Nimetendwa jamani

Nimetendwa jamani

salula

Member
Joined
Feb 21, 2014
Posts
16
Reaction score
6
Mimi ni msichana nilitokea kumpenda kijana mmoja sana kiasi ambacho sikuwahi kuhis kama naweza kuishi bila yeye but yamenikuta,kuanzia valentine asubuhi alinitumia sms ananipenda sana ila anaondoka anaenda huko vijijini kuna project anafanya since that day hajapatikana mpaka leo,nikaona nimuulize rafiki yake ananiambia mbona kabadilisha namba na hataki nimpe mtu,nimelia usiku mzima sijalala naumia jamani hata nashindwa kufanya kazi
 
Acha ujinga mwanangu salula,songa mbele.Kwani yeye kaanza kwako na wewe kwake?

Mzee Tupatupa
 
Last edited by a moderator:
Kwani mwanamme ndiye yy pekee duniani?Nenda kwa strikers wengine watakutuliza mtima wako
 
Ah,pole sana ,lkn kulia sana si dawa ya tatizo,dawa ni kutafuta jembe lingine litakalolima vizuri.Mi ni mmoja wao,jaribu sasa
 
Njoo pm bibie nikuliwaze. Achana nao hao wasiojua thamani ya chozi la mwanamke
 
Pole sana,piga moyo konde maisha uyashinde bado safari ndefu yenye miiba na mabonde.
 
Pole mpendwa....mahusiano yenu yana muda gani? una uhakika hajaoa..hana mke? Futa machozi, songa mbele binti
 
Hili ndilo kosa nambari moja wafanyalo baadhi ya wanawake wawapo kwenye mahaba...hukabidhi mioyo yao kwa wanaume.

Amka kutoka katika usingizi uliolala eeh binti
yaani alikabidhi mwili mzima mzima siyo moyo tu hakujua wenzie wanaanzaga hata na ukucha tu, pole sana binti amka futa vumbi maisha bado yanasonga mbele, usijali akunyimaye mbaazi kakunyima mashuzi.
 
Hili ndilo kosa nambari moja wafanyalo baadhi ya wanawake wawapo kwenye mahaba...hukabidhi mioyo yao kwa wanaume.

Amka kutoka katika usingizi uliolala eeh binti

ndugu yangu sisi wanwake ndo tulivyo tukipenda tumependa bwana hatuna matuta kwenye moyo kama nyinyi wanaume, its nature, once give up our heart we give up our part
 
Binti ukilia hujasolve tatizo kwa kumtumia rafiki yake utajua hatma yoko.

afu kwan huyo mwanaume anatatizo la kutojiamin hv hawez kuachana na mwanamke kiroho safi tu?? nadhan angekwambia ukwel kubadilisha no, sio sln
 
yaani alikabidhi mwili mzima mzima siyo moyo tu hakujua wenzie wanaanzaga hata na ukucha tu, pole sana binti amka futa vumbi maisha bado yanasonga mbele, usijali akunyimaye mbaazi kakunyima mashuzi.

Hahaha!! jambo zuri ni kuwa ingali mapema kashajua mbivu na mbichi
 
ndugu yangu sisi wanwake ndo tulivyo tukipenda tumependa bwana hatuna matuta kwenye moyo kama nyinyi wanaume, its nature, once give up our heart we give up our part

Nimepata kushuhudia baadhi ya wanawake wanaoshirikisha akili katika mapenzi, huwa hawababaishwi na porojo zetu za kiume
 
pole dada,,,,,,,,,,,,,,,,,,
Badilika sasa na priority yako iwe hivi;
1 Tumia akili yako na nguvu kusaka pesa
2 jipende mwenyewe na tambua thamani yako
3 mapenzi.
 
Hahaha!! jambo zuri ni kuwa ingali mapema kashajua mbivu na mbichi

Na kweli bado mapema ashukuru,ila unaweza kukuta huyo ndo mwanaume wake wa kwanza ndo maana kaumia sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom