Nimeoneshwa kuwa ni mwenzi wangu!!

Malingumu

JF-Expert Member
Apr 5, 2012
616
429
Jambo la kuomba ili upate mwenzi wako huwa wakati mwingine ni gumu na si rahisi sana kuamini miongoni mwa vijana wengi.Je ushawahi kuota ndoto yenye sauti elekezi? Hii ni aina ya ndoto ambayo mtiririko wote wa matukio katika ndoto huongozwa na sauti fulani,this is what happened to me! Wakati nasoma kidato cha nne siku moja nilioteshwa hii ndoto; nilioneshwa wadada wa3 wakiwa wamesimama,kiurefu dada wa katikati alikuwa mrefu kushida wale wawili wa pembeni yake,ile sauti elekezi ilinielekeza kwamba "wawili kati ya watatu hawa wataondoka" na kweli wale wadada wawili pembeni ya dada yule mrefu wakaondoka na hatimaye akabaki yule mrefu kuzidi wale wawili aliyesimama kati yao,ile sauti ikanijia tena na kuniambia"huyo aliyebaki hapo ndiye atakayekuwa mke wako wa maisha" baada ya pale nikastuka kutoka usingizini.Tangu pale huwa namwomba Mungu anisaidie nimpate yule binti(mrefu,mweupe afu mrembo).nilipojiunga na chuo siku moja nilimwona yule binti,sijawahi kumuongelesha na cha ajabu huwa hana mpango na mimi hata interest kisalamu.kiniumizacho zaidi jamaa yangu huwa anamzungumzia yule binti na kusema kuwa si punde atamtokea,hilo linanipa headeche kwamba sijui nimuhawi au nizidi kusubiri nikijiaminisha kwamba jamaa atakataliwa nami nitamkaribia yule binti kwan itakuwa ni ishara mojawapo kuwa ni wangu!! (Nakaribisha maoni wadau!!)
 
1.Una historia ya kuota ndoto alafu jambo hilo linakua la kweli

2.Huyo dada ulomwona umempenda au unafuata ndoto ilivyo kuelekeza?

3.Vipi kuhusu mienendo yake hapo chuo?inaridhisha?

4.What if hiyo ndoto ilitokana na mawazo yako ya muda mrefu au ya siku hiyo?


5.Sawa unaweza kupiga moyo konde ukamtokea what if akakukataa? Utajitosa kumwambia kua ulioteshwa?

Jipime then fuata moyo wako
 
Duuh, mimi nasema ni ndoto tu...sometimes ukiwa umeweka kitu akilini sana kwa muda inakuwa part of you, fantasizing, daydreaming and so forth. Wewe simply ulikuwa unaota matamanio yako kwa mwanamke unayemtaka maishani. Pagumu, vipi utamwingia huyo binti ikiwa mshikaji wako keshaonyesha ana nia hiyo, acha kwanza ajaribu bahati yake na wewe kwanza lazima uanze urafiki nae, aanzisha salamu uone kama anaingilika.

Otherwise, warefu na weupe ni wengi....
 
Duuh, mimi nasema ni ndoto tu...sometimes ukiwa umeweka kitu akilini sana kwa muda inakuwa part of you, fantasizing, daydreaming and so forth. Wewe simply ulikuwa unaota matamanio yako kwa mwanamke unayemtaka maishani. Pagumu, vipi utamwingia huyo binti ikiwa mshikaji wako keshaonyesha ana nia hiyo, acha kwanza ajaribu bahati yake na wewe kwanza lazima uanze urafiki nae, aanzisha salamu uone kama anaingilika.

Otherwise, warefu na weupe ni wengi....
poa madameX! Kwa maneno yako mfano la kuanza na salamu ni jema,kwan unanifanya nijaribu kutumia different schools of thoughts and different scholars mfano rostow kwa kusema kuwa maendeleo hayaji ghafla(it followS stages
) ngoja nijaribu kwa kuanza kudevelop courage ya salamu na mawasiliano may b 1 day yes!
 
hta mi niliota afu akawa ndie....na ujue kama ndie atakuwa tu, hata usipomtokea leo wala kesho,lzm kuna mazingira yatawafanya/yatatokea ya kutimiza ndoto...gud lucky
 
1.Una historia ya kuota ndoto alafu jambo hilo linakua la kweli

2.Huyo dada ulomwona umempenda au unafuata ndoto ilivyo kuelekeza?

3.Vipi kuhusu mienendo yake hapo chuo?inaridhisha?

4.What if hiyo ndoto ilitokana na mawazo yako ya muda mrefu au ya siku hiyo?


5.Sawa unaweza kupiga moyo konde ukamtokea what if akakukataa? Utajitosa kumwambia kua ulioteshwa?

