Nimepima Hepatitis B niko positive

Nimepima Hepatitis B niko positive

NYOTIENO JARIEKO

Senior Member
Joined
Apr 29, 2017
Posts
196
Reaction score
325
Baada ya kufuatilia uzi hapa inayohusu Hepatitis B, leo nilienda kufanya vacination, wakasema hawawezi kutoa vacination bila kupima, wakapima nikiwa naona kwa sababu aliyenipima tunazoea naye.

Baada ya kupima, ikatiki (ikareact), akabadilisha kipimo ya kampuni nyingine.

Ikatiki tena (ikareact) hapo nikaprove am Hepatitis B positive, akaniomba nakapime na HIV ili ajue jinsi ya kunikacounsel kwa kuwa sikuwa na wasi wasi kwenye HIV coz najijua na najitahidi sana kujikinga pamoja na kupima HIV mara kwa mara vipimo viwili tofauti ikaonyesha Negative (Non reactive).

Hapa nimeshauriwa nitatumia ARV kwa miezi sita alafu narudia kupima tena, wakanitia moto nitapona bila shida.

Nawauliza kuna aliyewahi kutumia ARV (TLD) kutibu Hepatitis B disease anipe mwongozo, alipoenda kupima baada ya kutumia dawa alipata majibu aina gani?

Unapona kweli? Au nikusubiri kifo mapema? Cha ajabu sijawahi kusikia tatizo lolote kubwa ya kiafya.

Naomba msaada kwa mwenye uelewa na cha kufanya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi siyo Virologist lkn nafikiri kuna utata, kwani cha muhimu ni viral load au kiasi cha viruses ulichonacho hilo ndiyo muhimu, na pia hepatetis B kuna chronic na acute, watu wengi walio na hepatetis B Tanzania walipata kutoka kwa mama zao wakati wanazaliwa kwa kuwa Tanzania hakuna chanjo ili kuzuia maambukizi ya virus ktk kwa mama kwenda kwa mtoto, hivyo bado Watanzania wengi bila ya kujua wanaishi na virus vya hepatetis B.

Kinachoamua kama uanze kutumia dawa au la ni kiasi cha virus au viral load, na hilo Daktari virologist lazima ajue.

Hepatetis B haina dawa, maana yake ni kwamba utaishi na virus mpaka mwisho wa maisha yako ila cha muhimu kuliko vyote ni afya ya ini, kwani hawa virus wa hep B husababisha saratani ya ini ambayo haina kinga, hivyo ni lazima kufanya vipimo vya ini, ...
 
Nenda Geita..Fanya Ngono zembe au kua na contact ya mate ,chuchu na wanawake tofauti 10 ..usipoondoka na HBV shukuru..... HBV kwa sasa inatishia Geita, Kahama, Sengerema.


Kwa habari ya HBV-

Ikiwa mgonjwa yupo kwa acute stage huyu akitumia Dawa vzuri ANAPONA


Lkn umejuaje kama ni acute au chronic? Kwa kawaida ni Daktari tu ndo anaweza kusema baada ya vipimo vya maabara.
 
nmesemea ni Acute kwa uzoefu tu Mkuu.....


Haya mambo hayana uzoefu, ni lazima vipimo kutoka maabara viseme na vile vile historia ya mgonjwa, kama ndo kwanza ameambukizwa basi ni lazima atakuwa na dalili za kuumwa lkn kama ni chronic huwa mara nyingi hamna dalili mpaka ini likishambuliwa na kuja kushtuka muathirika ana saratani ya ini, na hapo ni mwisho kwani saratani ya ini haina dawa.
 
