Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Sijui kama watanielewa, nahisi watachukia. Ila kama posho zao zimeongezwa, labda watacheka tu. Lakini ukweli ndio huu, na nimeamua kuusema wazi hapa JF -where we dare to talk openly! Kila nikikumbuka niliyofanya, najua kabisa madaktari wana kila sababu ya kunikazia macho. Lakini kabla wewe msomaji hujanihukumu, soma hadi mwisho, kisha uniambie kama nimekosea kuwanyima pesa madaktari au la.
Iko hivi: mimi nikiona dalili za magonjwa mwilini, sikimbilii kwa madaktari kuomba wanipime naumwa nini. Badala yake naweka mkono wangu sehemu inayouma na kukemea dalili za ugonjwa kwa Jina la Yesu. Kwa njia hii na kwa kumuomba Mungu, nimepona magonjwa mengi bila kulipa pesa ya kumuona daktari au kununua dawa. Jana nilisikia maumivu makali sana mwilini. Nikayakemea kwa Jina la Yesu. Instantly, nikapona. Jambo hili nimelifanya mara nyingi sana. Hivyo kwa sehemu kubwa nimewanyima pesa madaktari. Najua, kuna madaktari wanaofurahia kuona 'nyomi' la wagonjwa wakiwa wamejipanga foleni hospitali kusubiri huduma. Hivyo watu kama mimi, wenye imani ya kupona kwa Jina la Yesu tukiwa wengi, ni huzuni kwao kwa sababu tutakuwa tunawanyima pesa ya kununua ugali.
Usininukuu vibaya. Sijasema madaktari hawafai. Nope. Ni watu muhimu sana. Wameokoa maisha ya watu wengi, na Mungu huwa anawatumia pia. Lakini mimi nimekuwa nikichagua shortcut, njia isiyo na gharama, sio kwa kiburi, bali kwa imani. Kama kwa kufanya hivyo nimewanyima riziki yao, basi wanisamehe bure tu. Maana sio kwa chuki, sio kwa dharau, ila kwa neema niliyopewa ya kutumia Jina lipitalo majina yote. Kama nimefanya makosa, basi ni imani yangu. Na kama ni kosa kuamini kwamba Yesu bado anaponya, basi sina la kujitetea, ila nitasimama na ushuhuda wangu hadi mwisho, kwamba Yesu anaponya hata leo!
NAKAZIA: Kwa bandiko hili, sikuambii usiende hospitali. Kama imani yako ni haba, ukisikia dalili za ugonjwa, fanya haraka uende ukapimwe, upewe dawa. La sivyo, utakata moto. Na kama hujaokoka, ukiondoka duniani, utaenda kuteseka zaidi jehanam.
Hata mimi huwa naenda hospitali mara moja moja, ila nikienda, siweki matumaini yangu kwa madaktari, kwa sababu na wao kuna wakati wanashindwa kujua chanzo cha ugonjwa ni nini. Na kuna wengine sijui ni kusahau waliyofundishwa chuoni au nini, mpaka wa-google kwanza websites za kitabibu ndio wanakuambia unaumwa nini.
Na wengine huwa wanatumiwa kabisa na Ibilisi, kuwakatisha tamaa wagonjwa. Kuna siku nilienda hospitali fulani ili kupata matibabu baada ya kupungukiwa damu. Swali la kwanza aliloniuliza daktari ni hili: "Wewe umepeleka wapi damu?" Hili ni swali la kishetani kabisa. Namshukuru Mungu aliyeiumba damu, aliiongeza mwilini mwangu ikarudi kwenye viwango vyake, kwa miujiza yake. Haleluya!
Iko hivi: mimi nikiona dalili za magonjwa mwilini, sikimbilii kwa madaktari kuomba wanipime naumwa nini. Badala yake naweka mkono wangu sehemu inayouma na kukemea dalili za ugonjwa kwa Jina la Yesu. Kwa njia hii na kwa kumuomba Mungu, nimepona magonjwa mengi bila kulipa pesa ya kumuona daktari au kununua dawa. Jana nilisikia maumivu makali sana mwilini. Nikayakemea kwa Jina la Yesu. Instantly, nikapona. Jambo hili nimelifanya mara nyingi sana. Hivyo kwa sehemu kubwa nimewanyima pesa madaktari. Najua, kuna madaktari wanaofurahia kuona 'nyomi' la wagonjwa wakiwa wamejipanga foleni hospitali kusubiri huduma. Hivyo watu kama mimi, wenye imani ya kupona kwa Jina la Yesu tukiwa wengi, ni huzuni kwao kwa sababu tutakuwa tunawanyima pesa ya kununua ugali.
Usininukuu vibaya. Sijasema madaktari hawafai. Nope. Ni watu muhimu sana. Wameokoa maisha ya watu wengi, na Mungu huwa anawatumia pia. Lakini mimi nimekuwa nikichagua shortcut, njia isiyo na gharama, sio kwa kiburi, bali kwa imani. Kama kwa kufanya hivyo nimewanyima riziki yao, basi wanisamehe bure tu. Maana sio kwa chuki, sio kwa dharau, ila kwa neema niliyopewa ya kutumia Jina lipitalo majina yote. Kama nimefanya makosa, basi ni imani yangu. Na kama ni kosa kuamini kwamba Yesu bado anaponya, basi sina la kujitetea, ila nitasimama na ushuhuda wangu hadi mwisho, kwamba Yesu anaponya hata leo!
NAKAZIA: Kwa bandiko hili, sikuambii usiende hospitali. Kama imani yako ni haba, ukisikia dalili za ugonjwa, fanya haraka uende ukapimwe, upewe dawa. La sivyo, utakata moto. Na kama hujaokoka, ukiondoka duniani, utaenda kuteseka zaidi jehanam.
Hata mimi huwa naenda hospitali mara moja moja, ila nikienda, siweki matumaini yangu kwa madaktari, kwa sababu na wao kuna wakati wanashindwa kujua chanzo cha ugonjwa ni nini. Na kuna wengine sijui ni kusahau waliyofundishwa chuoni au nini, mpaka wa-google kwanza websites za kitabibu ndio wanakuambia unaumwa nini.
Na wengine huwa wanatumiwa kabisa na Ibilisi, kuwakatisha tamaa wagonjwa. Kuna siku nilienda hospitali fulani ili kupata matibabu baada ya kupungukiwa damu. Swali la kwanza aliloniuliza daktari ni hili: "Wewe umepeleka wapi damu?" Hili ni swali la kishetani kabisa. Namshukuru Mungu aliyeiumba damu, aliiongeza mwilini mwangu ikarudi kwenye viwango vyake, kwa miujiza yake. Haleluya!
