Hellow
Leo nimepata makasririko gafla sana yaani nilikuwa naenda zangu mbezi kwa magufuli na mgeni wangu nimeshuka kwenye gari mdada anakuja unaenda wapi nikamjibu mbinguni yapo mabus? Akaniacha niendelee nasafari yangu
Mbele tena nakutana mwingine kaka wapi mdogo wetu wapi mbona hujibu mh unaharaka utafikiri unaenda kumzika baba yako ase nilichukia hilo jibu nikifikilia baba yangu kafariki kaniacha mtoto niligeuka na kofi moja akaangukia kwenye fensi
Wakaja nishika watu bila ya watu ningemfundisha adabu huwa sipendi ujinga na nachokaga sana nikiwaza kwenda kwa magufuli nikifikilia tu madalali
Mkuu umempiga kwa mikono yako mwenyewe au ilikuwa ni ndoto tu?
Maana ndoto nazo waweza kuzitungia simulizi katika sura ya uhalisia.
Sioni mantiki yoyote ya ugomvi hapo.
Ujue kila eneo lina mazingira yake, utamaduni wake na lugha zake.
Ukianza safari kwa usafiri wa mabasi unapofika stendi ni lazima ukutane na hao watu na lugha zao hizo za mitaani.
Kurusha ngumi ni dalili za ukorofi uliopitiliza, kukosa ustaarabu, kukosa uhimilivu na kukosa uvumilivu.
Wafungwa wa matabaka yote mpaka wale wa "condemn", ukipata wasaa kuhoji mmoja mmoja akueleze sababu zilizomtia matatani, wengine watakueleza chanzo chake ni sababu za kujitakia kama za kwako hizo.
Jiepushe siku zote kujiingiza katika shari zisizokuwa na manufaa.
Kunguru mjanja na muoga huziepusha mbawa zake, ndiyo maana huishi miaka mingi.
Kosa la kupigana hadharani unalijua adhabu yake?
Uliyempiga, ulimpima afya yake ukabaini ni mzima wa afya inayohimili vishindo vya masumbwi yako?
Ungelimpiga akazima mazima ungelikuja kuanzisha thread hapa?
jamani vijana nyie!