Nchi Kavu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 4,271
- 2,401
- Thread starter
- #61
Wallet umeongea kitu kimoja muhimu sana, kuwa unaogopa usije kufuata channels zote hizo halafu ukaja kugundua kuwa kumbe binti labda hutaweza kuwa nae... nina mfano kama huo, wakati tuko wadogo tulikuwa na msichana msaidizi wa kazi za ndani (kama unvyoita wewe HG) mmoja, basi akatokea jamaa akajidai anataka kumchumbia, akaja home akajitambulisha kabisa, sasa wakati mama yangu anafanya mipango ya kuwasiliana na wazazi wa yule msichana jamaa akawa kumbe ana chakachua, mara jamaa akamtosa yule binti. You know what happened yule binti akachangayikiwa akataka mpaka kunywa sumu, mara akawa muhuni sana na hakuwa hivyo before, yaani vijana mtaani walitungua mpaka ikawa noma, ikabidi arudishwe kwao, tulikuja kupata taarifa kuwa alikufa kwa ukimwi. Ilinisikitisha sana kwani hakuwa hivyo kabisa na linilea vizuri sana.
Sasa mzee ushauri wangu hapo ni kuwa, labda wewe kiaina mtafute mwenyewe kwa muda wako, yaani isiwekwe rasmi sana kwani na yeye anaweza kujipa hope.. jamaa yako atengeneze mazingira tu kiujanja ili wewe uweze kuongea nae na kumpima.
I hope hiyo itasaidia.
nami nahofia hayo mkuu. Tatizo informal channels ni imposibo. Ni bora pia wangekuwa majirani