Kayoka
JF-Expert Member
- Jun 21, 2011
- 2,389
- 2,217
"Habari Wakuu,
Kama mjuavyo jinsi maisha yalivyo magumu kwa sasa huku mtaani, lazima akili na maarifa yaongezeke.
Nilimaliza chuo tangu 2015 ila mpaka sasa sijabahatika kupata kazi ya kueleweka na kila ndugu mwenye uwezo niliyemwomba msaada hakuwa tayari kunisaidia (niliwaomba mtaji tu wa kuanzia).
Nikaondoka home na kwenda kujitafutia maisha mwenyewe mbali na nyumbani ila bado nikapigika nikaamua kurudi tena nyumbani kwa baba na mama kujipanga upya.
Kuja tu hapa nikapata wazo la kutangaza kuoa na kufunga ndoa na mpenzi wangu wa siku nyingi huku nikimpa taarifa kila ndugu, rafiki, jamaa na watu wa karibu na wao pia wameniunga mkono na kutangaza kuchangia kiasi kikubwa cha pesa, mpaka sasa tayari nimechangiwa 5.4M na ahadi zingine kibao.
Ndoa inataarijiwa kufungwa 10/08/2019 ila dhumuni langu nikipata tu hiyo hela natokomea huko Msumbiji kutafuta maisha machimboni kwani tayari mtaji nitakuwa nimepata.
Ushauri wenu wakuu katika hili ninalotaka kufafanya, Je niko sawa au najitafutia laana na kufungwa mbele ya sheria?"
Kama mjuavyo jinsi maisha yalivyo magumu kwa sasa huku mtaani, lazima akili na maarifa yaongezeke.
Nilimaliza chuo tangu 2015 ila mpaka sasa sijabahatika kupata kazi ya kueleweka na kila ndugu mwenye uwezo niliyemwomba msaada hakuwa tayari kunisaidia (niliwaomba mtaji tu wa kuanzia).
Nikaondoka home na kwenda kujitafutia maisha mwenyewe mbali na nyumbani ila bado nikapigika nikaamua kurudi tena nyumbani kwa baba na mama kujipanga upya.
Kuja tu hapa nikapata wazo la kutangaza kuoa na kufunga ndoa na mpenzi wangu wa siku nyingi huku nikimpa taarifa kila ndugu, rafiki, jamaa na watu wa karibu na wao pia wameniunga mkono na kutangaza kuchangia kiasi kikubwa cha pesa, mpaka sasa tayari nimechangiwa 5.4M na ahadi zingine kibao.
Ndoa inataarijiwa kufungwa 10/08/2019 ila dhumuni langu nikipata tu hiyo hela natokomea huko Msumbiji kutafuta maisha machimboni kwani tayari mtaji nitakuwa nimepata.
Ushauri wenu wakuu katika hili ninalotaka kufafanya, Je niko sawa au najitafutia laana na kufungwa mbele ya sheria?"