Mdude_Nyagali
Member
- Dec 11, 2022
- 60
- 1,237
Ndugu watanzania wenzangu wavuja jasho wa nchi hii, hiyo sauti mnayoisikia ni ya katibu tawala DAS wilaya ya Mbongwe mkoani Geita akiiba mafuta ya serikali kwenye moja ya vituo vya mafuta vilivyopo wilayani hapo.
Tukio hili limetokea January 2024 katika kituo cha mafuta kiitwacho Minzingo kilichopo Masumbwe wilayani Mbongwe.
Katika sauti hii DAS huyo anasikika akimuambia mhudumu wa kituo cha mafuta ampe pesa kash Tsh. 235,000/- kutoka katika fungu la mafuta ya serikali. Mhudumu anamjibu DAS huyo kuwa yeye kama mhudumu anaruhusiwa kutoa mafuta na sio pesa. Lakini Katibu tawala huyo mr. Jacob Rombo anamlazimisha mhudumu huyo ampe pesa hizo huku mhudumu akihofia kupoteza kazi kwani kitendo hicho ni kinyume na maadili yake ya kazi. Baadaye mhudumu huyo analazimika kumpa pesa hiyo huku akiwa na wasiwasi na katibu tawala huyo akijaribu kumfariji na kumtania kumuita shemeji.
Kitendo hiki kimeuumiza moyo wangu ukizingatia kwamba kabla ya uteuzi wa katibu tawala huyu kulikuwa na (mchujo) vetting. Nasikitika kwamba Samia alijua ameteuwa mtu mchapakazi ambaye anaenda kumsaidia kazi yake kule Mbongwe kumbe kateuwa jambazi linaloenda kuhujumu uchumi wa nchi. Bado najiuliza idara ya Usalama wa taifa ilikuwa wapi kumshauri Samia kuhusu uteuzi wa katibu tawala huyu mwizi na jambazi wa mali za umma? Idara ya Usalama wa taifa pale Mbongwe wanafanya kazi gani kiasi kwamba wizi wa mali za umma namna hii hawajui?
Katika mazingira haya, mimi kama mwanaharakati na mdau wa utawala wa sheria na uwajibikaji nazitaka mamlaka zinazohusika kutengua uteuzi wa katibu tawala huyu. Pili akishatenguliwa haraka sana akamatwe na kufanyiwa ukaguzi ili kujua hayo mafuta ameiba kwa muda gani na afikishwe mahakamani.
Hatuwezi kukaa kimya wakati wananchi wanalia na gharama kubwa za matibabu halafu kuna DAS mmoja anakunja laki 2 kila siku za wizi wa mafuta ya serikali.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.
Tukio hili limetokea January 2024 katika kituo cha mafuta kiitwacho Minzingo kilichopo Masumbwe wilayani Mbongwe.
Katika sauti hii DAS huyo anasikika akimuambia mhudumu wa kituo cha mafuta ampe pesa kash Tsh. 235,000/- kutoka katika fungu la mafuta ya serikali. Mhudumu anamjibu DAS huyo kuwa yeye kama mhudumu anaruhusiwa kutoa mafuta na sio pesa. Lakini Katibu tawala huyo mr. Jacob Rombo anamlazimisha mhudumu huyo ampe pesa hizo huku mhudumu akihofia kupoteza kazi kwani kitendo hicho ni kinyume na maadili yake ya kazi. Baadaye mhudumu huyo analazimika kumpa pesa hiyo huku akiwa na wasiwasi na katibu tawala huyo akijaribu kumfariji na kumtania kumuita shemeji.
Kitendo hiki kimeuumiza moyo wangu ukizingatia kwamba kabla ya uteuzi wa katibu tawala huyu kulikuwa na (mchujo) vetting. Nasikitika kwamba Samia alijua ameteuwa mtu mchapakazi ambaye anaenda kumsaidia kazi yake kule Mbongwe kumbe kateuwa jambazi linaloenda kuhujumu uchumi wa nchi. Bado najiuliza idara ya Usalama wa taifa ilikuwa wapi kumshauri Samia kuhusu uteuzi wa katibu tawala huyu mwizi na jambazi wa mali za umma? Idara ya Usalama wa taifa pale Mbongwe wanafanya kazi gani kiasi kwamba wizi wa mali za umma namna hii hawajui?
Katika mazingira haya, mimi kama mwanaharakati na mdau wa utawala wa sheria na uwajibikaji nazitaka mamlaka zinazohusika kutengua uteuzi wa katibu tawala huyu. Pili akishatenguliwa haraka sana akamatwe na kufanyiwa ukaguzi ili kujua hayo mafuta ameiba kwa muda gani na afikishwe mahakamani.
Hatuwezi kukaa kimya wakati wananchi wanalia na gharama kubwa za matibabu halafu kuna DAS mmoja anakunja laki 2 kila siku za wizi wa mafuta ya serikali.
Mdude Nyagali 7 x 70 Sumu ya Nyigu.