Nimepoteza Pete ya ndoa, ushauri wa haraka

Nimepoteza Pete ya ndoa, ushauri wa haraka

Mzalendo39

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2015
Posts
881
Reaction score
1,035
Habari za humu wanajamiiForums,

Tangu saa 10 jioni nikiwa njiani kuelekea nyumbani kutoka kazini baada ya kumaliza kazi za leo, nimejikuta ghafla sina pete ya ndoa na katika kumbukumbu zangu nikakumbuka kuwa niliivua nikiwa ofisini nikageuza gari kurudi kazini kwa ajili ya kwenda kuichukua.

Nimefika ofisini nimetafuta pete mpaka muda huu saa 2 usiku sijafanikiwa kuipata kwa bahati mbaya mke wangu bado sijamjulisha. Kwa bahati mbaya maduka muda huu Karikoo yamefungwa.

Naombeni ushauri kwani nahisi nikifika nyumbani mambo yanaweza yasiwe sawa kutokana na;

1. Nimezoea kurudi mapema nyumbani kufikia 12 jioni huwa tayari nimefika nyumbani na leo hii kuchelewa halafu sina pete.

2. Siku za hivi karibu mke wangu amekuwa akihisi natoka nje ya ndoa hivyo tumekuwa na kamvutano ka chinichini.

3. Narudi bila pete ya ndoa
 
Yaani we huna defence yoyote uliivua ili iweje kama sio nia mbaya? Nani kakuambiaga kuwa inavuliwa ukiwa kazini? MI SIKUSHAURI KITU WE NENDA TU NYUMBANI MKEO AKATHIBITISHE KUWA UMEAMUA KUINYEA NDOA YENU KWA AJILI YA VIMADA VYA OFISINI KWENU.
 
Ukiwa muaminifu kwenye ndoa utaishi kwa amani ila ukianza ujanja ujanja tu ipo siku utafumwa na maisha yako yanakuwa hayana Amani.
NB:KUWA MUAMINIFU KUNATUNZA HESHIMA YAKO NA KUTUNZA KIPATO CHAKO MAISHA YAMEKUWA MAGUMU TUSIISHI TULIVYOZOEA
 
Ingia kwa machinga, vibandani huko kuna pete za buku 2..
 
Heee sasa mkuu ofisin kwenu hawajui kama umeoa?au hauruhusiwi kufanya kazi ukiwa umevaa pete ya ndoa?
 
Hahahaaaa bila shaka ofisin kwenu kuna intake mpya. Pole mkuu we nenda tu. Ila hakikisha unanipa namba ya mai waifu wako nimpigie kabla hujafika home. Otherwise moto wake hutauweza. Namjua sana yule. Tuma namba fasta nimpoze
 
Habari za humu wanajamii forum tangu saa 10 jioni nikiwa njiani kuelekea nyumbani kutoka kazini baada ya kumaliza kazi za leo, nimejikuta ghafla sina pete ya ndoa na katika kumbukumbu zangu nikakumbuka kuwa niliivua nikiwa ofcn.....nikageuza gari kurudi kazini kwa ajili ya kwenda kuichukua.

Nimefika ofcn nimetafuta pete mpaka muda huu saa 2 usiku sijafanikiwa kuipata kwa bahati mbaya mke wangu bado cjamjulisha. Kwa bahati mbaya maduka muda huu karikoo yamefungwa

Naombeni ushauri kwani nahisi nikifika nyumbani mambo yanaweza yasiwe sawa kutokana na

1. Nimezoea kurudi mapema nyumbani kufikia 12 jioni huwa tayari nimefika nyumbani na leo hii kuchelewa halafu sina pete

2. Siku za hivi karibu mke wangu amekuwa akihisi natoka nje ya ndoa hivyo tumekuwa na kamvutano ka chinichini

3. Narudi bila pete ya ndoa
Kidole umepoteza pia?
 
IMG-20170215-WA0051.jpg
 
Nahisi ipo kwenye Wallet....ukikosa tazama mfuko wa suruali wa nyuma.....inaonekana mgeni kwenye ndoa.
 
Unapigwa na mkeo au?!..kwan pete ikipotea kuna tatizo gani...si unampa taarifa tu,maana hauhitaji kumwrleza story ndefu pete imepotea basi hamna la zaidi
Mh!kwanza mke alishahisi jamaa anachepuka,pili pete imepotea kirahisi rahisi tuu halaf wewe unadhan ni kitu rahisi
 
Back
Top Bottom