Malingumu
JF-Expert Member
- Apr 5, 2012
- 616
- 429
Jambo la kuomba ili upate mwenzi wako huwa wakati mwingine ni gumu na si rahisi sana kuamini miongoni mwa vijana wengi.Je ushawahi kuota ndoto yenye sauti elekezi? Hii ni aina ya ndoto ambayo mtiririko wote wa matukio katika ndoto huongozwa na sauti fulani,this is what happened to me! Wakati nasoma kidato cha nne siku moja nilioteshwa hii ndoto; nilioneshwa wadada wa3 wakiwa wamesimama,kiurefu dada wa katikati alikuwa mrefu kushida wale wawili wa pembeni yake,ile sauti elekezi ilinielekeza kwamba "wawili kati ya watatu hawa wataondoka" na kweli wale wadada wawili pembeni ya dada yule mrefu wakaondoka na hatimaye akabaki yule mrefu kuzidi wale wawili aliyesimama kati yao,ile sauti ikanijia tena na kuniambia"huyo aliyebaki hapo ndiye atakayekuwa mke wako wa maisha" baada ya pale nikastuka kutoka usingizini.Tangu pale huwa namwomba Mungu anisaidie nimpate yule binti(mrefu,mweupe afu mrembo).nilipojiunga na chuo siku moja nilimwona yule binti,sijawahi kumuongelesha na cha ajabu huwa hana mpango na mimi hata interest kisalamu.kiniumizacho zaidi jamaa yangu huwa anamzungumzia yule binti na kusema kuwa si punde atamtokea,hilo linanipa headeche kwamba sijui nimuhawi au nizidi kusubiri nikijiaminisha kwamba jamaa atakataliwa nami nitamkaribia yule binti kwan itakuwa ni ishara mojawapo kuwa ni wangu!! (Nakaribisha maoni wadau!!)