[h=5]Unaenda nyumbani kwa mpenzi wako kutembea,na kwa mmomonyoko wa maadili wa siku hizi unalala hukohuko japo hata ndoa hujaambiwa ipo au haipo,sio neno...Unaondoka asubuhi unaacha Khanga...next time unaacha pichu,tena nyuma ya mlango...next time unaacha hereni..Next time gagulo...Hivi hii tabia mmepewa na mganga yuleyule au ni vipi?Unaacha vikorombwezo as if hao watu wana kabati special ku-accomodate miguo yako kwao...Eti madai yenu mnaacha alama ili incase akiingia mtu mwingine akute...Nimetumwa niseme hili,wamechoka kuficha vifaa vyenu maana inabidi wanunue mabegi maalum kuficha madude mnayojifanya mmeyasahau,kumbe makusudi tu,waone kwanza!,mwishowe haya magheto yanakuwa kama ya muuza mtumba,Vibanio,pichu,pajama,khanga,lipshine ,mawigi,mwishowe rafiki zetu wanaweza kudhani tumekuwa mashoga sasa....Au wazazi wetu waje ghafla wakute Girls' items,SIO HESHIMA....njoo salimia,beba mikanga yako nenda nayo kwenu,sisi sio wauza urembo![/h]