Haya mambo hayana uzoefu, ni lazima vipimo kutoka maabara viseme na vile vile historia ya mgonjwa, kama ndo kwanza ameambukizwa basi ni lazima atakuwa na dalili za kuumwa lkn kama chronic huwa mara nyingi hamna dalili mpaka ini likishambuliwa na kuja kushtuka muathurika ana saratani ya ini, na hapi ni mwisho kwani saratani ya ini haina dawa.
Aiseee haya maisha huwezi kuona thamani yake ukiwa na afya njema.ukipata magonjwa kama haya ndio unaona thamani ya kuwa na afya njema.dah!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
unajua tunaposema Hepatitis ni maambukizi ya Ini yanasosababishwa na Virus tofauti kama vile Flavivirus, Hepadna Virus , Calicivirus , Enterovirus n.k......kwa Hepatitis B ..maana yake unamaambukiz ya Hepadna Virus ..
mkuu hayo ni maelezo kutoka kwa Docta ,kama unajua toa msaada

Sent using Jamii Forums mobile app
ARVs ni anti retroviral Dawa mahususi za kuzuia HIV .. Unajua kwann umepimwa na HIV?? Ni kwasababu ni Co-infenctions yaan Ni rahisi kumkuta mwenye HIV ana HBV lkn sio lazima mwenye HBV awe na HIV.


Sasa kwann unatumia ARV za HIV?? Kwa sababu HBV yeye kama yeye hana Dawa, Ila katika kufanya utafiti ikaonekana Dawa za ARVs mahususi kwa HIV zinauwezo wa kumzuia HBV asizidi kuzaliana nahatimaye kufutiliwa mbali na kinga ya mwili.



Ndio sababu, ARV zinatumika ..nakama ni acute nirahisi kupona kama utafuata Mashariti kwa muda huo wote .
 
Nikweli ulichosema... Nami nmesema ni acute kwa sababu kwanza ya aina ya vipimo vilivyotumika vinavyodetect IgM against HBV .. IgM Mara nyingi ni Marker wa Acute infection au Past infection.

Haya mambo hayana uzoefu, ni lazima vipimo kutoka maabara viseme na vile vile historia ya mgonjwa, kama ndo kwanza ameambukizwa basi ni lazima atakuwa na dalili za kuumwa lkn kama chronic huwa mara nyingi hamna dalili mpaka ini likishambuliwa na kuja kushtuka muathurika ana saratani ya ini, na hapi ni mwisho kwani saratani ya ini haina dawa.

Sasa nimechagua acute ,kwa sababu naamin angekua ni Chronic wala asingeenda kwa lengo LA chanjo ,Bali angeenda kutafuta huduma sababu ya dalili ambazo zinamnyemelea nahuko ndiko angeambiwa 'Kutokana na moja mbili, umegundulika una Hii"

Lkn hapa , mtoa mada anaonekana hakua na shaka ,wala hakua anaumwa wala hakua anajisikia chochote Bali kaenda kupata chanjo, na sababu ya utaratibu wa chanjo kumlazim kupima ndio sasa akashikwa na butwaa.

Ipo hivi Mtu aliye katika acute stage ya HBV au HIV anakua Mara nyingi ni asymptomatic .( haoonyeshi Dalili) Ndo maana nimesema kwa uzoefu.
 
Mkuu achana na hayo ma -ARVs...
Hepatitis B ikiwa kwenye stage ya awali inaponywa kwa lishe tu. Piga lishe Safi halafu nenda kapime baada ya muda utakuja niletea ushuhuda hapa.

Mimi nimewahi pima na nikawa negative nikapata hizo sindano za chanjo tatu ... Ya mwisho namalizia mwezi January mwakani. Huyo daktari niliongea nae Sana kwanini wanatoa ARVs ... Wanatoa Kama supplement ya lishe kwa mgonjwa ambae Hana uwezo wa mlo kamili ... Ila Kama una uwezo lishe kamili hauna haja ya kumeza hayo madawa.

Nakushauri ongea na Huyo daktari wako Kama iko kwenye stage ya awali upige mlo kamili ... Hizo ARVs ndugu yangu sitaki kuelezea Sana ila Kama ungejua side effects zake usingetaka hata zisikia.

Fuatilia vifo vingi vya wanaotumia wanakufa kwa either mapafu, ini, figo n.k

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu hapa washaanza kumpoteza mwenzao..... Mkuu fuata ushauri wa daktari....... Usicheze na hilo jitu....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom