Nimemsamehe mapema

Nimemsamehe mapema

ELNEY

Senior Member
Joined
Aug 10, 2017
Posts
106
Reaction score
48
Habari wana jukwaa pendwa la jf..
Habari za usiku huu tulivu ...
Nilitamani mda mwingi sana kujiunga na hili jukwaa lakini nikawa naishia kusoma tuu wala sikuwa member kuanzia miaka miwili nyuma imekata..

Wacha niende kwenye mada jamani miaka karibu minne mpaka sasa hivi huko awali niliwahi kuwa kwenye mahusiano na binti mmoja ambaye kwa sasa ni single mother

KWENYE mahusiano yetu Mimi na huyoo mdada hapo awali kabla ya kuachana naye aisee huyoo binti jamani...mpaka basi hadi sasa naandika hapaa moyo wangu bado upo kwake kabisa ....

Picha linaanza mwaka wa pili wa mahusiano kwa kua nilimpenda nikamuomba kuwa tuwe wapenzi wa kudumu kabisa na hatimaye ndoa Mungu akijalia ila yeye alishauriana na mama yake juu ya mpango huo mama yake akawa anapinga kwa maana kuwa family yetu kiwango kikubwa wasomi pili umri wetu Mimi na binti huyoo unafanana kwaio mama yake aliadhimia kwa binti yake hadi kumpa maneno magumu kuwa nisikuone kule kwa yule mwanaume anataka kukulaghai tuu ..

Wakati huo mwaka wa kwanza wa mahusiano mama yake hakujua ila zilipoanza story za ndoa ndio zogo lilianza na mama yake akawa anahisi kuwa nataka kumalaghai binti yake ..

Niliumia sana kusikia hivyoo haikupita mda binti alipewa ujauzito na mwanaume mwingine kwaio mwanaume akawa anatunza mimba wakati huo mtaa tuliokuwa tunakaa binti alihama akahamia kwingine kabisa ..

Lakini hiyoo story haikuvuma kabisa kiwa binti anaujauzito mana mama wa yule binti alikua anaficha iwe siri aliondoka pale binti akiwa na ujauzito wa miezi miwili huko alipo tulikua tunaendelea kufanya mawasiliano licha ya Kuwa yupo kwa bwana ...

Moto unaanza bwana aliyempa ni dereva tena dereva wa mkoa full kuzurura home hakaliki matumizi shidaa binti akawa ananitafuta ELNEY naomba hela ya matumizi Mimi nikawa namsaidia nisijue Mke wa mtu nikawa namsaidia kwa sababu nampenda ..

Kufupisha story mwisho wa siku binti alirudi kwa mama yake na kuanza kulalamika kuwa maisha magumu na mwanaume full michepuko. ..mama akampokea binti yake maisha yakasonga ila

Mimi mawasiliano hayakufa yalikua kama kawaidaa na mwishoe akaomba turudiane kama wapenzi nikakubali mana alikua bado yupo kwenye nafsi yangu..

Mama mazazi wa binti kwa Mara ya pili bado anamwambia binti yake kuwa huyoo mwanaume anakupenda kweli amekubali kirahisi kukusamehe tuu huyoo anataka kukurudishia kisasi na wewe

Waungwana Mimi Sina lengo baya na huyu binti bado nampenda sana na kwa sasa nimempa mtaji wa laki Sita mana yeye fundi cherehani na kafungua ofisi yake na anawafunzi watatu ...

Mwenye ushauri jamani binti haamini kama kweli nampenda anahisi nataka kurudisha kisasi ...
 
PIA MAMA YAKE ANASEMA KUWA SURA YAKE ATAIWEKA WAPI MANA MARA YA KWANZA ALIKATAA BINTI YAKE KUOLEWA NA MIMI SAIZI NTAMUONAJE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuma washenga wapeleke barua,lakini pia uwe makini na huyo single mother,yaan anakufanya chaguo la pili,je mambo yasingekuwa magumu angerudi? Nawewe una take advantage ya njaa yake kumvuta kimapenzi,bado hapajatulia hapo,

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu.sio njaa tuu hali ya kumsaidia ilikua tangu mwanzo kabisa
 
Ppita zako hvi katafute wife material maana kama n upendo wa dhat asinge kubal kuwa na uyo jimwanaume n kama mim nkpenda nmependa stak ushaur wa mzaz wa kunvurugia
 
Ppita zako hvi katafute wife material maana kama n upendo wa dhat asinge kubal kuwa na uyo jimwanaume n kama mim nkpenda nmependa stak ushaur wa mzaz wa kunvurugia

Sawa mkuu umesomeka haina shidaaa
 
kijana wew bado ni mdogo, mtafute mwingine fresh from home, hao masingle madhaz wana changamoto sana, akija mwenye mtoto inakuwa ishu
 
To be honest naweza kukwambia kwamba uusikilize moyo wako unataka nini kwa uyo dada na pia mshirikishe sana Mungu katika kila stege unayopitia. Inawezekana uyo akawa mke wako au la. All the best
 
To be honest naweza kukwambia kwamba uusikilize moyo wako unataka nini kwa uyo dada na pia mshirikishe sana Mungu katika kila stege unayopitia. Inawezekana uyo akawa mke wako au la. All the best

Unachokisema kweli

Mana moyo wako bado upo na yeye

Ila changamoto kubwa yeye hiyoo na mama yake
 
Swali la Kizushi.

Bado Mjamzito?

Au ameshajifungua?

Jibu kwanza Suali langu ili nipate kukusaidia.

Maana hapo kwenye Ujauzito hukufunguka tena.

Ni kama kuna kitu fulani unakificha.

Hebu funguka kwanza
 
Kaa na mama yake na huyo binti akiwemo ongea nao kuwa huna lengo baya la kuwafanyia, na unampenda binti yake na upo tayari kuishi naye kwa namna yeyote ile, kikubwa ni kwamba mama mkwe anaonekana hapendezwi na wewe sasa jaribu kutafuta muda ukae naye umueleweshe tena kwa ushawishi nadhani atakuelewa kwa sababu yeye ni mtu mzima.
 
yaelekea we ni fogo,maana kwa jinsi unavyojitolea hiyo misaada ni kwamba una hali nzuri kiuchumi.
 
Unachokisema kweli

Mana moyo wako bado upo na yeye

Ila changamoto kubwa yeye hiyoo na mama yake
Kama ni changamoto ni mama yake basi unaweza mkaongea mkayamaliza ya naweza kana ila jua kua kuna mapenzi na upendo unaweza ukamchukua na kumuona kwa sababu ya mapenzi and then yakaja kuisha. Na mkaachana na pia kama una upendo ni her pia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
aisee ukiona wazaz hawatak mwanao aolewe na mtu wala usilazimishe! kwanza huyo mama anaoneka yupo kimaslahi! na bint kakurudia wewe kwasababu kwakwe kuchungu! sema ndo hvyo umezama penzini ngumu kunielewa! akitokea kibosile mmoja mama atamuuza mwanae tena kwa kibosile ww kazi yako kula makombozi!... binafs naogopa wakwe km hao! pole!

na sasa hv mama lazima awe na kaadab kwasabb umempa mtaj binti yake! yaan ww utakuwa wakuendeshwa till u die na huyo mama!
 
Back
Top Bottom