Nimependana na mwanamke wa ajabu

Nimependana na mwanamke wa ajabu

kenny mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2021
Posts
322
Reaction score
902
Wakuu poleni na miangaiko ya hapa na pale nimependa niwape mkasa ulionipata Jana.

Npo mtaa x sasa Jana jioni kuna sehemu nilikuwa naenda sasa njiani nikakutana na demu mmoja mkali kinoma ana shape kama lote kwa ujasiri nilionao ikabidi nimsimamishe nikaanza kuongea nae uwa natumia swaga ya kuwaambia mademu kuwa kama nakufahamu au nimekufananisha then demu akirespond ameingia cha kike.

Kweli demu akawa ana-respond akisema unanifananisha na nani basi nilifanikiwa kuchukua namba then jioni nikawasiliana nae sasa Leo asubuhi nikamuomba appointment demu akawa anakaata nikafosi hadi akakubali basi tulipanga tuingie swimming sehemu flani Mbezi,
Nipo na demu kila ninachomnunulia anakataa yaani demu hataki nitumie hata mia kwaajili yake.

Basi tumeenda swimming tumeoga then tumerudi. My point kukatisha stori ni kwamba demu hapendi hela na ananijali sana nisitumie hela kwaajili yake nilinunulia chakula kwa kulazimisha hadi akakubali pia nimemtongoza demu kakubali japo aliniuliza maswali magumu magumu na future yangu kwake nikashinda mtiani so my swali hivi kumbe kuna wanawake ambao hawapendi hela siku hizi?

Kwenye kupiga stori ameniambia babaake ni MTU mkubwa sana serikalini lolooo!

Wakuu demu mpole kinoma halafu pisi Kali aiseee huu asipobadilika namuoa j3 ijayo
 
Mhhhh babayake mkubwa serikalini afu mwanae azurule mitaani hovyo au ulikutana nae Msasani huko. Hio gear tu anaona aibu kuanza kukuchuna ngoja siku kadhaa zipite kama hutosikia mara baba katumbuliwa saivi hali imekuwa ngumu naomba hata 30k nikanunue sijui nini

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom