Makongoro Igana
New Member
- Jan 8, 2023
- 4
- 31
Mimi ni kijana (Me) wa miaka 30 na ninaishi Dar es salaam. Mimi ni mhitimu wa shahada ya kwanza ya elimu na niko katika hatua ya mwisho ya kuhariri tasnifu yangu ili niweze kuhitimu shahada ya umahiri katika mipango na menejimenti ya miradi.
Nilikuwa nafanya kazi kwny kampuni moja na miezi sita iliyopita nmepandishwa cheo na kuanza kusimamia idara mbili kama meneja. Toka nilipopandishwa cheo zikaibuka fitna, majungu, uchonganishi na husuda za waziwazi kutoka kwa wafanyakazi wenzangu wakiongozwa na jamaa mmoja wa makamo ya 40’s ambaye kwa uwezo, elimu na vigezo vya nafasi nilipo hawezi kurithi nafasi yangu. Nilitamani nielezee hiki kisa kwa kirefu ili hata iwe funzo Kwa wengine lakini naogopa ku-disclose mambo ya kampuni hyo hapa.
Nasema wazi wanafamilia wenzangu wa Jf nimefanyiwa vitimbwi vingi ambavyo nimevumilia na kupotezea maana nafasi yangu kazini ilihitaji hitaji hekima, busara na utulivu. Kuna muda nilikubali kuumia na hata kuhatarisha uhai wangu. Lakini imefika hatua hivi vita wamevishinda nimepoteza kazi.
Nmekaa nikatafakari na nikaomba ushauri sana juu ya reaction yangu kwa hawa watu. Wengi wamenishauri niwaharibie kitu ambacho kwangu nikiamua naweza hata nikiwa nje ya kazi. Nmetafakari kuhusu destiny za ndugu zao, familia na wengine wanaowategemea. Nmeamua kutokulipa kisasi na kuamua kuacha Karma na Mungu vichukue nafasi. Kwani kilichonipata sitaki kimpate mwingine hata huyu aliyekisababisha.
Nmepoteza kazi katika kipindi ambacho nauguza wazaz wangu wote wawili nmewatoa kijijini wapo hapa Dar na nikiwa katika majukumu ya kusomesha mwanangu na watoto wa marehem dada yangu. Nmeumia sana moyo unadunda kila saa, kula Siwez na najikaza wazaz wasijue nisiwaue kwa pressure. USIOMBE HALI HII IKUKUTE
Kabla sijapata hii kazi niliyokuwa nafanya mara ya mwisho, Nimewahi kufanya kazi katika kampuni moja ya biashara na nmefanya kazi za muda kwa makubaliano na CSOs changa ambazo mara nyingi ni za kujitolea au kwa ujira kidogo kutokana na uchanga wa taasisi hizi, kuandika proposal za research za watu na kazi nyingine za kitaalumu kusaidia watu.
Katika kipindi hiki ndugu zangu nipo katika hali mbaya sana. Kwa mwana JF yeyote atakayeguswa na hili anisaidie angalau hata Kwa kazi, connection au hata ushauri wa mawazo tu. Nipo kwenye hali ya kukata tamaa na sijui moyo wangu utawaza nini kesho.
Nimelazimika kutokutaja kampuni na mambo mengine mengi kwa sababu ya kulinda image yake.
Nilikuwa nafanya kazi kwny kampuni moja na miezi sita iliyopita nmepandishwa cheo na kuanza kusimamia idara mbili kama meneja. Toka nilipopandishwa cheo zikaibuka fitna, majungu, uchonganishi na husuda za waziwazi kutoka kwa wafanyakazi wenzangu wakiongozwa na jamaa mmoja wa makamo ya 40’s ambaye kwa uwezo, elimu na vigezo vya nafasi nilipo hawezi kurithi nafasi yangu. Nilitamani nielezee hiki kisa kwa kirefu ili hata iwe funzo Kwa wengine lakini naogopa ku-disclose mambo ya kampuni hyo hapa.
Nasema wazi wanafamilia wenzangu wa Jf nimefanyiwa vitimbwi vingi ambavyo nimevumilia na kupotezea maana nafasi yangu kazini ilihitaji hitaji hekima, busara na utulivu. Kuna muda nilikubali kuumia na hata kuhatarisha uhai wangu. Lakini imefika hatua hivi vita wamevishinda nimepoteza kazi.
Nmekaa nikatafakari na nikaomba ushauri sana juu ya reaction yangu kwa hawa watu. Wengi wamenishauri niwaharibie kitu ambacho kwangu nikiamua naweza hata nikiwa nje ya kazi. Nmetafakari kuhusu destiny za ndugu zao, familia na wengine wanaowategemea. Nmeamua kutokulipa kisasi na kuamua kuacha Karma na Mungu vichukue nafasi. Kwani kilichonipata sitaki kimpate mwingine hata huyu aliyekisababisha.
Nmepoteza kazi katika kipindi ambacho nauguza wazaz wangu wote wawili nmewatoa kijijini wapo hapa Dar na nikiwa katika majukumu ya kusomesha mwanangu na watoto wa marehem dada yangu. Nmeumia sana moyo unadunda kila saa, kula Siwez na najikaza wazaz wasijue nisiwaue kwa pressure. USIOMBE HALI HII IKUKUTE
Kabla sijapata hii kazi niliyokuwa nafanya mara ya mwisho, Nimewahi kufanya kazi katika kampuni moja ya biashara na nmefanya kazi za muda kwa makubaliano na CSOs changa ambazo mara nyingi ni za kujitolea au kwa ujira kidogo kutokana na uchanga wa taasisi hizi, kuandika proposal za research za watu na kazi nyingine za kitaalumu kusaidia watu.
Katika kipindi hiki ndugu zangu nipo katika hali mbaya sana. Kwa mwana JF yeyote atakayeguswa na hili anisaidie angalau hata Kwa kazi, connection au hata ushauri wa mawazo tu. Nipo kwenye hali ya kukata tamaa na sijui moyo wangu utawaza nini kesho.
Nimelazimika kutokutaja kampuni na mambo mengine mengi kwa sababu ya kulinda image yake.