Jipime then fuata moyo wako

Dah! Kweli !
 
poor you, kama unasoma UDSM kamuone padri Mbiku atakusaidia. ana kitabu cha mafundisho ya uchumba na ndoa, atakuelekeza jinsi ya kusali novena. (kama ni mkatoliki)
 
Kwa kawaida ndoto lazima ifanyiwe kazi, nakushauri fanyia kazi ndoto yako kama ni ya kutoka kwa Mungu itakuwa kweli kutimizwa. Mfuate mweleze kama ni huyo msichana aliyekuwa katika ndoto.
 
we ucamin sana ndoto,cku ukiota umependwa/umependa jini je?ucwekee too much faith kwenye ndoto.
 
Jambo la kuomba ili upate mwenzi wako huwa wakati mwingine ni gumu na si rahisi sana kuamini miongoni mwa vijana wengi.Je ushawahi kuota ndoto yenye sauti elekezi? Hii ni aina ya ndoto ambayo mtiririko wote wa matukio katika ndoto huongozwa na sauti fulani,this is what happened to me! Wakati nasoma kidato cha nne siku moja nilioteshwa hii ndoto; nilioneshwa wadada wa3 wakiwa wamesimama,kiurefu dada wa katikati alikuwa mrefu kushida wale wawili wa pembeni yake,ile sauti elekezi ilinielekeza kwamba "wawili kati ya watatu hawa wataondoka" na kweli wale wadada wawili pembeni ya dada yule mrefu wakaondoka na hatimaye akabaki yule mrefu kuzidi wale wawili aliyesimama kati yao,ile sauti ikanijia tena na kuniambia"huyo aliyebaki hapo ndiye atakayekuwa mke wako wa maisha" baada ya pale nikastuka kutoka usingizini.Tangu pale huwa namwomba Mungu anisaidie nimpate yule binti(mrefu,mweupe afu mrembo).nilipojiunga na chuo siku moja nilimwona yule binti,sijawahi kumuongelesha na cha ajabu huwa hana mpango na mimi hata interest kisalamu.kiniumizacho zaidi jamaa yangu huwa anamzungumzia yule binti na kusema kuwa si punde atamtokea,hilo linanipa headeche kwamba sijui nimuhawi au nizidi kusubiri nikijiaminisha kwamba jamaa atakataliwa nami nitamkaribia yule binti kwan itakuwa ni ishara mojawapo kuwa ni wangu!! (Nakaribisha maoni wadau!!)


afu utaota tena kabla ya kumchukua rafiki yako atajisevia, baada ya kumtumia we ndo utampiga kanzu afu ndo awe mkeo. usijali subiri ajisevie kwanza, kama unahisi hauna vitamkwa (maneno ya kumuimbisha)
 
unankumbusha swaiba wangu mmoja nae kamaliza ud 2006... alikuwa na mdada mmoja ambaye kwao unaweza kusema ndipo zinapotengezezwa noti nadhani mnanielewa namaanisha nn... jamaa yeye alikuwa kama wenzangu na mimi, nyumbani kawaida sanaaaa..... walidumu na yule dada miaka tisa kwenye mahusiano.... kila mtu aliwachukulia kama mfano wa kuigwa kwenye mahusiano, maana walipendana na walishibana haswa... walipitia vikwazo vingi sana ikiwa pamoja na kukataliwa na wazazi wa dada lakini bado walimudu... ajabu wakati wametafuna ng'ombe wote umebaki mkia dada akamwaga yule kaka wakiwa mwaka wa mwiso chuoni udsm, na walipanga soon wakimaliza wafunge ndoa... kaka aliugua akalia akawa hana hamu... ikawa ibada kwa sana, na kuokoka akaokoka...
katika kuokoka kwake akaoteswa ndoto kama yako kuwa kuna mdada anamtoke na kumwambia kuwa yeye ni mwenza wa maisha... ajabu na mama huko kijana pia akaota ndoto kama hiyo kwa msichana huyohuyo sema aliota wamefunga ndoa tayari na mwanae..... jamaa akajiambia kama ni yeye ntampata tu.... walikutana supermarket siku moja town and it was the same dat jamaa alimtamkia dada kuwa anampenda, na dada alikubali hapo hapo bila swali na sasa wamefunga ndoa wanaishi kigamboni dar es salaaa....
inaweza kuwa mungu anazungumza nawe pia kwa njia hiyo......
 
Mkuu Mungu ni 'Almighty' halafu 'He makes sure His word comes to pass'. Kama ni yeye kakuotesha basi uwe na amani kwa sababu hawezi kukuotesha ili upambane kumpata-He will bring her to you. Kama sie yeye kuwa na amani pia...
 
frankly speaking, me kuna ndoto niliota last wiki na leo imenitokea hivo hivo.... mara nyingi me huwa nikiota kitu flani ambacho ckuwa nimekiwaza wala kukifanya last time huwa chatokea...mf.nikiota maji kama mto,ziwa,bahari kama kuna mpango nafatilia huwa hautimii kabisa... so huwa nakata tamaa kabisa!
 
jaribu kuwahi kumtokea-maana wakati ndo huu-baada ya chuo mambo yanaparangika sana-
we mtokee maana ndoto yako haijakwambia lini umtokee
 
Back
Top Bottom