavulia kofia 'HALOTEL'

Nimewavulia kofia 'HALOTEL'

Naantombe Mushi

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
6,254
Reaction score
15,735
Aisee haya majambazi sijui ndo majizi HALOTEL ni kasheshe kwenye simu yangu.

Ipo hivi, wiki mbili zilizopita nilijiunga na kifurushi cha mwezi cha 10,000 nikapata Dakika 800 halotel, 80 mitandao yote, na MB 6500. Sasa cha kushangaza mimi huwa nawasiliana na mchumba wangu na yeye ana halotel tu.

Na ni mara chache sana huwa napiga simu mitandao yote na kwa kipindi cha wiki moja baada ya kujiunga na hiki kifurushi sikumbuki hata kutumia zaidi ya dakika 10 mitandao yote.

CHA KUSHANGAZA
Leo naangalia salio la kifurushi nakuta sina dakika halotel halotel, na sina dakika mitandao yote.. nikacheki mda nilioongea na mpenzi wangu hata jumla dakika miatano kwa wiki nzima hazijafika. Yaani nimechoka mpaka sasa najiuliza sipati majibu.

Nafikiria kuliamsha dude ila napiga huduma kwa wateja siwapati.. Nipo nje ya mji kwa sasa mpwawa nafikiria nikirudi nikaliamshe dude.

ILA KWA WANOTUMIA HUU MTANDAO WA MAJAMBAZI KUWENI MAKINI, HAYO MAJITU NI MAJAMBAZI YA KIMATAIFA YENYE MTANDAO WA SIMU
 
Aisee haya majambazi sijui ndo majizi HALOTEL ni kasheshe kwenye simu yangu.

Ipo hivi, wiki mbili zilizopita nilijiunga na kifurushi cha 10,000 nikapata Dakika 800 halotel, 80 mitandao yote, na MB 6500. Sasa cha kushangaza mimi huwa nawasiliana na mchumba wangu na yeye ana halotel tu.

Na ni mara chache sana huwa napiga simu mitandao yote na kwa kipindi cha wiki moja baada ya kujiunga na hiki kifurushi sikumbuki hata kutumia zaidi ya dakika 10 mitandao yote.

CHA KUSHANGAZA
Leo naangalia salio la kifurushi nakuta sina dakika halotel halotel, na sina dakika mitandao yote.. nikacheki mda nilioongea na mpenzi wangu hata jumla dakika miatano kwa wiki nzima hazijafika. Yaani nimechoka mpaka sasa najiuliza sipati majibu.

Nafikiria kuliamsha dude ila napiga huduma kwa wateja siwapati.. Nipo nje ya mji kwa sasa mpwawa nafikiria nikirudi nikaliamshe dude.

ILA KWA WANOTUMIA HUU MTANDAO WA MAJAMBAZI KUWENI MAKINI, HAYO MAJITU NI MAJAMBAZI YA KIMATAIFA YENYE MTANDAO WA SIMU
Ulijiunga kifurushi cha muda gani?
Maana inawezekana kifurushi chako kime expire Mkuu
 
Kuna siku walinikata mb 500 ndani ya masaa 3 tu na nilikuwa nimezitumia jf na whatsapp tu na sikudownload kitu chochote, tangu siku hiyo sijawahi kuitumia tena.
 
Hilo tokeo limenitokea juzi na nikwafata ofisin kuwauliza ikiwa wana tatizo manake naona kifurush na dakika zilikatwa hafla. Wakaniambia hakuna tatizo
 
Kuna siku walinikata mb 500 ndani ya masaa 3 tu na nilikuwa nimezitumia jf na whatsapp tu na sikudownload kitu chochote, tangu siku hiyo sijawahi kuitumia tena.
Hawafai hawa jamaa.. Na kwa hali hii ya vyuma kukaza nahisi wanazidi kuvichomelea kabisa
 
Back
Top Bottom