Smt016
JF-Expert Member
- Jan 11, 2016
- 2,287
- 3,019
Kwanzia mashindano ya Mapinduzi yaanze, Gamondi wala haumizi kichwa juu ya mashindano hayo, squad yake imesheeni watoto wa Yanga B na wachezaji wasiopata namba kwenye kikosi cha Yanga. Mapinduzi cup ni bonanza lisilo na maana wala faida yoyote ile zaidi ya kisiasa, hata ikitokea Yanga wamekutana na timu ngumu au yenye ubora kama Simba, Azam au Singida, ni vyema kocha aachwe abakie na mtazamo wake huo huo pasipo kupewa presha yoyote na mashabiki, au viongozi ili kushinikiza wapangwe wachezaji wa first eleven. Hata Yanga ikifungwa, ifungwe ila squad ibakie vile vile tu.